#SheriaYaLeo (118/366); Epuka vitu vya bure.

By | February 26, 2022

#SheriaYaLeo (118/366); Epuka vitu vya bure. Epuka sana vitu unavyopewa na wengine bure, kwa sababu huwa vina mtego wa kukunasa uwe mtumwa kwao. Watu wanaokupa au kukufanyia vitu bure bila kudai malipo yoyote, baadaye huja na matakwa makubwa kwako ambayo yanazidi hata fedha ambayo ungewalipa. Wengine kwa kukusaidia watatumia hilo (more…)

2613; Sasa na baadaye.

By | February 25, 2022

2613; Sasa na baadaye. Chochote kinachokulipa vizuri sasa, hakitakulipa vizuri baadaye. Chochote kinachokupa raha sasa, kitakuumiza baadaye. Ni kitu kinachoweza kuonekana ni kigumu, lakini ndivyo asili ilivyo. Vizuri huwa haviambatani kwa pamoja Kupata kimoja lazima uwe tayari kupoteza kingine. Kitu ambacho ni tofauti kabisa na asili yetu binadamu. Ambao huwa (more…)

#SheriaYaLeo (117/366); Yafanye mafanikio yako yaonekane siyo ya juhudi kubwa.

By | February 25, 2022

#SheriaYaLeo (117/366); Yafanye mafanikio yako yaonekane siyo ya juhudi kubwa. Sisi binadamu huwa tunavutiwa na mafanikio ya watu wengine. Huwa tunakubali pale mtu anapoweja juhudi na kupata mafanikio makubwa. Lakini inapotokea mtu amepata mafanikio makubwa bila kuonekana akiweka juhudi kubwa, tunamkubali zaidi. Tunaona ana uwezo mkubwa na vipaji vya kipekee. (more…)

2612; Kushughulika na watu.

By | February 24, 2022

2612; Kushughulika na watu. Changamoto na migogoro mingi unayokutana nayo kwa watu wengine vinatokana na wewe kusahau jambo hili la msingi kabisa. Kwamba binadamu ni viumbe wa kihisia na siyo viumbe wa kimantiki. Kwamba wanafanya maamuzi yao kwa hisia na kisha kuyahalalisha kwa mantiki. Na kubwa kabisa ni kwamba hisia (more…)

#SheriaYaLeo (116/366); Chukua Hatua Kwa Ujasiri.

By | February 24, 2022

#SheriaYaLeo (116/366); Chukua Hatua Kwa Ujasiri. Wengi wetu huwa ni waoga. Tunapenda kuepuka mivutano na migogoro na tunataka kukubalika na wote. Tunaweza kufikiria kufanya jambo la kijasiri, lakini huwa vigumu kutekeleza. Huwa tunaficha woga wetu kwa kujiambia tunajali wengine na hatutaki kuwaumiza. Lakini huo siyo ukweli, tunachohofia zaidi ni wengine (more…)

2611; Maoni ya wengine.

By | February 23, 2022

2611; Maoni ya wengine. Mstoa Marcus Aurelius amewahi kunukuliwa akisema, kila mtu anajipenda na kujiheshimu, lakini anaishia kuyapa maoni ya wengine uzito kuliko maoni yake binafsi. Wengi tunasahau kwamba maoni siyo ukweli au uhalisia. Bali ni kile ambacho watu wanafikiria kwa wakati huo, ambacho pia ni rahisi sana kunadilika baada (more…)

#SheriaYaLeo (115/366); Epuka muungano wa uongo.

By | February 23, 2022

#SheriaYaLeo (115/366); Epuka muungano wa uongo. Hakuna mtu anayeweza kufanikiwa peke yake kwenye maisha bila ya kuungana na wengine. Tunategemeana sana katika safari ya maisha na mafanikio. Lakini siyo kila muungano una manufaa kwako. Kuna muungano wa uongo na muungano wa kweli. Unapaswa kujua tofauti za aina hizo za muungano (more…)

2610; Jenga.

By | February 22, 2022

2610; Jenga. Kila kitu tunachonufaika nacho leo hapa duniani ni kwa sababu watu walichukua hatua ya kukijenga. Chakula, mavazi, nyumba, magari na mengine yote, ni matokeo ya watu kujenga. Watu walioweza kujenga yote tunayofurahia sasa, walikuwa na maono makubwa ambayo wengine hawakuamini yangewezekana. Laki kwa kujiamini na kufanyia kazi, mwishowe (more…)

#UkurasaWaLeo (114/366); Waepuke wenye kisirani.

By | February 22, 2022

#UkurasaWaLeo (114/366); Waepuke wenye kisirani. Kuna watu mbalimbali ambao wamepitia magumu na kushindwa kwenye maisha. Huwa tunasukumwa kuwaonea huruma watu hao na kuchukua hatua mbalimbali kuwasaidia. Lakini siyo wote wanaofaa kusaidia. Wapo ambao magumu na kushindwa wanakopitia wanakuwa wamejitakia wenyewe. Hao ni watu wenye kisirani na mikosi ambao kwa tabia (more…)

ONGEA NA KOCHA; Tathmini Ya Robo Mwaka, Kigawe Kikuu Cha Mafanikio, Instant Cashflow.

By | February 21, 2022

Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambacho kina mambo yafuatayo. Moja ni mrejesho wa tathmini za robo mwaka ya kwanza kwenye mwaka wa mafanikio 2021/2022. Nimeshirikisha yale muhimu kutoka kwenye tathmini hizo na namna ya kujiandaa vyema kwa tathmini ijayo. Mbili ni andiko la KIGAWE KIKUU CHA MAFANIKIO (THE (more…)