Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Mambo matano(5) muhimu ambayo hujawahi kuambiwa kuhusu ujasiriamali.

By | November 16, 2015

Watu wengi wanaingia kwenye ujasiriamali kwa sababu wanaona ndio sehemu nzuri ya kujitengenezea kipato huku ukiwa na uhuru mkubwa. Ni kweli kabisa kwamba ujasiriamali unakupatia uhuru mkubwa. Lakini pia kuna mambo mengi ambayo watu wengi wanaoingia kwenye ujasiriamali huwa hawajui mpaka pale wanapokutana nayo. Na hata baada ya kukutana nayo (more…)

Mbinu bora za kupata wafanyakazi sahihi wa biashara yako.

By | November 9, 2015

Ili biashara yako iweze kukua na kukuletea mafanikio makubwa, unahitaji watu makini sana wa kukusaidia kwenye biashara yako. na ili uweze kupata watu hawa makini ni lazima wewe mwenyewe uwe makini kwenye kuajiri. Wafanyabiashara wengi wamekuwa na malengo mazuri sana na biashara zao na wamekuwa wakijitoa sana ili biashara zao (more…)

Sababu za biashara kushindwa ni za ndani na sio nje ya biashara.

By | November 2, 2015

Karibu tena kwenye kona yetu hii ya mjasiriamali ambapo tunajifunza mambo muhimu kuhusu biashara na ujasiriamali. Kupitia kona hii unapata mbinu mbalimbali za kuiwezesha biashara yako kwenda vizuri na wewe kufikia malengo yako ya kibiashara. Kama wote tunavyojua biashara zina changamoto nyingi. Kabla hujaingia kwenye biashara unaweza kuwa na mipango (more…)

Kwa nini mchanganuo wa biashara yako ni muhimu sana kwako.

By | October 19, 2015

Wafanyabiashara wengi huwa hawaandai michanganuo ya biashara yao kwa matumizi yao wenyewe. Wengi hulazimika kuandaa michanganuo pale ambapo wanahitajika kufanya hivyo na taasisi mbalimbali. Labda mfanyabiashara anataka kuchukua mkopo na moja ya vigezo na masharti ya mkopo ni kuwasilisha mchanganuo wa biashara na jinsi mkopo huo utakavyotumika. Wafanyabiashara wengi huandaa (more…)

Jiridhishe na mambo haya kabla hujasema NDIO kwa mkopo wa biashara.

By | October 12, 2015

Ili biashara yako iweze kukua, unahitaji ongezeko la mtaji kadiri muda unavyokwenda. Na mtaji wako unaweza kuuongeza kutokana na faida unayopata kwenye biashara, japo hii itakuchukua muda mrefu. Lakini pia unaweza kuongeza mtaji wa biashara yako kwa kupokea fedha nyingi kwa wakati mmoja kutoka kwa watu au taasisi mbalimbali. Fedha (more…)

Mambo muhimu ya kuzingatia pale unapoanza biashara na mtaji mdogo.

By | September 28, 2015

Moja ya maswali ambayo huwa napokea sana kutoka kwa watu wanaotaka kuanza biashara huwa ni biashara gani waanze kwa mtaji kidogo wanaokuwa nao. Mfano wa swali huwa, “nina laki tano, naweza kuanza biashara gani kwa kiasi hiki cha fedha?” swali hili huwa linaulizwa mara nyingi sana kwa viwango vidogo na (more…)

Jinsi ya kutengeneza bajeti ya matumizi mazuri ya muda wako kama mjasiriamali.

By | August 31, 2015

Wajasiriamali na wafanyabiashara wote tunajua ni jinsi gani ilivyo changamoto kuendesha biashara. Japokuwa wengi hufikiri kuendesha biashara ni kuwa na uhuru mkubwa, bado changamoto ni nyingi sana. Ni changamoto hizi ndio zinazuia wafanyabiashara wengi kukua na kusababisha wengine kushindwa kabisa. Changamoto za kibiashara zinaweza kusababishwa na mambo mengi sana, matatizo (more…)

Matatizo yote kwenye biashara yanaanza na kitu hiki kimoja.

By | August 24, 2015

Wewe kama mfanyabiashara, kipato unachopata kinatokana na fedha ambazo mteja analipa. Gharama zote za kuendesha maisha yako zinazotokana na biashara ni kwa sababu kuna mteja ambaye ametoa fedha zake ili kupata huduma au bidhaa unazotoa. Kwa kifupi tunaweza kusema kwamba bosi hasa wa biashara yako ni mteja wako. Hii ni (more…)

BIASHARA LEO; Wauzie Wanaoijua Thamani Unayotoa.

By | August 21, 2015

Moja ya njia unazotumia kupoteza muda na rasilimali nyingine kwenye biashara yako, ni kujaribu kumuuzia kila mtu kile unachouza. Ni vigumu sana kila mtu kuona thamani ya ile biashara ambayo unafanya. Hivyo katika harakati zako za kutafuta wateja utakutana na watu wengi. Kuna ambao wataiona thamani na kuchukua hatua haraka, (more…)

Kama mteja ataacha kufanya biashara na wewe, ataenda wapi?

By | August 17, 2015

Ni rahisi sana kutabiri kama biashara yako itafanikiwa au haitafanikiwa. Japo watu wengi huwa hawachukui hatua hii muhimu. Kwenye biashara yako, kwa bidhaa au huduma unayotoa, wewe mwenyewe kwenye moyo wako unaweza kuwa unajua kama unatoa thamani kweli au hutoi thamani. Leo tutajadili swali moja muhimu sana unalotakiwa kujiuliza kila (more…)