Category Archives: #TAFAKARI YA LEO

#TAFAKARI YA LEO; KUJIDANGANYA NA KUJIFARIJI…

By | July 12, 2021

Sababu nyingi unazojipa za kwa nini hujaweza kufanya au kupata unachotaka siyo sababu halisi, bali ni visingizio tu. Kwa visingizio hivyo umekuwa unajidanganya na kujifariji, kitu ambacho ni kikwazo kwa mafanikio yako. Kama kuna kitu unajipa kama sababu ya kikwazo, lakini wengine wameweza kuvuka kitu hicho, basi hiyo siyo sababu, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; GEUZA HOFU KUWA FURAHA…

By | July 11, 2021

Jamii imekutengenezs kuhofia mambo yasiyo na tija yoyote kwako. Mfano kuhofia wengine wanakuchukukiaje, kuhofia kukosolewa na hata kuhofia kupitwa na yanayoendelea kwenye mitandao. Hofu zote hizo hazina manufaa yoyote kwako. Ili kuziondoa zisiwe kikwazo, zigeuze kuwa furaha. Furahia pale wengine wanapokupinga au kukukosoa na kama ni watu sahihi jifunze kwao, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USICHANGANYE VIPAUMBELE…

By | July 10, 2021

Mafanikio makubwa ndiyo kipaumbele cha kwanza kabisa kwenye maisha yako, hupaswi kuruhusu kitu kingine kuingilia kipaumbele hicho. Utaona wengine wakihangaika na mambo mbalimbali kwenye maisha na kutamani kufanya kama wao. Lakini jua wengi hawafiki kwenye mafanikio makubwa na sababu kuu ni kuhangaika na mambo mengi badala ya kuweka vipaumbele sahihi. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; CHAGUA KUELEWEKA AU KUFANIKIWA…

By | July 8, 2021

Vyote viwili haviwezi kwenda pamoja. Ukitaka ueleweke na kila mtu huwezi kufanikiwa. Na ukitaka upate mafanikio makubwa, huwezi kueleweka na kila mtu. Wanaofikia mafanikio makubwa wanajali zaidi ndoto zao kuliko wengine wanawachukuliaje. Wanaoshindwa wanajali sana wengine wanawachukuliaje kuliko wanavyojali ndoto zao kubwa. Kipenga kimepulizwa, unachagua upande upi? Ukichagua upande wa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HAZINA YA BIASHARA YAKO…

By | July 7, 2021

Ni wateja ambao tayari walishanunua kwenye biashara yako na kuridhika na kile walichokipata. Ukishakuwa na wateja wa aina hii basi biashara yako ina hazina kubwa. Ni wateja ambao ni rahisi kuwashawishi wanunue tena, lakini pia ni wateja ambao wanaweza kuweta wateja wengine. Kila siku pambana kujenga hazina hii kwenye biashara (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WAPE TAARIFA MPYA…

By | July 6, 2021

Kama kuna watu unataka wabadili maamuzi na misimamo yao, usikazane kuwaonyesha kwamba wamekosea, badala yake wape taarifa mpya zinazowapa nafasi ya kufanya maamuzi mapya. Hakuna mtu anayependa kukiri kwamba amekosea, hivyo kuwaonyesha wamekosea kunawafanya wazidi kusimamia maamuzi yao. Lakini unapowapa taarifa mpya ambazo zinawapa mtazamo mpya, wanaamua wenyewe kufanya maamuzi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UPO TAYARI KUTOA NINI?

By | July 5, 2021

Wengi wanapoyaangalia mafanikio, wanachoangalia ni wanakwenda kupata nini. Huo ni upande mbaya wa kuangalia maana ndiyo ambao kila mtu anauangalia na ndiyo maana wengi hawafanikiwi. Wewe angalia kwanza upande wa unatoa nini. Uko tayari kutoa nini ili uweze kufanikiwa? Mafanikio siyo rahisi na ndiyo maana wengi hawafanikiwi. Kikwazo kikubwa ni (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KAMA HAKIKUI, KUNA TATIZO…

By | July 4, 2021

Kama kitu kimezaliwa au kuanzishwa, kinapaswa kukua. Kama hakuna ukuaji maana yakr kuna tatizo, kuna kikwazo kinachozuia kitu hicho kisikue. Wajibu wako ni kujua tatizo au kikwazo kiko wapi, kukifanyia kazi ili kitu kiweze kukua. Na ili ujue kama kitu kinakua au la, lazima uwe na njia ya kukipima. Bila (more…)

#TAFAKARI YA LEO; IFANYE KAZI HII NGUMU….

By | July 3, 2021

Kwa kawaida huwa hatupendi kufanya vitu vigumu, badala yake tunakimbilia kwenye vitu rahisi. Sasa kwa kuwa vitu rahisi kila mtu anafanya, vinakosa thamani na inakuwa vigumu kufanikiwa. Moja ya kazi ngumu ambayo huwa tunaitoroka ni kufikiri na akili zetu huwa zinatafuta kila aina ya sababu ili tu tusifikiri mambo magumu. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNATAKA KUJISIKIA VIZURI AU KUWA BORA?

By | July 2, 2021

Ukitaka kujisikia vizuri, sikiliza uongo, maana huo unakubembeleza na haukuumizi. Ukitaka kuwa bora sikiliza ukweli, huo hakubembelezi na unakuumiza. Walio wengi wanapenda kubembelezwa na kutokuumizwa, ndiyo maana hawapigi hatua kwenye maisha yao. Ni wachache sana walio tayari kuukabili ukweli unaowaumiza na usiowabembeleza, lakini unawafanya kuwa bora zaidi. Kama unataka kufanikiwa, (more…)