#SheriaYaLeo (215/366); Tumia hali yao ya ushindani.

By | June 3, 2022

#SheriaYaLeo (215/366); Tumia hali yao ya ushindani. Sisi binadamu huwa tuna hali ya ushindani ndani yetu. Huwa hatupo tayari kuona wengine wanatushinda kwenye kitu fulani, hata kama ni kidogo kiasi gani. Ili kuwashawishi wengine, tumia hali yao ya ushindani. Waweke kwenye hali ambayo wanashindana na watu wengine na hawatakubali kushindwa. (more…)

2710; Rahisi kupatikana.

By | June 2, 2022

2710; Rahisi kupatikana. Chochote ambacho ni rahisi kupatikana huwa siyo chenye thamani kubwa na unachohitaji ili kufika kule unakotaka. Hili ni jambo la msingi kabisa ambalo wengi huwa hawalielewi na kuishia kuwa kikwazo kwao kufanikiwa. Vitu vyenye thamani kubwa kwenye maisha huwa ni vigumu kupatikana na hilo ndiyo linapelekea wengi (more…)

#SheriaYaLeo (214/366); Sanaa ya ushawishi.

By | June 2, 2022

#SheriaYaLeo (214/366); Sanaa ya ushawishi. Lengo la hotuba ya ushawishi ni kutengeneza hali ya mtu kukubaliana na hoja bila ya kuihoji. Hotuba ya aina hiyo huwa inawavuruga watu, kuondoa mapingamizi yao na kuwafanya wawe rahisi kushawishika. Hotuba hiyo huwa inakuwa na maneno yanayojirudia rudia, yenye msisitizo na yanayogusa hisia. Lengo (more…)

2709; Uvivu na uzembe.

By | June 1, 2022

2709; Uvivu na uzembe. Hawa ni maadui wakubwa wawili ambao ndiyo kikwazo kinachowazuia wote ambao hawajafanikiwa. Kwa kila ambaye hajafanikiwa, unapochunguza lazima unakuta maadui hao wawili wapo. Uvivu ni pale mtu unapojua nini unachopaswa kukifanya, ila hukifanyi. Unaweza kujipa sababu lukuki kwa nini hufanyi. Lakini ukweli ni kwamba una uvivu. (more…)

#SheriaYaLeo (213/366); Ufanye uwepo wako uwe wa msisimko.

By | June 1, 2022

#SheriaYaLeo (213/366); Ufanye uwepo wako uwe wa msisimko. Kwenye dunia ambayo ni ngumu na iliyojaa hali za kukatisha tamaa, watu wanapenda sana kukaa na watu wanaowapa msisimko. Hilo linarahisisha zoezi la ushawishi kwa sababu watu wanakazana sana kupata nafasi ya kuwa karibu na wewe. Ili kuwezesha hilo, hakikisha watu hawakuelewi (more…)

2708; Usiombe ruhusa, usiombe samahani.

By | May 31, 2022

2708; Usiombe ruhusa, usiombe samahani. Kitu kikubwa kuhusu maisha ya mafanikio ni huwezi kuw kama watu wengine. Huwezi kuishi maisha ambayo wengine wanayaishi na kutegemea upate mafanikio makubwa kabisa. Ni lazima maisha yako yawe ya tofauti kabisa na maisha ya wengine. Na njia moja ya kuonyesha tofauti hiyo ni kutokuomba (more…)

#SheriaYaLeo (212/366); Raha ya maigizo.

By | May 31, 2022

#SheriaYaLeo (212/366); Raha ya maigizo. Huwa tunayaangalia maigizo na kuyafurahia japo tunajua siyo kitu cha kweli. Mavazi ya waigizaji na jinsi mtiririko unavyokwenda huwa inakamata sana hisia na umakini wetu. Japo ni maigizo, huwa tunachukulia ni uhalisia. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye maisha halisi. Ili kuweza kuwashawishi watu, unapaswa kuwa (more…)

2707; Mtu wa ajabu.

By | May 30, 2022

2707; Mtu wa ajabu. Jamii huwa inapenda kumwelewa kila mtu kwenye yale anayoyafanya. Pale jamii inaposhindwa kumwelewa mtu, huwa inamchukulia ni mtu wa ajabu kabisa. Inamwona ni mtu asiyefaa au aliyepotoka na ambaye hawezi kufanikiwa. Anapopitia magumu ambayo kila mtu anayapitia, yeye ataonekana anayapitia hayo kwa sababu ya utofauti wake. (more…)

#SheriaYaLeo (211/366); Kumshawishi anayetaka kukushawishi.

By | May 30, 2022

#SheriaYaLeo (211/366); Kumshawishi anayetaka kukushawishi. Kuna wakati unajikuta kwenye hali ambapo unahitaji kumshawishi mtu ambaye na yeye pia anataka kukushawishi. Hapo unapaswa kutumia mbinu ya kumwonyesha kitu au tabia ya kutaka kushawishika naye. Yaani unamrahisishia zoezi lake la kukushawishi wewe, kitu ambacho kinakuwa rahisi kwako kumshawishi yeye pia. Unapomnasa mtu (more…)

2706; Kupanga na kufanya.

By | May 29, 2022

2706; Kupanga na kufanya. Kwa ujumla, mchakato mzima wa mafanikio unategemea sana kwenye kupanga na kufanya. Ni kitu rahisi lakini chenye nguvu kubwa sana ya kuamua mtu afanikiwe au ashindwe. Watu wengi huwa wanapanga lakini hawafanyi. Kupanga ni rahisi, kufanya siyo. Hivyo watu wana mipango mingi, lakini hawaitekelezi. Watu wengine (more…)