Category Archives: #TAFAKARI YA LEO

#TAFAKARI YA LEO; NYENZO…

By | August 1, 2021

Kwa juhudi zako pekee hutaweza kufanya makubwa. Lakini kwa kutumia nyenzo mbalimbali, juhudi zako ndogo zinakuzwa na kuzalisha matokeo makubwa. Tumia nyenzo kwenye kila eneo la maisha yako unalotaka kufanya makubwa. Mfano ukifanya kazi mwenyewe kwa masaa 10, unakuwa na hayo tu kwa siku. Ukiwa na watu 5 wanaokufanyis kazi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NGUVU HAIPOTEI…

By | July 31, 2021

Kanuni ya fizikia inasema nguvu haitengenezwi wala haipotei, bali inabadilishwa kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine. Unapokuwa na hisia kali, huwa zinachochea nguvu kubwa ndani yako, nguvu hiyo huwa haiishi yenyewe. Nguvu hiyo hukimbilia kuleta uharibifu kama haitatumika vizuri. Hivyo panga kabisa mambo utakayofanya pale hisia zinapoibua nguvu ndani yako ili (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MTU PEKEE UNAYEWEZA KUMRIDHISHA…

By | July 30, 2021

Kuna mtu mmoja tu unayeweza kumridhisha na kumfurahisha kwenye maisha yako. Mtu huyo ni wewe mwenyewe. Utajiridhisha kwa kuishi maisha ya kweli kwako na siyo kuishi maisha ya maigizo ili kuwaridhisha wengine. Haijalishi unafanya nini, wapo watu watakaokuona wewe ni takataka na hufai kabisa. Siyo kwa sababu yako, bali kwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NI HISIA…

By | July 29, 2021

Hisia zako ndizo zinahusika kwenye maamuzi yote unayofanya. Unaweza kujiambia umetumia fikra, lakini ulichofanya kwenye fikra ni kuzihalalisha hisia zako. Bila hisia ni vigumu sana kufikia maamuzi yoyote yale, maana utatumia muda mwingi kuchambua kila chaguo kililopo. Lakini kwa hisia utachagua kile unachopenda kisha kuhalalisha kwa fikra kwamba ndiyo maamuzi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UGUMU WA MABADILIKO…

By | July 28, 2021

Kama unataka kubadili matunda ambayo mtu unazalisha, kukata matawi hakutasaidia. Unapaswa kung’oa kabisa shina la mtu huo na kupanda mti mwingine. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye mabadiliko ya maisha yetu. Hutaweza kuyabadili maisha kwa kuhangaika na tabia pekee, bali anza kwa kubadili imani ya ndani yako. Tabia ulizonazo ni matokeo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUSHINDWA KABLA YA KUANZA…

By | July 27, 2021

Unayashindwa maisha, kazi au biashara kabla hata hujaanza kwa sababu unawaiga wengine. Unapofanya kama wanavyofanya wengine, watu wanakuwa hawana sababu ya kuja kwako. Unakuwa umewaambia kwamba wewe huna umuhimu wowote. Njia pekee ya kushinda ni kuwa wewe, wewe ambaye ni wa kipekee, ambaye hujawahi kutokea na hutakuja kutokea tena. Weka (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAAMUZI NA MATOKEO…

By | July 26, 2021

Usiunganishe moja kwa moja maamuzi unayofanya na matokeo unayopata. Maamuzi sahihi yanabaki kuwa sahihi hata kama matokeo yake ni tofauti na ulivyotarajia. Usikimbilie kubadili maamuzi kwa sababu matokeo siyo mazuri, badala yake badili mbinu unazofanyia kazi. Kuwa na mchakato wa kufikia maamuzi sahihi na pia kuwa na mchakato wa kufanyia (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WAJUE KUHUSU WEWE, ILA WASIKUJUE…

By | July 25, 2021

Mafanikio yana gharama kubwa. Na mafanikio yanapoambatana na umaarufu, yanakuwa na gharama kubwa zaidi. Wengi kabla hawajafanikiwa hutamani sana wapate umaarufu kwani huamini mafanikio yanayoendana na umaarufu ndiyo mazuri. Lakini wakishafanikiwa na kuwa maarufu ndiyo wanagundua jinsi hilo lilivyo mzigo mkubwa. Unapofanikiwa na kuwa maarufu unakuwa lengo la mashambulizi kwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; GIZA HALIDUMU MILELE.

By | July 24, 2021

Giza linapoingia, huwa hatuna wasiwasi kwamba huenda giza hilo likadumu milele. Tunajua kwa hakika kwamba kesho kutakucha, mwanga utakuna na giza kitapotea. Hivyo pia ndivyo maisha yetu yalivyo, kuna nyakati tunapitia magumu mbalimbali. Cha kushangaza huwa tunaona kama magumu hayo yatadumu maisha yetu yote. Ukweli ni hayadumu, ni kitu cha (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HUHITAJI TAARIFA ZAIDI…

By | July 23, 2021

Kwa chochote unachotaka kufanya, huhitaji taarifa zaidi ndiyo uanze. Tayari unazo taarifa za kukutosha kuanza kufanya. Ukijiambia unasubiri mpaka upate taarifa za kutosha, utakuwa unajidanganya. Unachopaswa ni kuanza kwa taarifa ambazo tayari unazo, na kisha kuendelea kujifunza kadiri unavyokwenda. Tunaishi kwenye zama za mafuriko ya taarifa, ni rahisi sana kuzama (more…)