Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Zingatia haya kuendesha biashara yenye mafanikio.

By | August 10, 2015

Kama kuna kitu muhimu kwa kila mfanyabiashara, basi ni muda. Kuna wakati unatamani siku ingekuwa na masaa mawili au matatu ya ziada ili uweze kukamilisha majukumu yako ya kibiashara. Katika wakati huu unakuta umeacha kuimiliki biashara na biashara inaanza kukumiliki wewe. Hii ni hali ya hatari sana kwenye maisha yako (more…)

Biashara ni uaminifu na sio pata potea.

By | August 3, 2015

Katika matatizo mengi ambayo wafanyabiashara na wajasiriamali wanakutana nayo kila siku kwenye maisha yao ya kibiashara, mengi yanaanzia kwenye mtazamo wao juu ya biashara wanayofanya. Hiki kinakuwa kikwazo kikubwa sana kwao kuendesha biashara yenye mafanikio. Kwa kuwa mtazamo ni kitu kinachoanzia ndani ya mtu kabisa, hata pale mtu anapopata elimu (more…)

BIASHARA LEO; Tafuta Mlango Wa Kutorokea Na Jua Wakati Wa Kutoroka.

By | July 24, 2015

Biashara unayofanya sasa, haitakuwa hivyo ilivyo kwa miaka kumi ijayo. Japo kipindi hiko kuna watu ambao bado watakuwa wanaifanya kama inavyofanywa sasa. Ila hawa ni wale ambao wanaendesha biashara za kawaida, zinazowaumiza vichwa na zisizo na faida kubwa. Wajanja wote kwenye biashara wajua mlango wa kutorokea na wakati wakutoroka. Bado (more…)

Mambo yanapokwenda vibaya kwenye biashara yako fanya hivi.

By | July 20, 2015

Mara nyingi wafanyabiashara huwa tunakuwa na mipango mizuri sana ya mambo yanapokwenda vizuri. Na mipango yetu hii tumeiweka tukiamini kwamba mambo yatakwenda vizuri wakati wote. Lakini haya ni maisha, na kama ilivyo sheria ya maisha, hakuna kitu kilichonyooka, hata bara bara nzuri bado ina kona. Hivyo kuna wakati kwenye biashara (more…)

Tatizo la kuajiri wafanyakazi wasio na sifa kwenye biashara yako.

By | July 13, 2015

Mapinduzi ya viwanda yaliyotokea takribani karne mbili zilizopita yalileta mabadiliko makubwa sana kwenye ufanyaji wa kazi. Kabla ya hapo hakukuwa na ajira rasmi na hivyo watu wengi walizalisha kwa kiwango kidogo na kubadilishana. Viwanda vilipokuja viliweza kuzalisha kwa kiwango kikubwa sana na hivyo kuhitaji wafanyakazi wengi. Na kwa kuwa wafanyakazi (more…)

BIASHARA LEO; Je Biashara Yako Inaendana Na Wateja Wako?

By | July 10, 2015

Tulishasema kwamba jambo muhimu kabisa kwenye biashara ni kujua mteja wako ni nani. Kama upo kwenye biashara na humjui mteja wako basi hujui ni nini unafanya kwenye biashara yako. Na ninaposema kumjua simaanishi kumjua kwa jina, bali kujua sifa za mteja wako kuanzia umri, kipato, anakoishi na mengine kama hayo. (more…)

BIASHARA LEO; Hili ndio tatizo la kushindana kwa bei na linavyokumaliza.

By | July 9, 2015

Tatizo la kushindana kwa bei kwenye biashara ni kwamba linawamaliza wote mnaoshindana. Watu wengi huwa wanafikiri kwamba kwa kuweka bei ndogo basi ndio wanavutia wateja wengi. Hivyo wanaweka bei ndogo na mwanzoni wateja wanakuja kweli, baadae mshindani wako naye anashusha bei na wateja wanaenda kwake tena. Mnafanya mchezo huu kwa (more…)

BIASHARA LEO; Je Umemridhisha Mteja Wako Leo?

By | July 8, 2015

Kama jibu lako ni sina mteja basi jitathmini vizuri. Kwanza kabisa kila mmoja wetu ana mteja, kama wewe ni mtu mzima na unaishi basi una mteja au una wateja wengi sana. Wateja hawaishii kwa wafanyabiashara tu. Wateja wapo kwa kila mtu. Kama wewe ni mfanyabiashara, mteja wako au wateja wako (more…)

SABASABA, mambo muhimu kwa kila mfanyabiashara kutafakari kwenye msimu huu.

By | July 6, 2015

Tarehe saba ya mwezi wa saba kila mwaka ni sikukuu ya wafanyabiashara. Ni siku maalumu ambayo imetengwa na serikali kwa ajili ya wafanyabiashara kuazimisha kile ambacho wamekuwa wanafanya kwenye biashara zao. Msimu huu wa sabasaba kila mwaka hutawaliwa na maonesho ya kibiashara kwenye viwanja mbalimbali nchini. Wafanyabiashara wengi wamekuwa wakitumia (more…)

BIASHARA LEO; Sikiliza Hawa Watu Wanaokupa Mawazo Ya Biashara Kila Siku.

By | July 3, 2015

Nikimaliza kuandika hapa na mtu akasoma, bado ataniandikia kwamba anatafuta wazo la biashara. Yaani wazo la biashara limechukuliwa kama ni kitu kikubwa sana ambacho watu wanapigana nacho ili wakipate. Ni kama ukishapata wazo basi mambo yako yote yamenyooka. Nimekuwa nikisema mara kwa mara mwamba wazo la biashara linaanza na wewe (more…)