Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2416; Kuanzia chini ni kazi kubwa…

By | August 12, 2021

2416; Kuanzia chini ni kazi kubwa… Mimi siyo mfuatiliaji wa michezo kabisa, lakini kama ambavyo nimekuwa nasema, kuna mambo utayasikia tu hata kama siyo mfuatiliaji wa habari. Siku za hivi karibuni kumekuwa na mivutano kwenye timu kubwa za mpira Tanzania, hasa timu ya Simba ambapo kuna migogoro mbalimbali ya ndani. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; CHANGAMOTO YA MOTISHA…

By | August 12, 2021

Unaweza kutoa motisha kwa nia njema kabisa, ili kuwasukuma watu wafanye kile unachotaka wafanye. Maana binadamu kwa asili ni wavivu na wazembe, bila motosha ni vigumu sana kufanya kitu. Lakini pia binadamu ni wajanja, wanaweza kuuchezea mfumo wowote ule ili waweze kujinufaisha zaidi. Hivyo kama unatoa zawadi, wanatafuta njia ya (more…)

2415; Zawadi na Adhabu…

By | August 11, 2021

2415; Zawadi na Adhabu… Kituo kimoja cha kulelea watoto (day care) kiliona baadhi ya wazazi wamekuwa na tabia ya kuchelewa kuwachukua watoto wao. Kituo hicho kikaamua kuweka adhabu ya faini kwa kila mzazi anayechelewa kumchukua mtoto wake. Lengo la faini hiyo ilikuwa ni kuondoa hali ya wazazi kuchelewa. Matokeo yakawa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KINACHOKUZUIA USIFAKIWE…

By | August 11, 2021

Ni ujuaji mwingi, kudhani unajua kila kitu na pale unaposhindwa basi unajipa kila aina ya visingizio. Hata pale wengine wanapokuwa wamefanikiwa kwenye kile ulichoshindwa bado hukubali kujifunza kwao, badala yake unawajibia kwa nini wao wamefanikiwa na wewe umeshibdwa. Usiendekeze tabia hiyo ya walioshindwa, kuwa mnyenyekevu na jifunze kwa wale waliopiga (more…)

2414; Ukishindwa, usiwajibie wengine…

By | August 10, 2021

2414; Ukishindwa, usiwajibie wengine… Nimekuwa nasema kama kuna kitu unatumia kama sababu ya kushindwa kupata unachotaka, lakini kuna mwingine ameweza kupata licha ya kuwa na hiyo wewe unaita sababu basi siyo sababu kweli, ni kisingizio tu. Moja ya dalili za kushindwa bila kukubali ni kuwa tayari kuwajibia wale walioweza, kwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAISHA HAYASIMAMI…

By | August 10, 2021

Maisha huwa hayasimami, mara zote yanaenda mbele. Na wewe pia hupaswi kusimama, mara zote nenda mbele. Iwe utaruka, kukimbia, kutembea au kutambaa, wewe songa mbele. Hiyo ndiyo njia pekee ya kujisogeza karibu na kile unachotaka. Pambana usonge mbele, kila siku jifunze na fanya kitu kipya ambacho hujawahi kufanya huko nyuma. (more…)

2413; Ubaya ni kusimama…

By | August 9, 2021

2413; Ubaya ni kusimama… Kitu pekee unachohitaji kwenye maisha ni kuwa kwenye mwendo. Haijalishi unakwenda kwa kasi kiasi gani, muhimu ni kuwa kwenye mwendo. Jambo baya kabisa kwenye maisha ni kusimama. Kwa sababu dunia haisimami, hivyo unaposimama unakuwa umechagua kurudi nyuma. Unapaswa kujikumbusha kwamba chochote cha maana unachotaka kwenye maisha (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UFUJAJI NI KIKWAZO…

By | August 9, 2021

Kutumia hovyo rasilimali ambazo zina uhaba mkubwa ni kikwazo kwako kuweza kupiga hatua na kufanikiwa. Kwa rasilimali hizo muhimu, unahitaji ubahili na ufanisi. Ubahili katika kutumia ili zitoshe na ufanisi katika kutumia ili zilete matokeo makubwa. Rasilimali ulizonazo tayari zinakutosha kupiga hatua kubwa, kama unaona hazitoshi ni kwa sababu huna (more…)

2412; Ubahili na Ufanisi…

By | August 8, 2021

2412; Ubahili na Ufanisi… Rasilimali zote muhimu huwa zina uhaba. Mahitaji huwa ni makubwa kuliko upatikanaji. Na hapo ndipo tofauti kati ya wanaofanikiwa na wanaoshindwa inapozaliwa. Wanaofanikiwa ni wale wanaoweza kutumia vizuri rasilimali muhimu zenye uhaba. Watu hao wanajua siri kubwa mbili ambazo wanazitumia vyema; uhaba na ufanisi. Kwenye uhaba (more…)