#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako

By | November 23, 2021

#SheriaYaLeo (23/366); Yagawe malengo yako makubwa kwenye vipande vidogo. Kuwa na malengo makubwa na ya muda mrefu kunakupa msukumo na umakini mkubwa wa kuyafikia. Malengo hayo ambayo ni makubwa, mfano biashara kubwa ya kujenga huwa yanakupa shauku kubwa na kukusukuma uwe bora zaidi. Lakini pia malengo hayo makubwa huwa yana (more…)

ONGEA NA KOCHA; Kisima Ni Jeshi, Amri 21 Za Maisha na Godfrey Mbise.

By | November 22, 2021

Habari Mwanamafanikio? Karibu usikilize kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kwa juma hili kuna mambo makubwa matatu. Moja ni mafanikio ni vita, KISIMA CHA MAARIFA ni jeshi na wewe ni mwanajeshi kwenye hii vita. Hapa utajifunza kwa ufupi sifa za wanajeshi wa Sparta na mambo muhimu ya kuzingatia kwenye jeshi (more…)

2518; Mabadiliko na Msimamo.

By | November 22, 2021

2518; Mabadiliko na Msimamo. Kwenye safari ya mafanikio na maisha kwa ujumla, kuna njia panda moja kubwa ambayo wengi huwa hawaielewi. Kuna mambo ambayo yanabadilika kila wakati. Na kuna mambo ambayo hayabadiliki kabisa. Njia panda inakuwa ni kujua mambo gani yanabadilika ili kubadilika nayo na mambo gani hayabadiliki ili kuwa (more…)

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu.

By | November 22, 2021

#SheriaYaLeo (22/366); Tumia ukinzani na magumu. Ufunguo wa mafanikio kwenye tasnia yoyote ile ni kujijengea ujuzi wa aina mbalimbali kisha kuchanganya ujuzi huo kwa namna ya kipekee. Lakini mchakato wa kufanya hivyo unaweza kuwa mgumu, wenye maumivu na kukatishwa tamaa. Maana kadiri unavyokwenda unagundua ukomo na ukosefu wa ujuzi muhimu. (more…)

2517; Kuiga mafanikio ni kujipoteza.

By | November 21, 2021

2517; Kuiga mafanikio ni kujipoteza. Pamoja na siri nyingi za mafanikio kuwa bayana. Pamoja na hadithi za watu waliofanikiwa kupatikana kwa urahisi kila mahali. Bado ni wachache sana wanaopata mafanikio makubwa. Tulidhani kwenye zama hizi ambapo maarifa ya mafanikio yanapatikana kwa wingi na urahisi basi wengi wangekuwa wamefanikiwa, lakini hali (more…)

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni

By | November 21, 2021

#SheriaYaLeo (21/366); Kuwategemea wengine ni tatizo. Hakuna kitu kibaya kama kuweka mategemeo yako yote kwa watu wengine. Utegemezi unakuweka kwenye hatari ya kuathiriwa na hisia hasi kama usaliti, kukatishwa tamaa, kuvurugwa na msongo. Hisia hizi huharibu sana utulivu wa akili yako. Kujitegemea mwenyewe ni muhimu sana kwa utulivu na mafanikio (more…)

2516; Makosa yanayojirudia rudia.

By | November 20, 2021

2516; Makosa yanayojirudia rudia. Kwenye kazi au biashara unayoifanya, kuna makosa huwa yanajirudia rudia kila mara. Unaweza kulalamikia makosa ya aina hii, lakini ni fursa nyingine nzuri ya kuboresha kile unachofanya na kujenga mfumo unaozuia hayo yasijirudie. Kwa kila kosa linalojirudia rudia, kaa chini uandike nini kinafanya kosa hilo lijirudie (more…)

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi.

By | November 20, 2021

#SheriaYaLeo (20/366); Ona Ubobezi Kama Ukombozi. Dunia imejaa matatizo mbalimbali, na sehemu kubwa ya matatizo hayo tumeyatengeneza wenyewe. Kutatua matatizo hayo kunahitaji juhudi na ubunifu mkubwa. Kutegemea mazoea, teknolojia na kuwa mwema haitatusaidia. Tunahitaji nguvu ya kuweza kuyatambua matatizo hayo na kutengeneza taasisi mpya zinazoweza kukabiliana na mabadiliko tunayopitia. Ni (more…)

2515; Maswali yanayoulizwa mara kwa mara.

By | November 19, 2021

2515; Maswali yanayoulizwa mara kwa mara. Kwa shughuli yoyote unayofanya, iwe ni kazi au biashara, kuna maswali ambayo wale unaowahudumia huwa wanayauliza mara kwa mara. Kwa kiingereza huwa wanaita FAQ (Frequently Asked Questions). Haya ni maswali yanayoweza kukukera na kuona kwa nini watu hawaelewi vitu vidogo na vya kawaida kiasi (more…)

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya

By | November 19, 2021

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya Ndani. Upo hapa duniani siyo tu kwa ajili ya kutimiza tamaa zako na kutumia vile wengine wametengeneza, bali pia kuchangia, kutimiza kusudi kubwa. Ili kuweza kutimiza kusudi hilo, lazima utengeneze kile cha kipekee ndani yako. Acha kusikiliza sana maneno na maoni ya wengine wanaokuambia (more…)