Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#TAFAKARI YA LEO; IGA HIKI…

By | August 8, 2021

Hufanani na wengine kwa chochote kile, hivyo mengi unayoiga kwao yanakupoteza kwa sababu hayaendani na wewe. Ila kuna kitu kimoja ambacho ukikiiga kwa wengine kinakuwa na manufaa makubwa sana kwako. Kitu hicho ni nidhamu. Kwa kila unayemuona amepiga hatua kuliko wewe, jua ni nidhamu zipi zimemwezesha kupiga hatua hizo, kisha (more…)

2411; Usiige Matumizi…

By | August 7, 2021

2411; Usiige Matumizi… Hakuna kitu rahisi kuiga kwa watu kama matumizi. Hicho ndiyo tunaona kwa nje na kujilinganisha nao kisha kukimbilia kuiga. Unapaswa kujua kitu chochote unachonunua kinapaswa kutokana na mahitaji yako kweli na siyo kwa sababu umeona wengine wanacho. Wala usinunue kitu kwa sababu unataka wengine wakuone na wewe (more…)

2410; Hupati Muda…

By | August 6, 2021

2410; Hupati Muda… Kama unajiambia ukipata muda utafanya kitu, jua ni njia tu ya kujifanganya. Ukweli unaopaswa kujiambia ni kitu hicho siyo muhimu sana kwako na hivyo hakipaswi kuwa kipaumbele cha kwanza kwako. Maana kitu kinapokuwa muhimu kabisa huwa hatusubiri mpaka tupate muda, badala yake tunatenga muda. Hivyo acha kujidanganya, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WABOBEZI WA KUANZA…

By | August 6, 2021

Watu wengi kwenye maisha huwa ni waanzaji wazuri wa mambo, ila huwa hawaendi mbali. Huwa hawana ung’ang’anizi kwenye kile wanachoanza mpaka wafike mwisho wake na kuona matokeo yake. Badala yake huwa wanakimbilia kuacha pale wanapokutana na ugumu au changamoto. Kama unayataka mafanikio makubwa, ondoka mara moja kwenye kundi hilo. Usiwe (more…)

2409; Mwanzo wa mwisho na mwisho wa mwanzo…

By | August 5, 2021

2409; Mwanzo wa mwisho na mwisho wa mwanzo… Rafiki, Nataka kusema na wewe leo kuhusu kuanza. Huwa kuna kauli ya Kiswahili inayosema mwanzo ni mgumu. Lakini kwenye safari ya mafanikio hakuna kitu rahisi kama kuanza. Najua ulishaanza mambo mengi mno, lakini hukuyafanya kwa muda mrefu. Ni pale ulipokutana na ugumu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; RASILIMALI TAYARI UNAZO…

By | August 5, 2021

Hakuna ambaye hana rasilimali muhimu anazohitaji ili kufanikiwa. Kila siku tunakutana na rasilimali ambazo tukizitumia vizuri tutapata matokeo bora sana. Kila magumu, changamoto na majanga unayokutana nayo ni rasilimali. Kila unayekutana naye ni rasilimali. Na kila unachojifunza ni rasilimali. Usijiambie huna rasilimali, bali jiulize umezitumiaje mpaka sasa hizo ambazo tayari (more…)

2408; Kila kitu ni rasilimali…

By | August 4, 2021

2408; Kila kitu ni rasilimali… Moto mkali unapokuwa unawaka, chochote kitakachowekwa kwenye moto huo hugeuka kuwa nishati ya kuuchochea zaidi. Hata ukimwaga maji kwenye moto ambao ni mkali, unakuwa kama ni mafuta, yanachochea zaidi moto huo. Hivyo ndivyo unapaswa kuyafanya maisha yako kuwa, tumia kila unachopitia au kukutana nacho kama (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MAJARIBU YANAPIMA MSIMAMO…

By | August 4, 2021

Majaribu huwa yanapima msimamo ambao mtu anao kwenye jambo lolote lile. Ambao hawajawahi kupitia majaribu makubwa kwenye kitu, wanaweza kudhani wana msimamo, kumbe siyo. Huwa tunawashangaa watu kwamba wamebadili msimamo wao, kwamba awali walikuwa na msimamo fulani, ila baada ya kupata fursa fulani wakabadilika. Hao hawakuwa na msimamo, ila tu (more…)