Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2638; Ni kujenga, siyo kuota.

By | March 22, 2022

2638; Ni kujenga, siyo kuota. Mafanikio huwa yanaanza na ndoto, mtu kuwa na picha ya kile unachotaka, ambacho kwa sasa huna. Lakini ili kufikia ndoto hiyo, ni lazima ujenge. Ndoto haitafikiwa tu kwa kuota, Bali itafikiwa kwa kujenga. Hatua unazochukua katika kuifikia ndoto ndizo zinaifanya ndoto hiyo kuwa uhalisia. Thamani (more…)

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza.

By | March 22, 2022

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza. Kuna watu ambao ni rahisi sana kukubaliana na wewe pale unapokutana nao. Wanatabasamu sana, wana shauku kubwa na wanakuwa tayari kukusaidia kwa lolote. Hilo linakufanya uwaone ni watu sahihi kwako na kuwakubali kwenye maisha yako. Wanakuwa ni watu wanaokuridhisha na hivyo unawapa fursa mbalimbali kwenye maisha (more…)

Ongea Na Kocha; Instant Cashflow – Kuongeza Idadi Na Kiwango Cha Manunuzi.

By | March 21, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo tumeendelea na uchambuzi wa kitabu cha INSTANT CASHFLOW kilichoandikwa na Bradley Sugars. Kitabu hiki ni mwendelezo wa msingi mkuu tuliojifunza kwenye kitabu cha BILLIONAIRE IN TRAINING cha mwandishi huyo huyo. Kwenye BILLIONAIRE IN TRAINING tulijifunza ngazi tano za ujasiriamali ambazo (more…)

2637; Sahihi na siyo sahihi.

By | March 21, 2022

2637; Sahihi na siyo sahihi. Mtu mmoja amewahi kunukuliwa akisema kipimo cha akili iliyokomaa ni kuweza kushikilia kwenye akili mawazo mawili yanayopingana kwa wakati mmoja. Hili ni zoezi gumu mno kwa sababu kwa kawaida binadamu huwa tunapenda sana uhakika. Kukaa na mawazo mawili yanayopingana ni kukosa uhakika. Wengi huona ni (more…)

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka.

By | March 21, 2022

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka. Kuna watu ambao kwa nje wanajifanya kama hawakitaki kitu, ila kwa ndani wanakitaka sana. Kwa nje wanakikataa, ila ni kwa lengo la kuwafanya watu wawabembeleze ndiyo wakubali. Watu hao wanakuwa wanajua tabia ya binadamu, kwamba ukionekana unataka sana kitu, watu wanakuzuia usikipate. Au hata ukikipata (more…)

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu.

By | March 20, 2022

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu. Njia nyingine ambayo hutumiwa sana na wale wanaotaka mamlaka bila ya kuonekana wazi wazi ni kutaka usawa kwa kila mtu. Hapa husisitiza kila mtu ni sawa na lazima watu wote wachukuliwe kwa usawa. Hukazana kuwaaminisha wengine kwamba uwezo, uimara na hadhi tofauti za (more…)

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa.

By | March 19, 2022

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa. Kunbuka kwa kawaida watu huwa wanatengeneza mwonekano fulani wanaotaka dunia ione. Hivyo kila mtu ni kama amevaa barakoa, akionyesha kile ambacho anataka wengine waone na kuficha nia kuu aliyonayo. Mtu anaweza kuwa na uso wa tabasamu na maneno mazuri kabisa. Hii ni barakoa inayowafanya (more…)

2634; Lakini unakosea.

By | March 18, 2022

2634; Lakini unakosea. Hayo ni maneno utakayoyasikia maisha yako yote, mpaka siku unayoondoka hapa duniani. Kwa maamuzi yoyote utakayofanya na chochote utakachofanya, kuna watu watakuambia unakosea. Sema unataka fedha na hicho ndiyo kipaumbele chako cha kwanza na kuna watu watakuambia unakosea, una tamaa sana ya fedha na fedha siyo kila (more…)