#SheriaYaLeo (270/366); Achana na yaliyopita.

By | July 28, 2022

#SheriaYaLeo (270/366); Achana na yaliyopita. Kinachowakwamisha watu wengi ni kushindwa kuukabili uhalisia na kuona vitu jinsi vilivyo. Kadiri tunavyokua kiumri, ndivyo tunavyozidi kufanya vitu kwa mazoea. Tunatawaliwa zaidi na tabia. Kitu ambacho kilitupa matokeo mazuri huko nyuma kinakuwa ndiyo msingi wetu, tunarudia hicho hicho kila wakati. Marudio yanachukua sehemu ya (more…)

#SheriaYaLeo (269/366); Epuka kukaa kwenye kona.

By | July 27, 2022

#SheriaYaLeo (269/366); Epuka kukaa kwenye kona. Kwenye michezo mbalimbali, kukimbilia kukaa kwenye kona ni kujipeleka kwenye kushindwa na hata kufa kabisa. Hali hiyo pia ipo kwenye maeneo mengine ya maisha yetu. Pale unapokabiliana na jambo lolote lile, kukimbilia kwenye kona ni kujipeleka kwenye kushindwa. Kwenye kona kunaweza kuonekana kama ni (more…)

2764; Wimbo unaoupenda sana.

By | July 26, 2022

2764; Wimbo unaoupenda sana. Rafiki, hebu fikiria wimbo mmoja ambao unaupenda sana. Tena hebu uimbe kidogo wimbo huo. Unaujua kwa hakika mashairi yake yote. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwa baadhi ya matangazo ya biashara. Kuna baadhi ya matangazo ambayo umekuwa unayapenda sana na unayajua maelezo yake yote. Sasa nina swali (more…)

#SheriaYaLeo (268/366); Rudi nyuma kupata mtazamo mpya.

By | July 26, 2022

#SheriaYaLeo (268/366); Rudi nyuma kupata mtazamo mpya. Tatizo kubwa linalotukabili kwenye mikakati na maisha kwa ujumla ni kwamba kila mmoja wetu ni wa kipekee kwa haiba yake. Tunatofautiana sana na hata hali tunazopitia pia zinatofautiana. Changamoto kubwa ni kwamba huwa hatuwezi kujua tofauti walizonazo wengine. Mbaya zaidi ni tunashindwa hata (more…)

2763; Hakuna anayekuangusha.

By | July 25, 2022

2763; Hakuna anayekuangusha. Ni rahisi sana kulaumu wengine kwamba wanakuangusha au kukukwamisha. Lakini nataka nikuhakikishie kitu kimoja, hakuna yeyote anayekukwamisha au kukuangusha. Bali hayo yote unajifanyia wewe mwenyewe. Kama hujapata au kufika kule unakotaka kufika, hakuna mwingine yeyote ambaye anakuzuia isipokuwa wewe mwenyewe. Siyo wazazi, mwenza, serikali, uchumi au mazingira (more…)

#SheriaYaLeo (267/366); Tumia machale yako.

By | July 25, 2022

#SheriaYaLeo (267/366); Tumia machale yako. Mara nyingi sana utahitajika kufanya maamuzi ya haraka kabla hujawa na taarifa za kutosha. Ni kwenye hali za aina hiyo ndiyo unapaswa kuyatumia vizuri machale yako. Kutumia hisia za ndani yako katika kufanya maamuzi sahihi. Kabla ya kutumia machale yako, lazima kwanza uyaendeleze. Na njia (more…)

2762; Kujiandaa kuishi.

By | July 24, 2022

2762; Kujiandaa kuishi. Watu wengi huwa wanayamaliza maisha yao hapa duniani kabla hata hawajaanza kuishi. Kila wakati wanakuwa wanajiandaa kuanza kuishi. Hatimaye mauti yanawafika kabla hata hawajawa tayari kuishi. Ukifuatilia maisha ya wengi, na huenda hata ya kwako binafsi, hilo lipo dhahiri kabisa. Wakati mtu akiwa mtoto, anaenda shule kujiandaa (more…)

#SheriaYaLeo (266/366); Wavuruge wasiweze kukusoma.

By | July 24, 2022

#SheriaYaLeo (266/366); Wavuruge wasiweze kukusoma. Nguvu ya maadui zako ipo kwenye uwezo wao wa kukusoma na kujua nia na mipango uliyonayo. Lengo la mikakati yako linapaswa kuwa ni kuwazuia maadui wasiweze kukusoma. Utaweza kukamilisha hilo kwa kuwavuruga maadui zako, kuwafanya wahangaike na mambo yasiyokuwa sahihi. Unachofanya ni kuigiza unafanya kitu (more…)

2761; Unajitofautishaje na wengine?

By | July 23, 2022

2761; Unajitofautishaje na wengine? Unajua ninj rafiki yangu, Neno siri za mafanikio limewanufaisha sana wengi. Kuna wengi ambao wameweza kuingiza kipato kikubwa kwa kuwaambia wengine kwamba wanazo siri za mafanikio. Sasa kwa sababu jamii kwa ujumla haiyaelewi mafanikio, hunasa kwenye huo mtego. Kwa kuamini kutakuwa na siri za mafanikio ndiyo (more…)