2557; Vipimo vya muda.

By | December 31, 2021

2557; Vipimo vya muda. Sekunde ndiyo kipimo cha chini zaidi cha muda. Huwa hatuhangaiki sana kuzipima sekunde, isipokuwa kwa mambo yenye ukomo mkali wa muda. Sekunde chache zinaweza kuleta tofauti kubwa. Dakika ni kipimo kinachofuatia. Ni kipimo ambacho tunaweza kutumia kufanya mengi, lakini huwa tunakipuuza. Mfano watu huwa wanalalamika hawana (more…)

#SheriaYaLeo (61/366); Endelea kutanua akili yako.

By | December 31, 2021

#SheriaYaLeo (61/366); Endelea kutanua akili yako. Kadiri unavyobobea ndivyo unavyoshawishika kwamba umeshajua kila kitu na hakuna kipya cha kujifunza. Lakini ubobezi huwa hauendi hivyo, ubobezi hauna kilele. Ubobezi ni zoezi endelevu. Siku utakayoona umeshafika kwenye kilele ndiyo siku ambayo utaanza kuanguka. Hivyo kwenye safari yako ya ubobezi, bila ya kujali (more…)

2556; Mbona huyu mtoto hakui haraka?

By | December 30, 2021

2556; Mbona huyu mtoto hakui haraka? Mara kwa mara huwa napata swali la aina hii ninapokuwa natibu wagonjwa. Mzazi mwenye wasiwasi anauliza mtoto anakaribia mwaka, lakini bado hajaota meno. Nilimchunguza mtoto vizuri nagundua hana shida yoyote, maendeleo yake yote yako vizuri. Hapo huwa napenda kudadisi nini kinampa hofu zaidi mzazi. (more…)

#SheriaYaLeo (60/366); Tumia njia ya kujaribu na kushindwa.

By | December 30, 2021

#SheriaYaLeo (60/366); Tumia njia ya kujaribu na kushindwa. Katika safari yako ya kujifunza ili kufikia ubobezi, usianze na ujuzi mmoja na kukomaa nao huo mapema. Badala yake jifunze ujuzi mwingi unaoendana na kile unachotaka kubobea. Kadiri unavyojikusanyia ujuzi mwingi, ndivyo unakuwa na uwanja mpana wa kufanya mengi na makubwa zaidi. (more…)

2555; Kuvunja mazoea kunahitaji kujali.

By | December 29, 2021

2555; Kuvunja mazoea kunahitaji kujali. Ipo hadithi ya mwanamke ambaye alikuwa anakata mkia wa samaki kabla hajamkaanga. Siku moja mume wake akamuuliza kwa nini anafanya hivyo, akamjibu ndivyo mama yake amekuwa anafanya. Mume akamtaka wampigie simu mama yake kumuuliza. Walifanya hivyo na mama akajibu alikuwa anafanya hivyo kwa sababu ndivyo (more…)

#SheriaYaLeo (59/366); Kata yasiyokuwa na umuhimu.

By | December 29, 2021

#SheriaYaLeo (59/366); Kata yasiyokuwa na umuhimu. Kwenye safari yako ya ubobezi, utakutana na mengi kutoka kwa wale ambao unajifunza kwao. Watakuwa na mengi ya kukufundisha na kukutana uyachukue yote kwa sababu ni muhimu. Lakini siyo yote yanayoweza kuwa na umuhimu kwako. Hivyo wewe unapaswa kuchagus yale muhimu yanayokufikisha wewe kwenye (more…)

2554; Akili ‘itajiseti’ yenyewe.

By | December 28, 2021

2554; Akili ‘itajiseti’ yenyewe. Akili zetu sisi binadamu zina uwezo mkubwa mno, uwezo ambao hatuwezi hata kuuelewa. Mara nyingi huwa tunafikiria baadhi ya mambo yakitokea basi maisha yetu yatavurugika sana. Labda ni kifo cha mtu wa karibu tunayemtegemea sana. Labda kufukuzwa kazi au biashara zetu kufa. Labda kuhama kutoka eneo (more…)

#SheriaYaLeo (58/366); Anzisha Mtindo wako mwenyewe.

By | December 28, 2021

#SheriaYaLeo (58/366); Anzisha Mtindo wako mwenyewe. Wakati unaanza kujifunza kutoka kwa wengine, unawaiga na kufanya kama wao. Hilo ni muhimu kwenye kujifunza na kuijua misingi muhimu ya kile ulichochagua. Lakini kama utaendelea hivyo kwa wakati wote, hutaweza kufikia ubobezi wa hali ya juu. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu, (more…)

2553; Mubashara na marudio.

By | December 27, 2021

2553; Mubashara na marudio. Ukiangalia mchezo wowote ule mubashara, kwa wakati ambapo unaendelea, unakuwa hujui nini hasa kitatokea muda wowote ujao. Hivyo unaangalia kwa shauku kubwa, ukijua chochote kinaweza kutokea. Ukiangalia mchezo huo huo kwa marudio, unakuwa huna shauku kubwa, kwa sababu tayari unajua nini kitakwenda kutokea. Kama ni magoli (more…)

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako.

By | December 27, 2021

#SheriaYaLeo (57/366); Toka nje ya mazoea yako. Kadiri unavyoendelea kujifunza kwa kufanya, utajikuta umejijengea aina fulani ya mazoea ambayo ndiyo unaridhika nayo. Mazoea hayo yanakuwa yametokana na wale ambao unakuwa umejifunza kutoka kwao, maana nao pia wanakuwa wamefikia kilele fulani na kufanya zaidi kwa mazoea. Huwezi kufikia ubobezi wa hali (more…)