Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2450; Hakuna Aliyekamilika.

By | September 15, 2021

2450; Hakuna Aliyekamilika. Sisi binadamu tuna changamoto na mapungufu mbalimbali. Hivyo ndivyo asili yetu ilivyo. Kama ilivyo kwamba ndege ni usafiri mzuri na wa haraka, ila ajali yake ni hatari kubwa sana. Inawezekana kabisa kutengeneza ndege ambayo ni salama kwenye ajali, lakini haitaweza kuruka hewani. Ni kanuni ya asili kwamba (more…)

2448; Ukiwa njia panda, chagua kazi zaidi…

By | September 13, 2021

2448; Ukiwa njia panda, chagua kazi zaidi… Pale unapojikuta njia panda, ukiwa hujui uchague kipi kati ya vingi vilivyo mbele yako, mara zote chagua kile kinachotaka kazi zaidi. Najua hili ni kinyume na wengi tunavyofikiri na kuamua. Huwa tunakimbilia kuchagua kile ambacho ni rahisi na hakihitaji kazi zaidi. Na hiyo (more…)

2447; Hakuna Kuchelewa.

By | September 12, 2021

2447; Hakuna Kuchelewa. Safari ya mafanikio huwa haina kuchelewa. Wakati wowote ambapo mtu unaamua unayataka mafanikio, ndiyo wakati sahihi kwako kuyafanyia kazi na kuyapata. Wapo ambao huona kwa sababu umri umekwenda na wamechelewa kujitambua kwenye eneo la mafanikio basi hawawezi tena kupata mafanikio makubwa. Hiyo siyo kweli, kama tu unaweza (more…)

2446; Nia njema huishia pabaya…

By | September 11, 2021

2446; Nia njema huishia pabaya… Kila mtu anayefanya jambo lolote lile, huwa anakuwa na sababu za msingi kabisa za kulifanya na huwa analifanya kwa nia njema kabisa. Hata kama kwa nje jambo hilo linaonekana ni la hovyo na la kijinga, sivyo anavyoona mfanyaji. Yeye anakuwa amefikiri na kufanya maamuzi ambayo (more…)

2444; Hakikisha Una Pa Kusimama.

By | September 9, 2021

2444; Hakikisha Una Pa Kusimama. Utegemezi uliopitiliza kwa wengine ndiyo kitu kinachowayumbisha wengi na kuwazuia kupata mafanikio makubwa. Ni kweli unawahitaji sana wengine na ushirikiano wao ni muhimu kwa mafanikio yako. Lakini kama unawategemea wengine kwa kila kitu na huna pa kusimama mwenyewe, unakuwa kwenye hatari kubwa. Unapowategemea wengine kwa (more…)

2443; Unahitaji kufikiri kwa utofauti.

By | September 8, 2021

2443; Unahitaji kufikiri kwa utofauti. Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema ujinga ni kufanya jambo lile lile, kwa namna ile ile halafu kutegemea kupata matokeo ya tofauti. Unaweza kuona hii ni kauli ambayo haikuhusu, lakini hebu itafakari kwa kina. Kuna maeneo ya maisha yako ambayo umekuwa unapata matokeo yale yale, japo (more…)

2442; Barabara lazima zifagiliwe.

By | September 7, 2021

2442; Barabara lazima zifagiliwe. Pata picha kama hakungekuwa na watu wanaofanya usafi kwenye barabara tunazotumia. Au hakuna watu wanaoondoa takataka kwenye mazingira yetu. Au hakuna watu wanaolima chakula tunachohitaji sana. Kwa hakika maisha yangekuwa magumu, bila ya kujali mtu una fedha kiasi gani. Ninachotaka kusema hapa ni hiki, kila kazi (more…)

2441; Kukata tamaa…

By | September 6, 2021

2441; Kukata tamaa… Kila mmoja wetu huwa anakutana na hali ya kukata tamaa katiks nyakati tofauti tofauti za maisha yake kulingana na kile anachokuwa anapitia. Hali hii ya kukata tamaa haisababishwi na kile ambacho mtu unapitia, bali inasababishwa na namna mtu unatafsiri kile unachopitia. Kuna mtazamo unaokuwa nao kuhusu unachopitia, (more…)