Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu.

By | March 18, 2022

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu. Kwenye safari yako ya maisha utakutana na watu ambao wanatumia nguvu kubwa kuonyesha tabia fulani nzuri kwa nje. Inaweza kuwa ni huruma iliyopitiliza, kujali sana, kuonekana watakatifu au imara sana. Lakini pale unapowajua watu hao kwa undani, unaona kuna kivuli kipo nyuma ya tabia (more…)

2633; Kafanyaje huyu?

By | March 17, 2022

2633; Kafanyaje huyu? Kuna picha ya kichekesho (meme) inayozunguka sana kwenye mitandao. Kwenye picha hiyo mtu anayeonekana kuzimia amebebwa kwenye machela na watu wawili. Mmoja anauliza mtu huyo aliyebebwa amefanya nini? Mwingine anajibu kitu alichofanya mtu huyo na kupata matokeo ambayo hakutegemea. Watu na taasisi mbalimbali wamebadili maelezo ya mtu (more…)

#SheriaYaLeo (137/366); Tambua Wanaojificha nyuma ya jadi.

By | March 17, 2022

#SheriaYaLeo (137/366); Tambua Wanaojificha nyuma ya jadi. Wapo watu ambao wanataka kuleta mabadiliko ya aina fulani. Lakini wanajua jamii huwa haipo tayari kwa mabadiliko makubwa na ya haraka. Hivyo hujificha nyuma ya jadi, kwa kujionyesha kwamba ni watu ambao wanadumisha jadi. Wanatumia nguvu nyingi kuonekana wanakubali mfumo uliopo na wanaulinda (more…)

2632; Unachojali zaidi.

By | March 16, 2022

2632; Unachojali zaidi. Kila unachokijali zaidi kwenye maisha yako ndiyo kinapata kipaumbele kikubwa kwako. Hicho kitakuwa na nguvu ya kukusukuma ufanye au usifanye mambo muhimu unayopaswa kufanya. Chukua mfano unataka kupata fedha ili kufikia uhuru wa kifedha, lakini pia unataka kila mtu akupende. Kitendo cha kujali kuhusu kupendwa na kila (more…)

#SheriaYaLeo (136/366); Zawadi za kimtego.

By | March 16, 2022

#SheriaYaLeo (136/366); Zawadi za kimtego. Watu wenye hila ya kupata kitu fulani, huwa wanapenda kuficha nia yao kwenye kitu kingine ili wasionekane waziwazi. Moja ya maeneo ambayo watu wanaotaka kujinufaisha kupitia wengine ni utoaji zawadi. Watu hao huwa wanatoa zawadi za kimtego. Wanachofanya ni kumpa mtu zawadi ndogo, halafu baadaye (more…)

2631; Kujieleza na kujitetea.

By | March 15, 2022

2631; Kujieleza na kujitetea. Ukweli huwa unabaki kuwa ukweli, uwe unatetewa au hautetewi. Wakati mwingine ukijaribu sana kuutetea ukweli, unaanza kuonekana kama uongo. Uongo ndiyo unahitaji maelezo mengi na kutetewa ili ukubalike na wengine. Na uongo huwa unahitaji uongo mwingine mkubwa zaidi ili usianguke. Mara zote jua upo upande upi, (more…)

#SheriaYaLeo (135/366); Wajue viongozi wanaopenda kutukuzwa.

By | March 15, 2022

#SheriaYaLeo (135/366); Wajue viongozi wanaopenda kutukuzwa. Katika safari yako ya maisha na mafanikio utapita maeneo mbalimbali. Kwenye baadhi ya maeneo utakutana na viongozi ambao wanapendwa kutukuzwa. Viongozi hao huamini hawawezi kukosea. Huona kila wanachofikiri wao ndiyo sahihi zaidi na wengine wote wanakubaliana nao. Kufikiri tofauti na wao wanachukulia kama usaliti (more…)

Ongea Na Kocha; Kisima, Tathmini, Rejoyce Otaru.

By | March 14, 2022

ONGEA NA KOCHA; KISIMA, TATHMINI, REJOYCE OTARU. Karibu mwanamafanikio kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambacho kina mambo makubwa manne ya kujifunza kwenye safari yetu ya mafanikio. Jambo la kwanza ni mambo ya muhimu na ya msingi ya kuzingatia kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Kwa sasa tunapotia mageuzi makubwa kwenye KISIMA (more…)

2630; Udhaifu wako mwenyewe.

By | March 14, 2022

2630; Udhaifu wako mwenyewe. Matatizo na changamoto nyingi vimekuwa vinajirudia kwa watu, kwa sababu huwa hawakubali chanzo cha hayo. Wao hukazana kutafuta wengine wa kulaumu isipokuwa wao. Wanakuwa na ushahidi kabisa wa jinsi wengine wamehusika kwenye yale wanayopitia. Lakini hata wanapomaliza hilo, bado mengine yanaibuka. Hayakomi kwa sababu mtu anakimbilia (more…)

#SheriaYaLeo (134/366); Watambue wenye majigambo kabla hawajakunasa.

By | March 14, 2022

#SheriaYaLeo (134/366); Watambue wenye majigambo kabla hawajakunasa. Watu wenye majigambo yaliyopitiliza (Narcissists) ni watu ambao ndani yao hawajiamini. Wanatumia majigambo hayo kuficha udhaifu huo mkubwa ulio ndani yao. Watu hao huwa wanajiona wao ni muhimu kuliko watu wengine na hivyo hutaka watu wote wawatii wao. Huwa wanataka kila mtu awe (more…)