Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo.

By | November 29, 2021

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo. Unapaswa kuwa jinsi ulivyo kwa kujifunza wewe ni mtu wa aina gani, kisha kuwa mtu huyo. Ulizaliwa na uwezo, tabia na vipaji vya kipekee ambavyo vinakutofautisha na wengine na kujenga hatima yako. Hivyo ndivyo ulivyo ndani yako. Ni kwa kuishi huo upekee wako ndiyo unaweza (more…)

2524; Pesa ziko wapi?

By | November 28, 2021

2524; Pesa ziko wapi? Wahenga walisema, mali bila daftari, hutumika bila habari. Kama hutunzi vizuri kumbukumbu zako za kila senti inayoingia na kutoka, hutajua pesa zako zinapotelea wapi. Utaona tu umeshika pesa nyingi, lakini hujui zimeenda wapi. Na hapo ndipo wengi huamini kuna chuma ulete, hali ya ushirikina ambapo fedha (more…)

#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka.

By | November 28, 2021

#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka. Wakati unaianza safari yako ya wito na kusudi la maisha yako, unachagua eneo linaloendana na yale yaliyo ndani yako. Sehemu unayoanzia inakupa nafasi ya kujifunza na kujijengea ujuzi na uzoefu muhimu. Pia inakupa nafasi ya kuingiza kipato na kujijengea kujiamini. Kadiri unavyokwenda unagundua kuna njia za (more…)

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka.

By | November 27, 2021

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka. Zoezi la kutoa na kupokea ushauri limekuwa zoezi lisilo na manufaa kwa wengi wanaoshiriki. Hiyo ni kwa sababu watu wengi wanaoomba ushauri, siyo kama wanataka ushauri kweli, ila wanataka wajue kama maamuzi waliyofanya ni sahihi. Yaani ndani yao wanakuwa tayari wameshafanya maamuzi, ila wanaomba ushauri (more…)

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio.

By | November 27, 2021

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio. Tangu enzi na enzi, watu wamekuwa wanatafuta njia za mkato na kanuni zahisi za kufanikiwa. Lakini mwisho wa siku wanaishia kupotea, kwa sababu hivi ni vitu ambavyo havipo kabisa. Wakati unahangaika kutafuta njia hizo za mkato zisizokuwepo, unapuuza nguvu kubwa ambayo tayari ipo ndani (more…)

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji?

By | November 26, 2021

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji? Kwenye safari ya mafanikio, hakuna sumu kubwa kama ujuaji. Sumu hii huanza pale mtu anapoona yale anayofundishwa tayari anayajua. Kwa sababu maarifa na siri za mafanikio ni zile zile, wengi hufika mahali na kuona wameshajua kila kitu, hakuna tena kitu kipya. (more…)

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia

By | November 26, 2021

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia Usifikie Ubobezi. Una nguvu kubwa ndani yako ambayo inakufanya wa tofauti na wa kipekee, nguvu hiyo ndiyo imebeba wito na kusudi lako. Lakini pia kuna nguvu kubwa za nje ambazo zinaipinga nguvu hiyo ya ndani na kukuzuia usiweze kuitumia ili kujitofautisha na kufanya makubwa. Nguvu (more…)

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali.

By | November 25, 2021

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali. Watu wawili, wanaweza kuwa wanafanya kazi au biashara ya aina moja, mmoja akafanikiwa sana na mwingine akashindwa kabisa. Watu wamekuwa wakitafuta sababu za tofauti hiyo, wakiona labda ni bahati, fursa, upendeleo na uwezo tofauti. Yote hayo yanaweza kuchangia, ila kuna kimoja kikubwa ambacho huwa hakipewi (more…)

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo.

By | November 25, 2021

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo. Sisi binadamu huwa tunahangaika na yale tunayoweza kuona kwa macho yetu. Tunapoangalia mabadiliko kwenye maisha ya wengine, tunaona bahati nzuri ambayo mtu aliipata kwa kukutana na mtu aliyemsaidia sana. Tunaona miradi iliyomletea mtu fedha na umaarufu. Kwa maneno mengine tunaona manadiliko yanayoonekana kwa nje. (more…)

2520; Mahali unapojificha.

By | November 24, 2021

2520; Mahali unapojificha. Kila mmoja kuna mahali huwa anajificha inapokuja kwenye uhitaji wa kufanya makubwa ili kufanikiwa. Kufanya hayo makubwa ni kugumu na pia matokeo siyo ya uhakika sana. Wakati huo sisi binadamu huwa ni wavivu na tunapenda vitu vya uhakika. Hivyo tunapokabiliwa na kitu kikubwa cha kufanya mbele yetu, (more…)