#SheriaYaLeo (290/366); Pima watu kama wana wivu.

By | August 17, 2022

#SheriaYaLeo (290/366); Pima watu kama wana wivu. Wivu ni moja ya hisia ambazo binadamu huwa tunakuwa nazo. Ni hisia inayochochewa na hali ya mtu kujilinganisha na wengine na kutokupenda pale wengine wanapokuwa wamemzidi. Wivu huweza kumsukuma mtu kufanya mabaya na kuwadhuru wengine kwa kutokupendezwa na namna walivyowazidi. Katika mahusiano na (more…)

2785; Kuanza na kuendelea.

By | August 16, 2022

2785; Kuanza na kuendelea. Mashine yoyote ile, huwa inatumia nishati kubwa zaidi kwenye kuanza kuwaka kuliko kuendelea kuwaka. Chukua mfano wa injini ya gari au ndege, inapowashwa na kuanza safari inatumia mafuta mengi. Lakini baada ya kuwaka na kuwa kwenye mwendo, mafuta yanayohitajika ili kuendelea na mwendo yanakuwa madogo kuliko (more…)

#SheriaYaLeo (289/366); Epuka nguvu ya kubadilishwa na kundi.

By | August 16, 2022

#SheriaYaLeo (289/366); Epuka nguvu ya kubadilishwa na kundi. Sisi binadamu ni viumbe wa kijamii, huwa tunapenda sana kuwa ndani ya makundi ya watu wengine. Lakini makundi hayo huwa yana nguvu kubwa ya kutubadili kwa namna tunavyofikiri, kusema na kufanya. Ndani ya kundi tunajikuta tukijilinganisha na wengine na kujali wanatuchukuliaje. Bila (more…)

2784; Tatizo ni kujidanganya.

By | August 15, 2022

2784; Tatizo ni kujidanganya. Mwanafizikia Richard Feynman aliwahi kunukuliwa akisema jukumu lako la kwanza kwenye maisha ni kutokujidanganya wewe mwenyewe. Na hakuna mtu rahisi kumdanganya kama wewe mwenyewe. Kauli hiyo ina ukweli mkubwa sana ambao ukiuelewa na kuufanyia kazi hakuna kitu kitakachokushinda kwenye maisha yako. Kitu cha kwanza kabisa unachopaswa (more…)

#SheriaYaLeo (288/366); Kabili upande wako mbaya.

By | August 15, 2022

#SheriaYaLeo (288/366); Kabili upande wako mbaya. Kila mmoja wetu ana upande wake ambao ni mbaya. Kuna tabia fulani na madhaifu ambayo mtu unakuwa nazo ambazo umekuwa unajaribu kuvificha kwa sababu havikubaliki kijamii. Kwa nje umejenga tabia na mwonekano ambao unafanya ukubalike na wengine na kuonekana mtu mzuri. Ule upande wako (more…)

2783; Haina matumizi.

By | August 14, 2022

2783; Haina matumizi. Kitu chochote kikishakosa matumizi, kinaanza kuharibika. Angalia majengo mazuri ambayo hayatumiki, huwa yanaanza kuharibika vibaya. Kadhalika kwenye vifaa mbalimbali tunavyotumia, kama kifaa hakitumiki kinaanza kuharibika. Tunapata funzo kubwa sana hapa kuhusu maisha ya mafanikio. Kama kuna kitu tunakosa au kushindwa kutumia, inasababishwa na sisi kukosa matumizi na (more…)

#SheriaYaLeo (287/366); Kubadili matokeo badili mtazamo wako.

By | August 14, 2022

#SheriaYaLeo (287/366); Kubadili matokeo badili mtazamo wako. Jinsi ambavyo unaona na kuchukulia vitu, siyo jinsi ambavyo vilivyo, bali ni jinsi wewe mwenyewe ulivyo, mtazamo ambao unao. Hiyo ndiyo maana unaweza kuwakuta watu wawili wako kwenye eneo moja, wakifanya kitu kinachofanana, mmoja akawa amefanikiwa na mwenye furaha huku mwingine akiwa ameshindwa (more…)

2782; Anaringa.

By | August 13, 2022

2782; Anaringa. Kwenye maisha, watu wanataka uwe vile wanavyotaka wao, ukiwa tofauti, watakupa kila aina ya shutuma. Lakini sasa, kwenye hii safari ya mafanikio, huwezi kuwa vile ambavyo kila mtu anataka uwe. Badala yake unapaswa kuwa na misingi ambayo unaisimamia wakati wote, hata kama haiwafurahishi wengine. Maana kama kuwafurahisha wengine (more…)

#SheriaYaLeo (286/366); Ona vitu kama vilivyo na siyo kama hisia zako zinavyokusukuma.

By | August 13, 2022

#SheriaYaLeo (286/366); Ona vitu kama vilivyo na siyo kama hisia zako zinavyokusukuma. Unapaswa kujua pale unaposukumwa na hisia katika maamuzi na kujidhibiti ili usilete madhara. Hiyo ni kwa sababu hisia huwa zinatuzuia tusione vitu kama vilivyo. Hofu inakufanya umkuze zaidi adui na kukimbilia kujihami haraka. Hasira zinakufanya ukimbilie kuchukua hatua (more…)

2781; Watu na matatizo yao.

By | August 12, 2022

2781; Watu na matatizo yao. Mtu mmoja alisikia mbwa wa jirani yake akilia kwa uchungu na kwa muda mrefu. Alishindwa kuvumilia na kuamua aende kuangalia nini kinaendelea. Alipofika kwa jirani yake, alimkuta amekaa kwenye bustani yake akisoma gazeti, huku pembeni yake mbwa wake akiwa amekalia msumari ambao unamuumiza ndiyo maana (more…)