Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2380; Usiangalie walipo sasa, angalia

By | July 7, 2021

2380; Usiangalie walipo sasa, angalia walipotoka… Nimekuwa nasema na ninaendelea kusema kwamba ushauri mwingi unaotolewa na watu waliofanikiwa siyo ushauri sahihi kwa wale ambao bado hawajafanikiwa. Na sababu kubwa ni mbili. Moja ni vingi walivyofanya, siyo ambavyo jamii inaweza kuelewa, hivyo wakivieleza wataonekana ni watu wa ajabu. Hata kama siyo (more…)

2379; Wateja Bora Wa Biashara Yako…

By | July 6, 2021

2379; Wateja Bora Wa Biashara Yako… Wateja bora kabisa wa biashara yako ni wateja ambao walishanunua kwako na wakapata kile walichotegemea kupata. Hawa ni rahisi kuwashawishi wanunue tena kuliko kuwashawishi wateja ambao hawajawahi kununua kabisa. Hivyo unapofanya biashara yoyote ile zingatia vitu hivi vitatu muhimu na ambavyo vitaiwezesha biashara kufanikiwa (more…)

2378; Maamuzi Mapya Kulingana Na Taarifa Mpya…

By | July 5, 2021

2378; Maamuzi Mapya Kulingana Na Taarifa Mpya… Watu huwa hawapendi kukubali kama wamekosea. Hivyo watu wakishaonesha msimamo fulani, wataendelea na msimamo huo hata kama utawaonesha ushahidi mkubwa kwamba hawako sahihi. Hii ndiyo maana ubishani huwa hausaidii, kwa sababu kadiri unavyombishia mtu, ndivyo unazidi kumfanya asimamie upande wake. Maana alikubaliana na (more…)

2376; Vinavyozuia Biashara Kukua…

By | July 3, 2021

2376; Vinavyozuia Biashara Kukua… Kwa asili, kitu chochote kinachozaliwa kinapaswa kukua. Na kama hakikui basi kuna sababu, kuna kitu kinazuia. Kama mtoto amezaliwa na hakui, haongezeki uzito, hukai na kuridhika, lazima ujue sababu ni nini na kuchukua hatua. Hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa kwenye biashara pia. Biashara inapoanzishwa, inapaswa kukua. Kama (more…)

2375; Ni Mapendekezo, Siyo Amri…

By | July 2, 2021

2375; Ni Mapendekezo, Siyo Amri… Mawazo mengi yanayokuja kwenye akili yako huwa ni mapendekezo na siyo amri. Ni maoni na siyo ukweli. Akili yako ni kiwanda cha kuchakata mawazo ya kila aina. Na huwa yanabadilika kulingana na hali na mazingira yanavyobadilika. Mfano unaweza kuwa umepanga jukumu muhimu la kufanya, lakini (more…)

2374; Mrejesho Ni Zawadi…

By | July 1, 2021

2374; Mrejesho Ni Zawadi… Huwa kuna kauli kwamba zawadi ni zawadi, hakuna ndogo wala kubwa. Ukipewa zawadi unapaswa kushukuru. Moja ya zawadi ambayo mtu yeyote anaweza kukupa ni mrejesho kwenye kile unachofanya. Unapompata mtu anayeelewa kile unachofanya, na akawa tayari kukupa mrejesho kwenye kile unachofanya, hiyo ni zawadi ya kipekee. (more…)

2373; Usichezee ‘Matirio’…

By | June 30, 2021

2373; Usichezee ‘Matirio’… Kila kitu unachokutana nacho kwenye maisha yako, ni ‘matirio’ ambayo unaweza kutumia kuyafanya maisha yako kuwa bora zaidi. Usikubali kupoteza chochote unachokutana nacho, badala yake kitumie kwa namna yenye manufaa kwako. Huwa unakula chakula, kinaenda tumboni na kumeng’enywa, virutubisho muhimu vinafyonzwa mwilini na uchafu kuondolewa. Hivyo ndivyo (more…)

2372; Tunategemeana Sana…

By | June 29, 2021

2372; Tunategemeana Sana… Pata picha hii, Kumetokea janga kubwa kabisa duniani na watu wote wamekufa isipokuwa wewe mwenyewe tu ndiye umebaki hai. Kwa kifupi wewe ndiye unayeimiliki dunia, iko wazi kwamba utakuwa ndiye tajiri namba moja na pekee kwenye hii dunia, maana unamiliki kila kitu. Sasa hebu pata picha unawezaje (more…)