Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2477; Hakuna nguvu za ziada.

By | October 12, 2021

2477; Hakuna nguvu za ziada. Moja ya kanuni muhimu niliyojifunza kwenye fizikia na ambayo inaendana sana na maisha ya mafanikio ni kuhusu nguvu. Kanuni ya nguvu kwenye fizikia inasema nguvu haiwezi kuzalishwa wala kuharibiwa, bali inaweza kubadilishwa kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine. Kwa mfano gari iliyo kwenye mwendo ina nguvu (more…)

2475; Angalia Muda.

By | October 10, 2021

2475; Angalia Muda. Tumekuwa tunaona jinsi watu wanalaghaiwa na kutapeliwa kwenye zama hizi. Kwa kuitwa kwenye fursa mbalimbali ambazo zinawahamasisha kweli kweli na wanaziamini, lakini baadaye wanakuja kugundua wametapeliwa. Nilishakushirikisha njia moja ya kupima kama fursa ni ya kweli au utapeli, ambayo ni kujiuliza kazi unayopaswa kuweka na thamani unayotoa. (more…)

2474; Fanya vichache kwa ubora.

By | October 9, 2021

2474; Fanya vichache kwa ubora. Moja ya sababu za wengi kushindwa kufanya wanayofanya kwa ubora ni kuhangaika na mambo mengi. Watu wanakazana kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja, kitu ambacho kinaathiri ufanisi wao. Unapofanya mambo mengi kwa wakati mmoja, unatawanya sana nguvu na umakini wako na kuishia kupata matokeo ya (more…)

2473; Uimara ndani ya udhaifu.

By | October 8, 2021

2473; Uimara ndani ya udhaifu. Tumeshajifunza sana jinsi ambavyo hakuna aliyekamilika. Kwamba kila mmoja wetu ana madhaifu yake. Wengi huwa wanalipokea hilo kwa mtazamo wa kuyaondoa madhaifu yao na ili yasiwe kikwazo. Kinachotokea ni madhaifu yao yanazidi kuwa imara huku uimara wao ukiwa dhaifu. Yaani unapoweka nguvu kuyaondoa madhaifu yako, (more…)

2472; Muda na Umakini…

By | October 7, 2021

2472; Muda na Umakini… Watu wengi wamekuwa wanasingizia muda kama kikwazo kwao kufanya yale yaliyo muhimu. Wanasema hawana muda wa kufanya mambo hayo. Mimi nimekuwa nalikataa hilo, nikisema kila mtu ana muda sawa. Hivyo ambao wanasema hawana muda, wanatafuta tu visingizio na wamekosa vipaumbele kwenye maisha yao. Nimekuwa nawakatalia kabisa (more…)

2471; Watu wanaamini msimamo.

By | October 6, 2021

2471; Watu wanaamini msimamo. Kuahidi kila mtu anaweza na wengi wanafanya hivyo. Kujaribu kufanya kila mtu anaweza na wengi huanza na kuacha. Wanachohitaji watu ili wakuamini ni msimamo wako kwenye kile ulichoahidi. Kama una biashara ambayo umeahidi kitu fulani, lakini mwanzoni huna wateja wengi, ni rahisi kutokutimiza ahadi hiyo, ukijiambia (more…)

2470; Zima, Washa.

By | October 5, 2021

2470; Zima, Washa. Jana dunia ilikubwa na taharuku baada ya mitandao mikubwa ya kijamii ambayo imeshakuwa tegemeo kwa wengi kutokupatikana hewani. Nimekuwa siyo mtumiaji wa mitandao ya kijamii, ila natumia mtandao wa WhatsApp kwa mawasiliano na huduma mbalimbali ninazotoa. Na hali ya jana ilinikuta nikiwa katikati ya mawasiliano na mtu, (more…)

2469; Kutokumuumiza Yeyote.

By | October 4, 2021

2469; Kutokumuumiza Yeyote. Kuna vitu ambavyo huwa tunahangaika navyo kwenye maisha, ambavyo tunajisumbua tu lakini haviwezi kuwa vile tunavyotaka. Moja ya vitu hivyo ni kutaka kufanya maamuzi ambayo hayatamuumiza mtu yeyote yule. Hizo ni ndoto ambazo ukiendelea kuziota hutakuja kufanya maamuzi makubwa kwenye maisha yako. Kwa sababu maamuzi yoyote yale (more…)

2468; Kutokujibu pia ni jibu.

By | October 3, 2021

2468; Kutokujibu pia ni jibu. Kwenye maisha huwa tunakutana na watu wa aina mbalimbali. Wapo ambao huwa wanasema au kufanya mambo ambayo yanatukwaza na tunasukumwa kuwajibu ili wajifunze. Tunaona tusipowajibu sawasawa na walichofanya au kusema, watazoea vibaya au watajiona washindi. Lakini wakati mwingine kutokujibu ndiyo jibu lenye nguvu kubwa mno. (more…)