Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (63/366); Jijengee nidhamu ya kazi.

By | January 2, 2022

#SheriaYaLeo (63/366); Jijengee nidhamu ya kazi. Watu wote walioweza kubobea na kufanya makubwa kwenye maeneo waliyochagua siyo ambao walikuwa wanasukumwa na fedha au umaarufu. Bali ni wale ambao walikuwa wamejijengea nidhamu kubwa ya kazi kwenye eneo walilochagua. Walichagua kufanya kazi kwa ustadi wa hali ya juu na kujali sana kuhusu (more…)

#SheriaYaLeo (62/366); Ingia Ndani.

By | January 1, 2022

#SheriaYaLeo (62/366); Ingia Ndani. Safari ya ubobezi inaweza kuelezewa kwa namna moja, kuzidi kuzama ndani kwenye kile unachotaka kubobea. Wakati unapoianza safari hii unakuwa unakiona kitu kwa nje na mambo mengi huyaelewi. Lakini kadiri unavyojifunza na kufanya, unazidi kuzama ndani zaidi. Unapata uelewa wa kina kuhusu kitu hicho na kuweza (more…)

#SheriaYaLeo (61/366); Endelea kutanua akili yako.

By | December 31, 2021

#SheriaYaLeo (61/366); Endelea kutanua akili yako. Kadiri unavyobobea ndivyo unavyoshawishika kwamba umeshajua kila kitu na hakuna kipya cha kujifunza. Lakini ubobezi huwa hauendi hivyo, ubobezi hauna kilele. Ubobezi ni zoezi endelevu. Siku utakayoona umeshafika kwenye kilele ndiyo siku ambayo utaanza kuanguka. Hivyo kwenye safari yako ya ubobezi, bila ya kujali (more…)

#SheriaYaLeo (60/366); Tumia njia ya kujaribu na kushindwa.

By | December 30, 2021

#SheriaYaLeo (60/366); Tumia njia ya kujaribu na kushindwa. Katika safari yako ya kujifunza ili kufikia ubobezi, usianze na ujuzi mmoja na kukomaa nao huo mapema. Badala yake jifunze ujuzi mwingi unaoendana na kile unachotaka kubobea. Kadiri unavyojikusanyia ujuzi mwingi, ndivyo unakuwa na uwanja mpana wa kufanya mengi na makubwa zaidi. (more…)

#SheriaYaLeo (59/366); Kata yasiyokuwa na umuhimu.

By | December 29, 2021

#SheriaYaLeo (59/366); Kata yasiyokuwa na umuhimu. Kwenye safari yako ya ubobezi, utakutana na mengi kutoka kwa wale ambao unajifunza kwao. Watakuwa na mengi ya kukufundisha na kukutana uyachukue yote kwa sababu ni muhimu. Lakini siyo yote yanayoweza kuwa na umuhimu kwako. Hivyo wewe unapaswa kuchagus yale muhimu yanayokufikisha wewe kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (58/366); Anzisha Mtindo wako mwenyewe.

By | December 28, 2021

#SheriaYaLeo (58/366); Anzisha Mtindo wako mwenyewe. Wakati unaanza kujifunza kutoka kwa wengine, unawaiga na kufanya kama wao. Hilo ni muhimu kwenye kujifunza na kuijua misingi muhimu ya kile ulichochagua. Lakini kama utaendelea hivyo kwa wakati wote, hutaweza kufikia ubobezi wa hali ya juu. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu, (more…)

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako.

By | December 27, 2021

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako. Kadiri unavyoendelea kujifunza kwa kufanya, utajikuta umejijengea aina fulani ya mazoea ambayo ndiyo unaridhika nayo. Mazoea hayo yanakuwa yametokana na wale ambao unakuwa umejifunza kutoka kwao, maana nao pia wanakuwa wamefikia kilele fulani na kufanya zaidi kwa mazoea. Huwezi kufikia ubobezi wa hali (more…)

#SheriaYaLeo (56/366); Endelea kutanua mipaka yako.

By | December 26, 2021

#SheriaYaLeo (56/366); Endelea kutanua mipaka yako. Unapoianza safari ya kujifunza ili kuelekea kwenye ubobezi wa hali ya juu, unakutana na ukweli ambao hukuwa unaujua. Ukweli huo ni safari hiyo ni ngumu na vikwazo ni vingi. Kikwazo kikubwa kabisa kitakuwa ni kupata watu sahihi kujifunza kutoka kwao ili kuweza kufikia ubobezi. (more…)

#SheriaYaLeo (55/366); Mpite Mwalimu Wako.

By | December 25, 2021

#SheriaYaLeo (55/366); Mpite Mwalimu Wako. Unapoanza kujifunza kwenye eneo unalotaka kubobea, unapaswa kufuata maelekezo unayopewa na mwalimu wako, ambaye tayari ameshabobea kwenye eneo hilo. Ukishaijua misingi yote muhimu ya eneo hilo ulilochagua, unapaswa kujifunza zaidi ya kile ambacho mwalimu wako anakufundisha. Unapaswa kuyageuza mafunzo yake yaendane na upekee na utofauti (more…)

#SheriaYaLeo (54/366); Usitosheke na maarifa.

By | December 24, 2021

#SheriaYaLeo (54/366); Usitosheke na maarifa. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu na kudumu kwenye ubobezi huo, hupaswi kuridhika na maarifa. Hupaswi kufika mahali na kuona tayari umeshajifunza vya kutosha na kujua kila kitu. Kila wakati unapaswa kuwa na njaa na kiu ya kuendelea kujifunza kwa kina zaidi. Jifunze kwa (more…)