#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka.

By | November 28, 2021

#SheriaYaLeo (28/366); Njia haijanyooka. Wakati unaianza safari yako ya wito na kusudi la maisha yako, unachagua eneo linaloendana na yale yaliyo ndani yako. Sehemu unayoanzia inakupa nafasi ya kujifunza na kujijengea ujuzi na uzoefu muhimu. Pia inakupa nafasi ya kuingiza kipato na kujijengea kujiamini. Kadiri unavyokwenda unagundua kuna njia za (more…)

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka.

By | November 27, 2021

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka. Zoezi la kutoa na kupokea ushauri limekuwa zoezi lisilo na manufaa kwa wengi wanaoshiriki. Hiyo ni kwa sababu watu wengi wanaoomba ushauri, siyo kama wanataka ushauri kweli, ila wanataka wajue kama maamuzi waliyofanya ni sahihi. Yaani ndani yao wanakuwa tayari wameshafanya maamuzi, ila wanaomba ushauri (more…)

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio.

By | November 27, 2021

#SheriaYaLeo (27/366); Siri Kuu Ya Mafanikio. Tangu enzi na enzi, watu wamekuwa wanatafuta njia za mkato na kanuni zahisi za kufanikiwa. Lakini mwisho wa siku wanaishia kupotea, kwa sababu hivi ni vitu ambavyo havipo kabisa. Wakati unahangaika kutafuta njia hizo za mkato zisizokuwepo, unapuuza nguvu kubwa ambayo tayari ipo ndani (more…)

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji?

By | November 26, 2021

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji? Kwenye safari ya mafanikio, hakuna sumu kubwa kama ujuaji. Sumu hii huanza pale mtu anapoona yale anayofundishwa tayari anayajua. Kwa sababu maarifa na siri za mafanikio ni zile zile, wengi hufika mahali na kuona wameshajua kila kitu, hakuna tena kitu kipya. (more…)

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia

By | November 26, 2021

#SheriaYaLeo (26/366); Epuka Nguvu Zinazokuzuia Usifikie Ubobezi. Una nguvu kubwa ndani yako ambayo inakufanya wa tofauti na wa kipekee, nguvu hiyo ndiyo imebeba wito na kusudi lako. Lakini pia kuna nguvu kubwa za nje ambazo zinaipinga nguvu hiyo ya ndani na kukuzuia usiweze kuitumia ili kujitofautisha na kufanya makubwa. Nguvu (more…)

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali.

By | November 25, 2021

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali. Watu wawili, wanaweza kuwa wanafanya kazi au biashara ya aina moja, mmoja akafanikiwa sana na mwingine akashindwa kabisa. Watu wamekuwa wakitafuta sababu za tofauti hiyo, wakiona labda ni bahati, fursa, upendeleo na uwezo tofauti. Yote hayo yanaweza kuchangia, ila kuna kimoja kikubwa ambacho huwa hakipewi (more…)

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo.

By | November 25, 2021

#SheriaYaLeo; Badilika kuanzia ndani kidogo kidogo. Sisi binadamu huwa tunahangaika na yale tunayoweza kuona kwa macho yetu. Tunapoangalia mabadiliko kwenye maisha ya wengine, tunaona bahati nzuri ambayo mtu aliipata kwa kukutana na mtu aliyemsaidia sana. Tunaona miradi iliyomletea mtu fedha na umaarufu. Kwa maneno mengine tunaona manadiliko yanayoonekana kwa nje. (more…)

2520; Mahali unapojificha.

By | November 24, 2021

2520; Mahali unapojificha. Kila mmoja kuna mahali huwa anajificha inapokuja kwenye uhitaji wa kufanya makubwa ili kufanikiwa. Kufanya hayo makubwa ni kugumu na pia matokeo siyo ya uhakika sana. Wakati huo sisi binadamu huwa ni wavivu na tunapenda vitu vya uhakika. Hivyo tunapokabiliwa na kitu kikubwa cha kufanya mbele yetu, (more…)

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea.

By | November 24, 2021

#SheriaYaLeo (24/366); Unganisha yale unayopendelea. Wakati mwingine kusudi na wito wako hautokani na kitu kimoja, bali unatokana na kuunganisha vitu ambavyo unapendelea kufanya. Kwa kujua vitu hivyo na kuviunganisha pamoja unaweza kutengeneza kitu cha kipekee kabisa kwako. Kama bado ni kijana na ndiyo unaianza safari yako, unapaswa kujaribu mambo mbalimbali (more…)

2519; Tatizo siyo muda, bali nguvu.

By | November 23, 2021

2519; Tatizo siyo muda, bali nguvu. Nimeshaliandikia hili hapa mara kadhaa, lakini nitaendelea kulirudia kwa sababu ni dhana ambayo wengi hawaielewi. Tumezoeshwa sana kuhangaika na muda. Tukafundishwa jinsi ya kupangilia na kudhibiti muda wetu ili kuweza kufanya makubwa. Tumekuwa tunaambiwa wazi kabisa kwamba muda ni zaidi ya fedha, maana ukipoteza (more…)