Category Archives: SHERIA ZA SIKU

SheriaYaLeo (43/366); Rudia rudia kufanya.

By | December 13, 2021

SheriaYaLeo (43/366); Rudia rudia kufanya. Mfumo wa elimu unafundisha vitu kwa nadharia, kwa mwanafunzi kusoma na kufanya mitihani. Katika kipindi chote cha elimu mwanafunzi anajifunza kwa kupewa maarifa na taarifa tu. Haishangazi kwa nini mwanafunzi anapohitimu masomo na kwenda kwenye dunia halisi anajikuta hakuna anachoweza kufanya. Anaweza kuwa na vyeti (more…)

#SheriaYaLeo (42/366); Jinsi ya kujifunza kwa kasi.

By | December 12, 2021

#SheriaYaLeo (42/366); Jinsi ya kujifunza kwa kasi. Kwa chochote unachojifunza, unajifunza kwa kasi zaidi kupitia kufanya kuliko kupitia kusoma au kusikiliza maelekezo. Mwanzo wa kufanya huwa ni mgumu, lakini kadiri unavyoendelea kufanya ndivyo inavyokuwa rahisi. Unajifunza kwa kasi na ubora zaidi kwa kufanya kile unachojifunza. Hata kama ni lugha mpya (more…)

#SheriaYaLeo (41/366); Jifunze Kutoka Kwenye Kila

By | December 11, 2021

#SheriaYaLeo (41/366); Jifunze Kutoka Kwenye Kila Kitu. Kila jukumu unalopewa au kuwa nalo linakupa fursa ya kujifunza kuhusu kile unachofanya, watu na dunia kwa ujumla. Hakuna jukumu ambalo halina fursa hiyo ya kujifunza na hakuna taarifa ndani ya kitu ambazo ni ndogo na zisizo na uzito. Kila kitu unachosikia au (more…)

#SheriaYaLeo (40/366); Raha itokane na unachofanya

By | December 10, 2021

#SheriaYaLeo (40/366); Raha itokane na unachofanya. Kadiri unavyoendelea kujifunza na kujijengea ujuzi wako, unaendelea kubadilika na kuwa bora zaidi. Unagundua uwezo mkubwa ulio ndani yako ambao ulikuwa umelala, ambao unaamshwa kadiri unavyokwenda. Unakua kiakili na kihisia na maana ya raha kwako inabadilika. Vitu vinavyotoa raha ya haraka kama ulevi mitandao (more…)

#SheriaYaLeo (39/366); Menta Sahihi Kwako.

By | December 9, 2021

#SheriaYaLeo (39/366); Menta Sahihi Kwako. Kupata menta sahihi kwako, angalia mtu ambaye kazi zake zinakuvutia sana, zinakupa hamasa na msukumo wa kuwa kama wao. Angalia mtu ambaye mtindo wake wa maisha na kazi anazofanya unakupa shauku kubwa, unajiona unaweza kufanya kwa namna kama yake. Pia angalia ni mtu wa aina (more…)

#SheriaYaLeo (38/366); Njia pekee ya mkato ya ya kufika kwenye ubobezi.

By | December 8, 2021

#SheriaYaLeo (38/366); Njia pekee ya mkato ya kufika kwenye ubobezi. Maisha ni mafupi na muda wako wa kujifunza na ubunifu una ukomo. Bila ya kuwa na mwongozo, utapoteza miaka yako ya thamani ukijariby kujifunza kutoka vyanzo mbalimbali na bado usifikie ubobezi. Badala ya kufanya hivyo, unapaswa kufuata mfano wa wabobezi (more…)

#SheriaYaLeo (37/366); Jichukulie Kama Mjenzi.

By | December 7, 2021

#SheriaYaLeo (37/366); Jichukulie Kama Mjenzi. Haijalishi upo kwenye tasnia gani, unapaswa kufikiri na kujichukulia kama mjenzi. Wewe ni mjenzi unayetumia rasilimali na mawazo mbalimbali kutengeneza kitu chenye manufaa kwa wengine. Kujenga kitu chochote vizuri, iwe ni nyumba, taasisi, biashara au kazi ya sanaa, ni lazima uuelewe mchakato wa ujenzi na (more…)

#SheriaYaLeo (36/366); Kusanya Ujuzi Mwingi.

By | December 6, 2021

#SheriaYaLeo (36/366); Kusanya Ujuzi Mwingi. Lengo lako kuu kwenye mafunzo unayoyapata ni kujifunza na kukusanya ujuzi mwenye kwenye yale maeneo yanayokuvutia na kukuhamasisha. Kama baadaye mambo yatabadilika na kulazimika kubadili kazi au biashara unayofanya, ujuzi mwingi uliojijengea unakupa fursa ya kufanya hivyo. Lakini pia utakuwa tayari unajua jinsi ya kujifunza (more…)

#SheriaYaLeo (35/366); Thamini kujifunza kuliko

By | December 5, 2021

#SheriaYaLeo (35/366); Thamini kujifunza kuliko mengine yote. Kadiri unavyopiga hatua kwenye maisha yako, utasukumwa kutafuta fursa zinazokuingizia kipato kikubwa zaidi ili kuweza kuendana na hali ya maisha. Hilo litakusukuma kutafuta kazi au biashara ambayo inakulipa vizuri zaidi. Kwa bahati mbaya sana, unapopata kile kinacholipa zaidi, huwa hakina fursa za kujifunza (more…)

#SheriaYaLeo (34/366); Lengo Kuu Moja.

By | December 4, 2021

#SheriaYaLeo (34/366); Lengo Kuu Moja. Unapochagua kufanya kazi chini ya mtu ambaye amebobea ili ujifunze kwake, lengo lako kuu ni kujifunza na siyo kulipwa vizuri au kupata hadhi kubwa. Unachohitaji ni kujijengea ujuzi bora na wa kipekee, ambao utaweza kuutumia kufanya makubwa kwenye maisha yako. Unapokuwa kijana na ndiyo unaanza (more…)