Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea.

By | November 24, 2021

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea. Wakati mwingine kusudi na wito wako hautokani na kitu kimoja, bali unatokana na kuunganisha vitu ambavyo unapendelea kufanya. Kwa kujua vitu hivyo na kuviunganisha pamoja unaweza kutengeneza kitu cha kipekee kabisa kwako. Kama bado ni kijana na ndiyo unaianza safari yako, unapaswa kujaribu mambo mbalimbali (more…)

2519; Tatizo siyo muda, bali nguvu.

By | November 23, 2021

2519; Tatizo siyo muda, bali nguvu. Nimeshaliandikia hili hapa mara kadhaa, lakini nitaendelea kulirudia kwa sababu ni dhana ambayo wengi hawaielewi. Tumezoeshwa sana kuhangaika na muda. Tukafundishwa jinsi ya kupangilia na kudhibiti muda wetu ili kuweza kufanya makubwa. Tumekuwa tunaambiwa wazi kabisa kwamba muda ni zaidi ya fedha, maana ukipoteza (more…)

#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako

By | November 23, 2021

#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako makubwa kwenye vipande vidogo. Kuwa na malengo makubwa na ya muda mrefu kunakupa msukumo na umakini mkubwa wa kuyafikia. Malengo hayo ambayo ni makubwa, mfano biashara kubwa ya kujenga huwa yanakupa shauku kubwa na kukusukuma uwe bora zaidi. Lakini pia malengo hayo makubwa huwa yana (more…)

ONGEA NA KOCHA; Kisima Ni Jeshi, Amri 21 Za Maisha na Godfrey Mbise.

By | November 22, 2021

Habari Mwanamafanikio? Karibu usikilize kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kwa juma hili kuna mambo makubwa matatu. Moja ni mafanikio ni vita, KISIMA CHA MAARIFA ni jeshi na wewe ni mwanajeshi kwenye hii vita. Hapa utajifunza kwa ufupi sifa za wanajeshi wa Sparta na mambo muhimu ya kuzingatia kwenye jeshi (more…)

2518; Mabadiliko na Msimamo.

By | November 22, 2021

2518; Mabadiliko na Msimamo. Kwenye safari ya mafanikio na maisha kwa ujumla, kuna njia panda moja kubwa ambayo wengi huwa hawaielewi. Kuna mambo ambayo yanabadilika kila wakati. Na kuna mambo ambayo hayabadiliki kabisa. Njia panda inakuwa ni kujua mambo gani yanabadilika ili kubadilika nayo na mambo gani hayabadiliki ili kuwa (more…)

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu.

By | November 22, 2021

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu. Ufunguo wa mafanikio kwenye tasnia yoyote ile ni kujijengea ujuzi wa aina mbalimbali kisha kuchanganya ujuzi huo kwa namna ya kipekee. Lakini mchakato wa kufanya hivyo unaweza kuwa mgumu, wenye maumivu na kukatishwa tamaa. Maana kadiri unavyokwenda unagundua ukomo na ukosefu wa ujuzi muhimu. (more…)

2517; Kuiga mafanikio ni kujipoteza.

By | November 21, 2021

2517; Kuiga mafanikio ni kujipoteza. Pamoja na siri nyingi za mafanikio kuwa bayana. Pamoja na hadithi za watu waliofanikiwa kupatikana kwa urahisi kila mahali. Bado ni wachache sana wanaopata mafanikio makubwa. Tulidhani kwenye zama hizi ambapo maarifa ya mafanikio yanapatikana kwa wingi na urahisi basi wengi wangekuwa wamefanikiwa, lakini hali (more…)

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni

By | November 21, 2021

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni tatizo. Hakuna kitu kibaya kama kuweka mategemeo yako yote kwa watu wengine. Utegemezi unakuweka kwenye hatari ya kuathiriwa na hisia hasi kama usaliti, kukatishwa tamaa, kuvurugwa na msongo. Hisia hizi huharibu sana utulivu wa akili yako. Kujitegemea mwenyewe ni muhimu sana kwa utulivu na mafanikio (more…)

2516; Makosa yanayojirudia rudia.

By | November 20, 2021

2516; Makosa yanayojirudia rudia. Kwenye kazi au biashara unayoifanya, kuna makosa huwa yanajirudia rudia kila mara. Unaweza kulalamikia makosa ya aina hii, lakini ni fursa nyingine nzuri ya kuboresha kile unachofanya na kujenga mfumo unaozuia hayo yasijirudie. Kwa kila kosa linalojirudia rudia, kaa chini uandike nini kinafanya kosa hilo lijirudie (more…)

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi.

By | November 20, 2021

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi. Dunia imejaa matatizo mbalimbali, na sehemu kubwa ya matatizo hayo tumeyatengeneza wenyewe. Kutatua matatizo hayo kunahitaji juhudi na ubunifu mkubwa. Kutegemea mazoea, teknolojia na kuwa mwema haitatusaidia. Tunahitaji nguvu ya kuweza kuyatambua matatizo hayo na kutengeneza taasisi mpya zinazoweza kukabiliana na mabadiliko tunayopitia. Ni (more…)