Tag Archives: MBINU ZA MAFANIKIO

Kama Unataka Kupata Unachotaka Fanya Hivi…

By | January 25, 2015

Kama kuna kitu ambacho unakitaka kweli, na upo tayari kufanya chochote ili kukipata, ulimwengu mzima utakusaidia kupata kitu hiko. Hivyo kupata chochote unachotaka, hakikisha unakitaka kweli na unaamini kwamba unaweza kukipata. SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako. Kama (more…)

Bado Huzioni Fursa Zinazokuzunguka? Jiulize Maswali Haya Matatu.

By | January 24, 2015

Maswali matatu muhimu ya kukusaidia kugundua fursa zinazokuzunguka. i. Ni kitu gani ambacho kinakupa msukumo mkubwa. Katika vitu vyote unavyofanya au unavyofuatilia kuna kimoja ambacho kinakupa hamasa kubwa. Ni kipi hiko? ii. Je una vipaji gani? Ni vitu gani ambavyo umekuwa unapendelea kufanya tangu ukiwa mdogo. Ni kitu gani ukikifanya (more…)

Jibu Swali Hili Na Fanyia Kazi Jibu Lako, Maisha Yako Yatabadilika Sana.

By | January 23, 2015

Hili ni swali la msingi sana ambalo kama ukiweza kujiuliza na ukajijibu kwa uaminifu basi maisha yako yatabadilika na kuwa bora sana. Msisitizo ni jibu kwa uaminifu na fanyia kazi majibu yako. Swali lenyewe ni hili; KAMA UNGEWEZA KUWA BORA SANA DUNIANI KWENYE KITU KIMOJA TU, UNGECHAGUA KITU GANI? Andika (more…)

Kama Sio Wewe Nani? Kama Sio Sasa Lini?

By | January 21, 2015

Kama sio wewe utakayebadili maisha yako unafikiri ni nani atakayefanya hivyo? Kama sio sasa utabadili maisha yako umafikiri ni lini utafanya hivyo? Usijidanganye kwamba kuna mtu atakayekuja kukutoa hapo ulipo, ni lazima nia hii itoke ndani yako. Usijidanganye kwamba utabadili maisha yako kesho, kesho haijawahi kufika. NI WEWE, NI SASA, (more…)

Kuna Makundi Matatu Ya Watu; Je Wewe Upo Kwenye Kundi Lipi Kati Ya Haya? Fungua Kujua.

By | January 20, 2015

Duniani kuna makundi matatu ya watu. Na watu wote duniani tunaingia kwenye moja wapo ya makundi haya. Kundi ulilopo linaweza kuw akiashiria kama utafikia mafanikio au la. Na habari njema ni kwamba unaweza kubadilisha na kwenda kwenye kundi jingine ambalo litakufikisha kwenye mafanikio unayotaka. SOMA; Wajasiriamali Wenye Mafanikio Hufanya Mambo (more…)

Jambo Muhimu La Kufanya Leo Jumapili Usiku.

By | January 18, 2015

Jumapili ndio inaisha na kesho tunaanza wiki nyingine mpya. Kuna mambo mengi unaweza kufanya siku ya leo kabla haijaisha. Ila kuna jambo moja muhimu sana ambalo kama utashindwa kulifanya unaweza kupoteza wiki yako nzima. Jambo muhimu la wewe kufanya leo ni kuipangilia wiki yako. Jua ni mambo gani ambayo utahitaji (more…)

Dunia Haitasimama….

By | January 11, 2015

Dunia haitasimama ikusubiri wewe umaliza kusoma.. Dunia haitasimama ikusubiri wewe umalize kulea… Dunia haitasimama ikusubiri wewe uongezwe mshahara… Dunia haitasimama ikusubiri wewe upate mtaji… Dunia haitasimama ikusubiri wewe mambo yako yawe mazuri. Kumbuka wakati wewe unasubiri dunia inaendelea kusonga mbele, wenzako wanaendelea kuboresha maisha yao na kufikia mafanikio makubwa. Kama (more…)

Wewe Ni Muumbaji… (Vitu Vitamu Muhimu Vya Kuzingatia)

By | January 10, 2015

Ndio wewe ni muumbaji… Mawazo yako yanaumba… Maneno yako yanaumba… Matendo yako yanaumba… Kuwa makini na vitu hivi vitatu ambavyo vina uhusiano wa karibu sana. Vitu hivi vitatu ndio vimekufikisha hapo ulipo, iwe unapafurahia au la. Vitu hivyo vitatu ndio vitakutoa hapo ulipo na kukufikisha unakotana. Hakuna wa kukuzuia bali (more…)

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutumia Akili Yako Vizuri Na Ikakuletea Kila Unachotaka

By | January 9, 2015

Kama UTATUMIA AKILI YAKO VIZURI ni vigumu sana kushindwa kuishi maisha unayotaka. Tambua kikubwa ni kuweza KUTUMIA AKILI YAKO VIZURI. Na ni vigumu sana kuitumia akili yako hasa kwenye ulimwengu wa sasa ambao kila mtu anataka uangalie anafanya nini. Huyu anakutumia video ya vichekesho, yule anakutumia picha yaaani ni fujo (more…)