Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (33/366); Anachohitaji Menta.

By | December 3, 2021

#SheriaYaLeo (33/366); Anachohitaji Menta. Ili kujifunza kwa vitendo na uhalisia, unahitaji mtu ambaye tayari ameshafanikiwa kwenye kile unachotaka kufanikiwa ili awe menta wako. Ni kupitia menta huyo ndiyo utajifunza kwa uzoefu ambao yeye ameupitia mpaka kufika alipofika. Atakusaidia kuepuka makosa ambayo yeye alifanya ili usijicheleweshe. Ni muhimu sana kumpata aliyefanikiwa (more…)

#SheriaYaLeo (32/366); Jifunze kwa kufanya.

By | December 2, 2021

#SheriaYaLeo (32/366); Jifunze kwa kufanya. Ulipokuwa mdogo, wazazi na jamii ilikufundisha mambo mengi kuhusu maisha kupitia maelekezo na mifano. Ulipoenda shule ukafundishwa mambo mengine mengi kuhusu kazi na biashara kupitia maelekezo na mifano. Unapoingia kwenye dunia ya uhalisia, katika kuyaishi maisha na kufanya kazi au biashara, ndiyo unagundua yale uliyojifunza (more…)

#SheriaYaLeo (31/366); Chanzo cha nguvu zote.

By | December 1, 2021

#SheriaYaLeo (31/366); Chanzo cha nguvu zote. Usijaribu kuikwepa kazi ya kugundua kusudi na wajibu wa maisha yako kwa kudhani vitakuja kwako vyenyewe. Japo inaweza kutokea hivyo kwa baadhi ya watu, kuweza kujua kusudi na wajibu wa maisha yao mapema na kwa matukio ya kipekee, kwa wengj wetu hilo linahitaji kazi (more…)

#SheriaYaLeo (30/366); Amini kwenye mchakato.

By | November 30, 2021

#SheriaYaLeo (30/366); Amini kwenye mchakato. Unapoanza kufanya kitu chochote kile kipya kwako, unakutana na ugumu mkubwa. Unakua hujui mambo mengi kuhusu kitu hicho na hivyo unasumbuka sana mwanzoni. Unaweza kukata tamaa kwa kuona vitu ni vingi na vigumu, huwezi kupambana navyo. Kama utakata tamaa, utakuwa umeishia hapo na kushindwa kufikia (more…)

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo.

By | November 29, 2021

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo. Unapaswa kuwa jinsi ulivyo kwa kujifunza wewe ni mtu wa aina gani, kisha kuwa mtu huyo. Ulizaliwa na uwezo, tabia na vipaji vya kipekee ambavyo vinakutofautisha na wengine na kujenga hatima yako. Hivyo ndivyo ulivyo ndani yako. Ni kwa kuishi huo upekee wako ndiyo unaweza (more…)

#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka.

By | November 28, 2021

#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka. Wakati unaianza safari yako ya wito na kusudi la maisha yako, unachagua eneo linaloendana na yale yaliyo ndani yako. Sehemu unayoanzia inakupa nafasi ya kujifunza na kujijengea ujuzi na uzoefu muhimu. Pia inakupa nafasi ya kuingiza kipato na kujijengea kujiamini. Kadiri unavyokwenda unagundua kuna njia za (more…)

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio.

By | November 27, 2021

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio. Tangu enzi na enzi, watu wamekuwa wanatafuta njia za mkato na kanuni zahisi za kufanikiwa. Lakini mwisho wa siku wanaishia kupotea, kwa sababu hivi ni vitu ambavyo havipo kabisa. Wakati unahangaika kutafuta njia hizo za mkato zisizokuwepo, unapuuza nguvu kubwa ambayo tayari ipo ndani (more…)

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia

By | November 26, 2021

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia Usifikie Ubobezi. Una nguvu kubwa ndani yako ambayo inakufanya wa tofauti na wa kipekee, nguvu hiyo ndiyo imebeba wito na kusudi lako. Lakini pia kuna nguvu kubwa za nje ambazo zinaipinga nguvu hiyo ya ndani na kukuzuia usiweze kuitumia ili kujitofautisha na kufanya makubwa. Nguvu (more…)

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo.

By | November 25, 2021

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo. Sisi binadamu huwa tunahangaika na yale tunayoweza kuona kwa macho yetu. Tunapoangalia mabadiliko kwenye maisha ya wengine, tunaona bahati nzuri ambayo mtu aliipata kwa kukutana na mtu aliyemsaidia sana. Tunaona miradi iliyomletea mtu fedha na umaarufu. Kwa maneno mengine tunaona manadiliko yanayoonekana kwa nje. (more…)

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea.

By | November 24, 2021

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea. Wakati mwingine kusudi na wito wako hautokani na kitu kimoja, bali unatokana na kuunganisha vitu ambavyo unapendelea kufanya. Kwa kujua vitu hivyo na kuviunganisha pamoja unaweza kutengeneza kitu cha kipekee kabisa kwako. Kama bado ni kijana na ndiyo unaianza safari yako, unapaswa kujaribu mambo mbalimbali (more…)