#TAFAKARI YA LEO; KUWA MAKINI NA UNACHOFANYA…

By | April 28, 2021

Unaweza kuwa bize kweli kweli, kila siku unachoka sana, lakini unayofanya yakawa ni kikwazo kwa unachotaka. Hili ndiyo linazuia wengi wasifanikiwe, wanahangaika na mambo ambayo siyo tu hayawasaidii, bali pia yanawazuia wasipate wanachotaka. Kila unachofanya, jiulize kwanza kama kitakufikisha unakotaka na kuwa na ushahidi kutoka kwa wale ambao wameshafika unakotaka (more…)

2309; Vitu vya kushangaza…

By | April 27, 2021

2309; Vitu vya kushangaza… Waliofanikiwa wanajua kuna mengi hawajui na hivyo kuwa tayari kuendelea kujifunza kupitia kila fursa wanayoweza kuitumia. Ambao hawajafanikiwa wanaamini wanajua kila kitu na hawana haja ya kijifunza, na hivyo hawajifunzi. Matajiri wana fedha nyingi, lakini matumizi yao huwa siyo makubwa. Masikini hawana fedha, ila matumizi yao (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUPATA UNACHOTAKA…

By | April 27, 2021

Kupata chochote kile unachotaka, kunahitaji ushujaa wa hali ya juu sana, maamuzi ya kwamba lazima utakipata na ung’ang’anizi mpaka ukipate. Kama chochote kinaweza kukuzuia, hutapata unachotaka, lazima uwe ambaye huwezi kuzuiwa na chochote. Ambaye umeamua utapata unachotaka au utakufa ukiwa unapambana kukipata, hakuba chaguo jingine. Ukurasa wa kusoma ni mambo (more…)

2308; Mambo muhimu ya kujikumbusha…

By | April 26, 2021

2308; Mambo muhimu ya kujikumbusha… Katika safari ya mafanikio, unakabiliana na mambo mengi kiasi kwamba usipojikumbusha yale muhimu unaweza kuyasahau na ukajiingiza kwenye wakati mgumu. Hapa kuna mambo muhimu ya kujikumbusha katika safari hii ya mapambano. Usijiwashe moto ili kuwapa joto wengine. Ni muhimu kuwajali wengine na kuweka maslahi yao (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MWENYE MACHAGUO MENGI NDIYE MWENYE NGUVU…

By | April 26, 2021

Kama mtu ana kitu ambacho watu wengi wanakihitaji na hawawezi kukipata pengine, huyo ana nguvu ya kukiuza kwa namna anavyotaka yeye. Kama watu wanaweza kupata wanachotaka popote, wana nguvu ya kuchagua wakapate wanachotaka wapi. Mwenye machaguo mengi ndiye mwenye nguvu ya kuamua apate kiasi gani kwenye majadiliano yoyote yale. Kama (more…)

2307; Wanachokulipa ndiyo thamani yako…

By | April 25, 2021

2307; Wanachokulipa ndiyo thamani yako… Ni kawaida kuwasikia watu walioajiriwa wakilalamika kwamba waajiri wao wanawalipa mshajara kidogo, ambao hauendani kabisa na thamani yao. Pia wapo waliojiajiri na walio kwenye biashara ambao wanalalamika kipato au faida wanayoingiza ni ndogo ukilinganisha na thamani yao. Iko hivi rafiki, kama umeajiriwa na mwajiri wako (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KINACHOFANYA MAISHA YAWE MAGUMU….

By | April 25, 2021

Ni kufanya mambo rahisi, kuishi kwa mazoea na kuigiza maisha. Unafanya mambo rahisi kwa sababu hutaki kuchoka, kusumbuka wala kuumia, hutaki pia kushindwa. Unafanya kwa mazoea kwa sababu hutaki kufikiri tofauti na unahofia kujaribu vitu vipya kwa kuwa huna uhakika navyo. Unaigiza maisha kwa kutaka uonekane tofauti na uhalisia wako (more…)

2306; Hadhi inaanzia mfukoni…

By | April 24, 2021

2306; Hadhi inaanzia mfukoni… Kuna watu hawana fedha, lakini wakishauriwa hatua za kuchukua ili watoke kwenye hali hiyo ya kutokuwa na fedha huwa wanaleta ubishi. Wanasema hawawezi kuchukua hatua hizo kwa sababu zitashusha hadhi yao. Iko hivi rafiki, kama huna fedha, hakuna njia halali ya kuingiza fedha ambayo siyo ya (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIKUBALI WATU HAWA WAKUBABAISHE…

By | April 24, 2021

Utakapochagua kuishi maisha ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa, watu wanaokuzunguka hawatapendezwa na hilo. Watakupinga, kukukatisha tamaa na hata kukushauri namna unavyopaswa kuyaishi maisha yako. Cha kushangaza sasa, watu hao hawajui hata wanavyopaswa kuyaishi maisha yao, lakini wanaona ni wajibu wao kukupangia wewe jinsi ya kuishi. Kama utawasikiliza watu hao, utakuwa (more…)