Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2430; Unaona kile unachotaka kuona…

By | August 26, 2021

2430; Unaona kile unachotaka kuona… Sisi binadamu kwa kujidanganya huwa tupo vizuri sana. Ila huwa hatujui kama tunajidanganya, tunakuwa na ukakika tumesimama kwenye ukweli. Ila ni mpaka pale uzio ulio kati ya ukweli na uongo unapoanguka ndiyo tunaona wazi tulikuwa tunajidanganya. Huwa tunaona kile tunachotaka kuona na kukusanya ushahidi unaoendana (more…)

2429; Wa mwisho kwako, wa kwanza kwake…

By | August 25, 2021

2429; Wa mwisho kwako, wa kwanza kwake… Kitu kimoja kikubwa ambacho najifunza kwenye taaluma ya udaktari ni mitazamo tofauti ambayo daktari na mgonjwa wanakuwa nayo. Kama daktari unaweza kuwa kwenye zamu ya kuona wagonjwa na umekaribia mwisho kabisa wa zamu yako, umechoka na anakuja mgonjwa wa mwisho. Wewe daktari unaweza (more…)

2428; Mafanikio yako ni hatari kwa wengine…

By | August 24, 2021

2428; Mafanikio yako ni hatari kwa wengine… Kabla hujafanikiwa, watu wanakuchukulia poa. Kwanza wanajua hutaweza kufanikiwa sana, hivyo huwi hatari kwake. Unapofanikiwa kwa viwango vya juu na kuwapita wao kimafanikio, ghafla wanabadilika na kuanza kuwa kikwazo kwako. Wanafanya hivyo kwa sababu wanakuona wewe ni hatari kwao, na hatari hiyo inatokana (more…)

2427; Makasiriko…

By | August 23, 2021

2427; Makasiriko… Katika hali yoyote ile, aliyekasirika ndiye mwenye matatizo. Yaani kama kuna mtu amekukasirisha, tatizo siyo mtu huyo, bali tatizo ni wewe uliyekasirika. Kwa maana nyingine, ukikasirika maana yake una matatizo. Na wewe angalia wazi tu ni wakati gani unakasirika. Mara nyingi ni moja kati ya nyakati hizi tatu. (more…)

2426; Kusikia na kuona…

By | August 22, 2021

2426; Kusikia na kuona… Kama unachosikia kinatofautiana na unachoona, amini kile unachoona. Uongo huwa ni rahisi sana kusemwa, lakini ni mgumu kuonyeshwa. Kwenye kila aina ya uongo, huwa kuna ukweli unaoonekana wazi, lakini kwa sababu tunataka sana kusikia kile tunachotaka, tunaishia kudanganywa. Ni vigumu sana kudanganywa kama macho yako yatakuwa (more…)

2424; Kipi kina nguvu ya kukuzuia?

By | August 20, 2021

2424; Kipi kina nguvu ya kukuzuia? Kama kuna kitu kina uwezo wa kukuzuia kupata kile unachotaka, basi ukweli ni kwamba hutaweza kukipata. Kwa sababu dunia huwa siyo nyepesi kutoa kile ambacho mtu anataka, huwa inapima kwanza ni kwa kiasi gani mtu huyo amejitos kukipata. Kama hujajiambia utapata unachotaka na hakuna (more…)

2423; Hakuna mawazo yako peke yako…

By | August 19, 2021

2423; Hakuna mawazo yako peke yako… Umewahi kupata wazo la kitu fulani, labda ni fursa nzuri umeiona na kujiambia utafanyia kazi baadaye. Halafu siku si nyingi unakuta watu wengine wameshafanyia kazi wazo hilo hilo? Hilo hutokea kila mara. Wakati mwingine unamwambia mtu kitu anakuambia alikuwa anafikiria hivyo hivyo. Mawazo tunayoyapata (more…)

2422; Siyo kweli..

By | August 18, 2021

2422; Siyo kweli.. Siyo kweli kwamba umeshafanya kila kinachowezekana kufanyika, kuna vingi hujafanya, hivyo endelea kufanya. Siyo kweli kwamba umeshamfikia kila mtu, kuna wengi hujawafikia, endelelea kuwafikia wengi zaidi. Siyo kweli kwamba kila kitu kimeshasemwa, bado dunia haijasikia sauti yako. Siyo kweli kwamba huna muda, hujaupangilia tu vizuri. Chochote unachojiambia (more…)

2421; Siyo kila ushauri unakufaa…

By | August 17, 2021

2421; Siyo kila ushauri unakufaa… Nianze kwa kusema kila kitu kwenye biashara kinawezekana. Na kwa biashara yoyote unayofanya, watu watakuja kwako na ushauri wa kila aina. Na kila ushauri unaopewa utaonekana ni sahihi kabisa na wenye tija kwa biashara. Lakini siyo kila ushauri unakufaa wewe na biashara yako. Unapoingia kwenye (more…)