2393; Sifuri, Moja, Kumi, Mia na kuendelea…

By | July 20, 2021

2393; Sifuri, Moja, Kumi, Mia na kuendelea… Safari ya maili elfu moja huwa inaanza na hatua moja. Hii ni kauli maarufu sana kwenye mafunzo ya hamasa na mafanikio. Lakini imekuwa kauli rahisu kusema kuliko kuweka kwenye vitendo. Watu wengi hawana subira wanapoianza safari ya mafanikio. Wakiwaangalia waliofanikiwa, wanataka wawe kama (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MCHANGO WAKO KWENYE CHANGAMOTO…

By | July 20, 2021

Hakuna changamoto unayopitia ambapo wewe mwenyewe huna mchango katika kuisababisha au kuichochea. Kwa kila changamoto au magumu unayopitia, wewe una mchango. Hata kama unaona wengine ndiyo wanaohusika, kuna namna na wewe pia unahusika. Na uhusika wako mkuu huwa ni kukosa umakini kwenye kile unachofanya. Unapoweka umakini wako wote kwenye jambo, (more…)

2392; Unavyojitengenezea Maumivu…

By | July 19, 2021

2392; Unavyojitengenezea Maumivu… Sehemu kubwa ya maumivu unayopitia kwenye maisha yako, huwa unayatengeneza wewe mwenyewe. Unafanya hivyo bila ya kujua. Hapa ni baadhi ya mambo ambayo umezoea kufanya ambayo yanakuweka kwenye hatari ya kupata maumivu. Kuwa na matarajio makubwa kwenye vitu usivyokuwa na udhibiti navyo. Kulazimisha matokeo ya aina fulani. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WATU WENYE CHUKI…

By | July 19, 2021

Ni watu ambao hupaswi kuwaruhusu wakusumbue kwa namna yoyote ile. Kwa sababu mtu akiwa na chuki na wewe, tayari ana chuki na yeye binafsi. Hakuna namna unaweza kumlazimisha anayekuchukia akupende, maana yeye mwenyewe hajipendi. Watu wanaojipenda hawana muda wa kuwa na chuki kwa wengine. Na watu wenye chuki, hawana manufaa (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kwa usomaji wa vitabu.

By | July 18, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kwa usomaji wa vitabu. Kitu kimoja ninachoamini sana ni kwenye zama tunazoishi sasa unaweza kulipwa kwa chochote unachofanya. Miezi michache iliyopita nilinunua simu mpya, wakati naiweka kwenye chaji ukaja ujumbe, ingiza kipato kwa kuchaji simu yako. Mwanzo nilishangaa, lakini baadaye nikajiambia kipi cha kushangaa kutoka (more…)

2391; Kutaka kupenda na kila mtu…

By | July 18, 2021

2391; Kutaka kupenda na kila mtu… Hakuna maisha magumu hapa duniani kama kutaka kila mtu akupende. Ni maisha magumu kwa sababu hata ujaribu kwa namna gani, huwezi kufanikiwa. Haijalishi unafanya nini, kuna watu wanachagua tu kukuchukia. Na hata kama unachofanya ni kizuri na chenye manufaa, bado wapo ambao hawatapenda namna (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAZURI NA MABAYA…

By | July 18, 2021

Yote huwa yanatokea, na siyo kwa kupenda au kutokupenda kwako, bali ni sehemu ya maisha. Lakini unapoweka mipango yako, huwa unaangalia mzuri yanayoweza kutokea na kuyasahau mabaya. Kinachotokea ni kuumizwa sana pale mabaya yanapotokea. Hupaswi kuruhusu kitu chochote kitokee kwa mshangazo kwako, yaani kitokee bila ya kutegemea kabisa. Tafakari matokeo (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia mawazo yako.

By | July 17, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia mawazo yako. Akili unayo na unaweza kuitumia kuzalisha mawazo mbalimbali. Zipo njia mbalimbali za kuingiza fedha kupitia mawazo yako. Hapa kuna mawazo kumi ya kufanya hivyo. Kuja na mawazo ya kuongeza kipato chako na kuyafanyia kazi. Kuja na mawazo ya kupunguza gharama zako ili (more…)

2390; Kipi Kibaya Zaidi Kinaweza Kutokea?

By | July 17, 2021

2390; Kipi Kibaya Zaidi Kinaweza Kutokea? Unapoweka mipango yako, huwa unaangalia mambo yakienda vizuri tu. Kama ni biashara, unangalia upande wa faida tu. Kama ni tabia unajijengea, unaangalia manufaa yake tu. Tunapenda sana mambo yaende vizuri, lakini hilo liko nje ya uwezo wetu. Kitu pekee tunachoweza kudhibiti ni juhudi unazoweka (more…)