Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2420; Kuna watu wananufaika hata kama

By | August 16, 2021

2420; Kuna watu wananufaika hata kama hawakuambii… Tatizo kubwa kwenye maisha, hasa kwenye safari ya mafanikio ni upweke utakaokutana nao. Mara kwa mara utajikuta kwenye hali ya upweke, ukijiona uko mwenyewe kwenye mapambano unayoendesha. Katika nyakati hizo ndiyo mawazo ya kukata tamaa hukujia, yakikushawishi kwamba hakuna anayejali. Lakini mimi nataka (more…)

2419; Kwa nini ukweli ni mgumu kufikiwa…

By | August 15, 2021

2419; Kwa nini ukweli ni mgumu kufikiwa… Ni vigumu kuufikia ukweli kwa sababu huwa haubembelezi. Ukweli hauangalii mtu anataka kusikia au kuona nini, unabaki kuwa ukweli. Ukweli hauna mbwe mbwe wala kelele, unasimama kwenye eneo sahihi. Sisi binadamu tunapenda mbwembwe nyingi, tunapenda vitu vinavyotusisimua. Hivyo tunahangaika na yale yasiyo kweli (more…)

2418; Kwa sababu maisha yako yote yanategemea

By | August 14, 2021

2418; Kwa sababu maisha yako yote yanategemea hapo… Huwa tunakipa kitu uzito kulingana na namna kinavyoathiri maisha yetu moja kwa moja. Kama maisha yanategemea zaidi kitu fulani, basi tunakipa kitu hicho kipaumbele cha kwanza. Ndiyo maana kwenye dharura, watu huwa tayari kufanya chochote ili tu kuokoa uhai wao. Hivyo basi, (more…)

2417; Maamuzi ya kufa na kupona…

By | August 13, 2021

2417; Maamuzi ya kufa na kupona… Kuna maamuzi machache sana ambayo ukiyafanya kwenye biashara ni ya kufa na kupona. Kwa maana kwamba kuna hatari ya biashara kufa kabisa. Lakini maamuzi hayo ni machache mno. Maamuzi mengine mengi, pamoja na ugumu na umuhimu wake, yanaweza kurekebishika tu. Funzo ni nini hapa? (more…)

2416; Kuanzia chini ni kazi kubwa…

By | August 12, 2021

2416; Kuanzia chini ni kazi kubwa… Mimi siyo mfuatiliaji wa michezo kabisa, lakini kama ambavyo nimekuwa nasema, kuna mambo utayasikia tu hata kama siyo mfuatiliaji wa habari. Siku za hivi karibuni kumekuwa na mivutano kwenye timu kubwa za mpira Tanzania, hasa timu ya Simba ambapo kuna migogoro mbalimbali ya ndani. (more…)

2415; Zawadi na Adhabu…

By | August 11, 2021

2415; Zawadi na Adhabu… Kituo kimoja cha kulelea watoto (day care) kiliona baadhi ya wazazi wamekuwa na tabia ya kuchelewa kuwachukua watoto wao. Kituo hicho kikaamua kuweka adhabu ya faini kwa kila mzazi anayechelewa kumchukua mtoto wake. Lengo la faini hiyo ilikuwa ni kuondoa hali ya wazazi kuchelewa. Matokeo yakawa (more…)

2414; Ukishindwa, usiwajibie wengine…

By | August 10, 2021

2414; Ukishindwa, usiwajibie wengine… Nimekuwa nasema kama kuna kitu unatumia kama sababu ya kushindwa kupata unachotaka, lakini kuna mwingine ameweza kupata licha ya kuwa na hiyo wewe unaita sababu basi siyo sababu kweli, ni kisingizio tu. Moja ya dalili za kushindwa bila kukubali ni kuwa tayari kuwajibia wale walioweza, kwa (more…)

2413; Ubaya ni kusimama…

By | August 9, 2021

2413; Ubaya ni kusimama… Kitu pekee unachohitaji kwenye maisha ni kuwa kwenye mwendo. Haijalishi unakwenda kwa kasi kiasi gani, muhimu ni kuwa kwenye mwendo. Jambo baya kabisa kwenye maisha ni kusimama. Kwa sababu dunia haisimami, hivyo unaposimama unakuwa umechagua kurudi nyuma. Unapaswa kujikumbusha kwamba chochote cha maana unachotaka kwenye maisha (more…)

2412; Ubahili na Ufanisi…

By | August 8, 2021

2412; Ubahili na Ufanisi… Rasilimali zote muhimu huwa zina uhaba. Mahitaji huwa ni makubwa kuliko upatikanaji. Na hapo ndipo tofauti kati ya wanaofanikiwa na wanaoshindwa inapozaliwa. Wanaofanikiwa ni wale wanaoweza kutumia vizuri rasilimali muhimu zenye uhaba. Watu hao wanajua siri kubwa mbili ambazo wanazitumia vyema; uhaba na ufanisi. Kwenye uhaba (more…)

2411; Usiige Matumizi…

By | August 7, 2021

2411; Usiige Matumizi… Hakuna kitu rahisi kuiga kwa watu kama matumizi. Hicho ndiyo tunaona kwa nje na kujilinganisha nao kisha kukimbilia kuiga. Unapaswa kujua kitu chochote unachonunua kinapaswa kutokana na mahitaji yako kweli na siyo kwa sababu umeona wengine wanacho. Wala usinunue kitu kwa sababu unataka wengine wakuone na wewe (more…)