Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2421; Siyo kila ushauri unakufaa…

By | August 17, 2021

2421; Siyo kila ushauri unakufaa… Nianze kwa kusema kila kitu kwenye biashara kinawezekana. Na kwa biashara yoyote unayofanya, watu watakuja kwako na ushauri wa kila aina. Na kila ushauri unaopewa utaonekana ni sahihi kabisa na wenye tija kwa biashara. Lakini siyo kila ushauri unakufaa wewe na biashara yako. Unapoingia kwenye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UPWEKE WA SAFARI YA MAFANIKIO…

By | August 17, 2021

Unapoamua kufanya makubwa na ya tofauti, utajiona kama uko peke yako. Dunia itaonekana kutokujali kabisa na kusubiri uanguke ili ikucheke. Lakini manbo hayako hivyo, kuna wengi sana ambao wako nyuma yako, japo wapo kimya kimya. Watu hao wananufaika na kile unachofanya na pia wanapata matumaini ya wao pia kufanya makubwa. (more…)

2420; Kuna watu wananufaika hata kama

By | August 16, 2021

2420; Kuna watu wananufaika hata kama hawakuambii… Tatizo kubwa kwenye maisha, hasa kwenye safari ya mafanikio ni upweke utakaokutana nao. Mara kwa mara utajikuta kwenye hali ya upweke, ukijiona uko mwenyewe kwenye mapambano unayoendesha. Katika nyakati hizo ndiyo mawazo ya kukata tamaa hukujia, yakikushawishi kwamba hakuna anayejali. Lakini mimi nataka (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUWA MAKINI NA TAARIFA UNAZOPOKEA…

By | August 16, 2021

Uongo na uzushi huwa unasambaa kwa kasi kuliko ukweli. Hiyo ni kwa sababu uongo uba mbwembwe nyingi na unagusa hisia hivyo kusambaa kama moto. Ukweli hauna mbwembwe wala hauchochei hisia. Hivyo kuwa makini sana na taarifa unazopokea, kama huwezi kuzithibitisha kama ni kweli au la, angalia kasi ambayo taarifa hizo (more…)

2419; Kwa nini ukweli ni mgumu kufikiwa…

By | August 15, 2021

2419; Kwa nini ukweli ni mgumu kufikiwa… Ni vigumu kuufikia ukweli kwa sababu huwa haubembelezi. Ukweli hauangalii mtu anataka kusikia au kuona nini, unabaki kuwa ukweli. Ukweli hauna mbwe mbwe wala kelele, unasimama kwenye eneo sahihi. Sisi binadamu tunapenda mbwembwe nyingi, tunapenda vitu vinavyotusisimua. Hivyo tunahangaika na yale yasiyo kweli (more…)

#TAFAKARI YA LEO; TATIZO NI KIPAUMBELE…

By | August 15, 2021

Kama kuna kitu unafanya na hufanikiwi, ila unaona wengine wanafanya kitu hicho hicho na wanafanikiwa, mnatofautiana kwenye vipaumbele. Wale wanaofanikiwa kwenye kitu hicho wanakuwa wamekipa kipaumbele cha kwanza, kwa sababu wameyafanya maisha yao kukitegemea kitu hicho. Wewe ambaye hufanikiwi kwenye kitu hicho hujakipa kipaumbele cha kwanza, kwa kuwa maisha yako (more…)

2418; Kwa sababu maisha yako yote yanategemea

By | August 14, 2021

2418; Kwa sababu maisha yako yote yanategemea hapo… Huwa tunakipa kitu uzito kulingana na namna kinavyoathiri maisha yetu moja kwa moja. Kama maisha yanategemea zaidi kitu fulani, basi tunakipa kitu hicho kipaumbele cha kwanza. Ndiyo maana kwenye dharura, watu huwa tayari kufanya chochote ili tu kuokoa uhai wao. Hivyo basi, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUKOSEA NI MWANZO WA KUJIFUNZA…

By | August 14, 2021

Huwa hatupendi kukosea kwa sababu tunachukulia kukosea ni kutokujua na kushindwa. Lakini kukosea ndiyo mwanzo mzuri wa kujifunza. Unapokosea unakuwa na fursa ya kujifunza kipi kinafanya kazi na kipi hakifanyi kisha kuchukua hatua zilizo sahihi. Usiache kufanya maamuzi au kuchukua hatua kwa sababu unaogopa kukosea, kukosea ndiyo mwanzo wa kujifunza, (more…)

2417; Maamuzi ya kufa na kupona…

By | August 13, 2021

2417; Maamuzi ya kufa na kupona… Kuna maamuzi machache sana ambayo ukiyafanya kwenye biashara ni ya kufa na kupona. Kwa maana kwamba kuna hatari ya biashara kufa kabisa. Lakini maamuzi hayo ni machache mno. Maamuzi mengine mengi, pamoja na ugumu na umuhimu wake, yanaweza kurekebishika tu. Funzo ni nini hapa? (more…)

#TAFAKARI YA LEO; TATIZO UNAHANGAIKA NA VITU RAHISI…

By | August 13, 2021

Ukisikia tu kuna kitu rahisi na kinakipa sana, mbio unakimbilia kukifanya. Kwa kuwa wengi wanapenda urahisi, mnajikuta wengi mpo kwenye kitu hicho, ushindani unakuwa mkali na wengi hamnufaiki. Mnasikilizia tena wapi ni rahisi, na kupakimbilia. Miaka inaenda unashangaa hupigi hatua kubwa. Unajiona labda una bahati mbaya, lakini tatizo ni moja, (more…)