Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2460; Lazima kuna mtu ataumia.

By | September 25, 2021

2460; Lazima kuna mtu ataumia. Kwenye moja ya vitabu ambavyo nimekuwa narudia kusikiliza mara kwa mara, How To Be A Billionaire, mwandishi anasema ukifanikiwa kutengeneza utajiri wa mabilioni, utakuwa pia umefanikiwa kutengeneza maadui wakubwa. Kwa kifupi ni hakuna namna utaweza kufanikiwa bila ya kuwaumiza baadhi ya watu kwa namna fulani, (more…)

2459; Siku Gani?

By | September 24, 2021

2459; Siku Gani? “Ipo siku yangu na mimi nitafanya makubwa.” Sawa, tunakubaliana na wewe, lakini tuna swali kidogo; “ni siku gani hiyo?” Kama huwezi kutujibu swali hilo, tafadhali usituhangaishe, kama umechagua kujidanganya mwenyewe ni sawa kwako, ila kuchagua kutudanganya na sisi siyo sawa. Siku moja haijawahi kutokea, siku ambayo haijatajwa (more…)

2457; Matumizi Ya Teknolojia Mpya.

By | September 22, 2021

2457; Matumizi Ya Teknolojia Mpya. Kila wakati huwa kuna teknolojia mpya ambazo zinavumbuliwa. Teknolojia hizo huwa zina nguvu ya kuleta mabadiliko makubwa na hivyo kuonekana ni fursa nzuri. Watu wengi hukimbizana na teknolojia hizo mwanzoni, ili kuzihodhi wakiona ndiyo namna ya kunufaika nazo. Lakini mwisho wa siku wanaofaidika sana siyo (more…)

2456; Kujaribu.

By | September 21, 2021

2456; Kujaribu. Mbwa huwa hajaribu kubwa mbwa, bali anakuwa mbwa. Kadhalika ukipanda mahindi, mche unapoota haujaribu kuwa mhindi, bali unakuwa. Kila kitu kwenye asili tayari kina uwezo na upekee ndani yake. Kinachopaswa kufanya siyo kujaribu bali kuwa. Hakipaswi kuiga vitu vingine bali kinapaswa kuwa kilivyo. Lakini inapokuja kwetu binadamu, pamoja (more…)

2455; Siyo lazima ujibu.

By | September 20, 2021

2455; Siyo lazima ujibu. Matatizo na changamoto nyingi tunazopitia kwenye maisha, chimbuko lake ni midomo yetu, tunaongea wana na kuongea hovyo. Mtu anaweza kufanya jambo, likakukera au kukuudhi, maneno yanaanza kukutoka ambayo yanazidi kuharibu kuliko kujenga. Mtu anaweza kukujibu vibaya na wewe ukasukumwa kumjibu vibaya zaidi. Maneno ni upepo mtupu, (more…)

2454; Ukitaka sana kitu, unakifukuza.

By | September 19, 2021

2454; Ukitaka sana kitu, unakifukuza. Pale unapokuwa unakitaka sana kitu na kutaka kukipata kwa wakati unaotaka wewe mwenyewe, huwa inakuwa vigumu zaidi kukipata. Utakazana na kulazimisha sana ukipate, utatumia kila aina ya njia. Lakini kadiri unavyohangaika ili kukipata, ndivyo kinakwenda mbali na wewe. Cha kushangaza sasa, pale unapokuwa hakitaki sana (more…)

2453; Ukiwa huna cha kupoteza.

By | September 18, 2021

2453; Ukiwa huna cha kupoteza. Umewahi kugundua kwamba ukiwa na fedha huwa hazikosi matumizi? Na ukiwa huna fedha bado maisha hayasimami? Yaani ukiwa na fedha, utashangaa zinatumika na bado yale mahitaji muhimu uliyonayo yanakuwa hayajaisha. Kadhalika ukiwa huna fedha, hata kama una mahitaji mengi kiasi gani ambayo hujaweza kuyatimiza, bado (more…)