Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2431; Kuchinja kuku anayetaga…

By | August 27, 2021

2431; Kuchinja kuku anayetaga… Ili upate mayai zaidi ni jambo la ajabu lakini ambalo limekuwa linafanywa na wengi. Wengi huanza na kitu chini kabisa, wanaweka juhudi kubwa na hizo kupelekea kitu hicho kuwapa matokeo mazuri. Wakishapata matokeo mazuri wanajisahau na kujikuta wanaharibu kabisa kile kilichokuwa kinawapa matokeo hayo. Kinachotokea ni (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAVYOJIANDAA KUUMIA…

By | August 27, 2021

Kutaka mambo yaende kama unavyotaka wewe na kuona hayawezi kwenda tofauti na hivyo ni kujiandaa kuumia. Kwa sababu dunia haipeleki mambo yake kwa kuangalia matakwa ya watu, bali inatumia kanuni zake yenyewe. Unachoweza kudhibiti wewe ni juhudi unazoweka na mchakato unaofanyia kazi. Kwa upande wa matakeo, yatakuja yenyewe kwa namna (more…)

2430; Unaona kile unachotaka kuona…

By | August 26, 2021

2430; Unaona kile unachotaka kuona… Sisi binadamu kwa kujidanganya huwa tupo vizuri sana. Ila huwa hatujui kama tunajidanganya, tunakuwa na ukakika tumesimama kwenye ukweli. Ila ni mpaka pale uzio ulio kati ya ukweli na uongo unapoanguka ndiyo tunaona wazi tulikuwa tunajidanganya. Huwa tunaona kile tunachotaka kuona na kukusanya ushahidi unaoendana (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KILA MTEJA NI WA KWANZA KWAKO…

By | August 26, 2021

Kila mteja unayemhudimia, mchukulie ndiye mteja wa kwanza kwako na wa kipekee kabisa. Kwa sababu hivyo ndivyo mteja anavyojichukulia. Wewe unaweza kuwa umeshawahudumia wateja wengi na umechoka, ila mteja mwingine anapokuja hajui wala kujali yote hayo. Ukimpa huduma mbovu hataangalia umehudumia wateja wangapi vizuri, yeye atakachojua ni kimoja, hujamhudumia vizuri (more…)

2429; Wa mwisho kwako, wa kwanza kwake…

By | August 25, 2021

2429; Wa mwisho kwako, wa kwanza kwake… Kitu kimoja kikubwa ambacho najifunza kwenye taaluma ya udaktari ni mitazamo tofauti ambayo daktari na mgonjwa wanakuwa nayo. Kama daktari unaweza kuwa kwenye zamu ya kuona wagonjwa na umekaribia mwisho kabisa wa zamu yako, umechoka na anakuja mgonjwa wa mwisho. Wewe daktari unaweza (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UPANDE WA PILI WA MAFANIKIO…

By | August 25, 2021

Tunapoyatafuta mafanikio, huwa tunaangalia upande mmoja pekee, ambao ni upande mzuri wa kupata kile tunachotaka. Lakini mafanikio huwa yana upande wa pili, ambao ni kuwapoteza baadhi ya watu wako wa karibu. Kuna watu walikuwa na wewe kabla hujafanikiwa, lakini baada ya kufanikiwa wanageuka kuwa maadui. Unapaswa kujua hili, kwamba kadiri (more…)

2428; Mafanikio yako ni hatari kwa wengine…

By | August 24, 2021

2428; Mafanikio yako ni hatari kwa wengine… Kabla hujafanikiwa, watu wanakuchukulia poa. Kwanza wanajua hutaweza kufanikiwa sana, hivyo huwi hatari kwake. Unapofanikiwa kwa viwango vya juu na kuwapita wao kimafanikio, ghafla wanabadilika na kuanza kuwa kikwazo kwako. Wanafanya hivyo kwa sababu wanakuona wewe ni hatari kwao, na hatari hiyo inatokana (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HASIRA NI MATATIZO BINAFSI…

By | August 24, 2021

Kinachokufanya ukasirike siyo kile alichofanya mtu au kilichotokea, bali ni matatizo yako binafsi. Unakasirika kwa sababu kuna namna unataka vitu viwe na havijawa, hivyo kupelekea kujiumiza zaidi. Kuondokana na hasira, anzia ndani yako mweyewe, acha kutaka vitu viwe kama unavyotaka wewe na vipokee kama vinavyokuja kwako. Pia usikubali tu kuchukua (more…)

2427; Makasiriko…

By | August 23, 2021

2427; Makasiriko… Katika hali yoyote ile, aliyekasirika ndiye mwenye matatizo. Yaani kama kuna mtu amekukasirisha, tatizo siyo mtu huyo, bali tatizo ni wewe uliyekasirika. Kwa maana nyingine, ukikasirika maana yake una matatizo. Na wewe angalia wazi tu ni wakati gani unakasirika. Mara nyingi ni moja kati ya nyakati hizi tatu. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NI KUKOSA UMAKINI…

By | August 23, 2021

Kama umewahi kudanganywa, kuibiwa au kutapeliwa, ni kwa sababu kuna umakini ambao uliukosa. Watu huwa wanadanganya kwa maneno, lakini vitendo vyao huwa wazo kabisa. Ukiwa makini, lazima utaona tofauti kati ya unachosikia na unachoona. Mtu anakuambia kuna fursa yenye manufaa mahali, wakati ukimuangalii hafananii na mwenye kujua fursa ya aina (more…)