Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (73/366); Jijengee ustahimilivu.

By | January 12, 2022

#SheriaYaLeo (73/366); Jijengee ustahimilivu. Safari ya kuelekea kwenye ubobezi wa hali ya juu na mafanikio makubwa siyo rahisi. Kadiri unavyokwenda ndivyo inataka zaidi kutoka kwako, ikitaka muda wako na juhudi zako zaidi na zaidi. Hilo huwachosha wengi na kuamua kuishia njiani, maana hujikuta wanaishiwa nguvu na kuchoka sana. Kama wewe (more…)

#SheriaYaLeo (72/366); Jiboreshe kupitia kushindwa.

By | January 11, 2022

#SheriaYaLeo (72/366); Jiboreshe kupitia kushindwa. Kukosea na kushindwa ni zawadi kubwa kwako. Kwani kunakuonyesha ni maeneo gani ambayo una madhaifu au bado hujawa imara kama inavyohitajika. Unapofanya kitu na ukakosea au ukashindwa, haimaanishi kwamba huwezi kamwe kukifanya. Bali inamaanisha kuna vitu bado hujavijua katika kufanya kitu hicho. Hivyo unapaswa kujifunza (more…)

#SheriaYaLeo (71/366); Weka umakini mkubwa.

By | January 10, 2022

#SheriaYaLeo (71/366); Weka umakini mkubwa. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu, unapaswa kuweka umakini mkubwa sana kwenye chochote kile unachoamua kufanya. Usifanye tu kwa juu juu au kwa mazoea, badala yake fanya kwa kina kabisa. Jua undani wa kile unachokifanya na kifanye kwa namna ya tofauti na ya kipekee (more…)

#SheriaYaLeo (70/366); Maarifa ndiyo ukuu wako.

By | January 9, 2022

#SheriaYaLeo (70/366); Maarifa ndiyo ukuu wako. Maarifa kidogo ni sumu kubwa. Kwa kujua kidogo unaweza kupata kiburi na kudhani tayari unajua kila kitu. Unachopaswa kujua ni kwamba maarifa yanaendelea kubadilika kadiri muda unavyokwenda. Historia iko wazi kabisa, vitu vingi ambavyo watu waliamini ni kweli, kwa sasa vimethibitishwa siyo kweli. Maendeleo (more…)

#SheriaYaLeo (69/366); Kukosa uvumilivu ni adui mkubwa.

By | January 8, 2022

#SheriaYaLeo (69/366); Kukosa uvumilivu ni adui mkubwa. Kikwazo kikubwa zaidi kwenye ubunifu wako ni kukosa uvumilivu. Ile hali ya kuharakisha na kutaka kupata matokeo makubwa kwa haraka ni kikwazo kikubwa kwako kufikia ubobezi wa hali ya juu. Unapoharakisha, hupati muda wa kujifunza kwa kina na kubobea yale ya msingi kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (68/366); Baki na udadisi wako.

By | January 7, 2022

#SheriaYaLeo (68/366); Baki na udadisi wako. Wakati unaanza safari ya ubobezi, unakuwa na udadisi mkubwa, kitu kinachokusukuma kujifunza mambo mengi na kuweza kufanya mapya na makubwa. Hilo linapelekea upate matokeo mazuri. Na hapo ndipo hatari inapoanzia. Kutokana na matokeo mazuri unayokuwa umepata, unaacha kuwa mdadisi, unajiona umeshajua kila kitu na (more…)

#SheriaYaLeo (67/366); Iweke akili kwenye mwendo.

By | January 6, 2022

#SheriaYaLeo (67/366); Iweke akili kwenye mwendo. Tulipokuwa watoto, akili zetu hazikuwa zikisimama. Tulikuwa wazi kwa ajili ya mawazo ba uzoefu mpya. Tulijifunza kwa kasi kwa sababu dunia ilitushangaza. Pale tulipokwama, tulitafuta njia ya kibunifu ya kuvuka kinachotukwamisha. Akili yetu ilikuwa kwenye mwendo muda wote na mara zote tulijawa na shauku (more…)

#SheriaYaLeo (66/366); Zawadi ya akili yetu halisi.

By | January 5, 2022

#SheriaYaLeo (66/366); Zawadi ya akili yetu halisi. Wote tunamiliki nguvu kubwa ya ubunifu tuliyozaliwa nayo na inayotaka kujidhihirisha. Hiyo ni zawadi ya akili yetu halisi, ambayo ina uwezo mkubwa sana. Akili ya binadamu kwa asili ina ubunifu mkubwa ndani yake. Kila wakati ikitafuta njia za kujenga uhusiano na muunganiko baina (more…)

#SheriaYaLeo (65/366); Angalia kwa upana na fikiri mbele zaidi.

By | January 4, 2022

#SheriaYaLeo (65/366); Angalia kwa upana na fikiri mbele zaidi. Kwenye mazingira yoyote yenye ushindani, ambapo kuna washindi na washindwa, yule mwenye mtazamo mpana na anayefikiria kwa ukubwa zaidi ndiye anayeshinda. Na sababu ni rahisi, mtu huyo anakuwa na uwezo wa kufikiri zaidi ya pale alipo kwa wakati huo na kuweza (more…)

#SheriaYaLeo (64/366); Mchakato wa ubunifu.

By | January 3, 2022

#SheriaYaLeo (64/366); Mchakato wa ubunifu. Hakuna darasa la ubunifu, yaani ubunifu ni kitu ambacho huwezi kufundishwa na mtu yeyote yule. Ubunifu ni kitu ambacho unajijengea wewe mwenyewe kwenye kile unachokuwa unafanya. Kupitia wale waliobobea kwenye maeneo mbalimbali, tunajifunza hatua muhimu za kujijengea ubunifu kwenye kile unachofanya. Hatua ya kwanza ni (more…)