Category Archives: #TAFAKARI YA LEO

#TAFAKARI YA LEO; MTU RAHISI KUMDANGANYA…

By | July 22, 2021

Richard Feynman aliwahi kusema jukumu letu la kwanza ni kutokujidanganya kwa sababu ni rahisi mno kujidanganya wenyewe. Hakuna mtu rahisi kumdanganya kwenye maisha yako kama wewe mwenyewe. Kwa vitu unavyotaka na hujapata, utatafuta kila sababu ya kukuridhisha, isipokuwa kuukabili ukweli. Utaangalia nini umekosa au ugumu gani unakabiliana nao. Lakini hutaangalia (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAFANIKIO NI HATUA…

By | July 21, 2021

Mafanikio hayatokei kama ajali au bahati. Bali ni hatua ambazo mtu unapiga, kutoka sifuri, kwenda moja, kisha kumi, mia na kuendelea. Wengi walio sifuri huwa wanataka watoke sifuri mpaka 100, kitu ambacho hakijawahi kutokea. Unatoka sifuri mpaka moja, hapo unajifunza mengi mno. Kisha unatoka moja mpaka 10 ambapo yapo ya (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MCHANGO WAKO KWENYE CHANGAMOTO…

By | July 20, 2021

Hakuna changamoto unayopitia ambapo wewe mwenyewe huna mchango katika kuisababisha au kuichochea. Kwa kila changamoto au magumu unayopitia, wewe una mchango. Hata kama unaona wengine ndiyo wanaohusika, kuna namna na wewe pia unahusika. Na uhusika wako mkuu huwa ni kukosa umakini kwenye kile unachofanya. Unapoweka umakini wako wote kwenye jambo, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WATU WENYE CHUKI…

By | July 19, 2021

Ni watu ambao hupaswi kuwaruhusu wakusumbue kwa namna yoyote ile. Kwa sababu mtu akiwa na chuki na wewe, tayari ana chuki na yeye binafsi. Hakuna namna unaweza kumlazimisha anayekuchukia akupende, maana yeye mwenyewe hajipendi. Watu wanaojipenda hawana muda wa kuwa na chuki kwa wengine. Na watu wenye chuki, hawana manufaa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAZURI NA MABAYA…

By | July 18, 2021

Yote huwa yanatokea, na siyo kwa kupenda au kutokupenda kwako, bali ni sehemu ya maisha. Lakini unapoweka mipango yako, huwa unaangalia mzuri yanayoweza kutokea na kuyasahau mabaya. Kinachotokea ni kuumizwa sana pale mabaya yanapotokea. Hupaswi kuruhusu kitu chochote kitokee kwa mshangazo kwako, yaani kitokee bila ya kutegemea kabisa. Tafakari matokeo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; BILA YA NAMBA…

By | July 17, 2021

Maendeleo na hatua zote ambazo tumepiga kama binadamu, ni kwa sababu ya mamba. Uwezo wa kupima na kulinganisha vitu umekuwa msukumo mkubwa kwetu kufanya vitu kwa utofauti mkubwa. Bila ya namba ni rahisi kujidanganya na kuamini unafanya makubwa. Lakini namba hazidanganyi, kama kitu kimefanyika kinaweza kupimika. Weka imani yako kwenye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HITAJI KUU LA MAFANIKIO…

By | July 16, 2021

Unapojifunza kwa wengine waliofanikiwa, haimaanishi uwe kama wao ili ufanikiwe. Njia ya uhakika ya kutokufanikiwa ni kujaribu kuwa kama wengine. Hitaji kuu la mafanikio ni wewe kuwa wewe, kujitambua, kujikubali, kujichagua na kujiamini. Hakuna anayeweza kukushinda wewe kuwa wewe na hapo ndipo ilipo nguvu kubwa kwako ya ushindani na kufika (more…)

#TAFAKARI YA LEO; CHAGUA KUWEKEZA VIZURI…

By | July 15, 2021

Muda na nguvu zako ni rasilimali muhimu sana kwako. Namna unavyochagua kutumia rasilimali hizo ni juu yako mwenyewe. Wapo wanaozitumia hovyo na kuzipoteza na wapo wanaozitumia vizuri na kunufaika. Wewe chagua kutumia rasilimali hizo vizuri, kwa kuhakikisha unaziwekeza kwenye kufanya mambo yenye tija kwako na kwa wengine pia. Iwe utachagua (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUNUFAIKA NA UNAYOSOMA…

By | July 13, 2021

Watu wengi hawanufaiki na yale wanayosoma, kwa sababu shule zimewaharibu. Shuleni mtu alisoma ili kufaulu mtihani, mtihani ukishapita basi hajali tena yale aliyosoma. Kwenye maisha husomi ili kujibu mtihani, bali unasoma ili kuyafanya maisha yako kuwa bora. Hivyo kwa kila unachojifunza, unapaswa kukitafakari ba kuona jinsi ya kukitumia kwenye maisha (more…)