Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (286/366); Ona vitu kama vilivyo na siyo kama hisia zako zinavyokusukuma.

By | August 13, 2022

#SheriaYaLeo (286/366); Ona vitu kama vilivyo na siyo kama hisia zako zinavyokusukuma. Unapaswa kujua pale unaposukumwa na hisia katika maamuzi na kujidhibiti ili usilete madhara. Hiyo ni kwa sababu hisia huwa zinatuzuia tusione vitu kama vilivyo. Hofu inakufanya umkuze zaidi adui na kukimbilia kujihami haraka. Hasira zinakufanya ukimbilie kuchukua hatua (more…)

2781; Watu na matatizo yao.

By | August 12, 2022

2781; Watu na matatizo yao. Mtu mmoja alisikia mbwa wa jirani yake akilia kwa uchungu na kwa muda mrefu. Alishindwa kuvumilia na kuamua aende kuangalia nini kinaendelea. Alipofika kwa jirani yake, alimkuta amekaa kwenye bustani yake akisoma gazeti, huku pembeni yake mbwa wake akiwa amekalia msumari ambao unamuumiza ndiyo maana (more…)

#SheriaYaLeo (285/366); Jihadhari na wivu.

By | August 12, 2022

#SheriaYaLeo (285/366); Jihadhari na wivu. Katika hisia zote za binadamu, hakuna ambayo ni mbaya na yenye madhara kama wivu. Hisia kwamba wengine wametuzidi kwenye yale ambayo tunayataka sana kama mali, umaarufu na mamlaka. Huwa tunaona tunastahili kupata kwa wingi kama hao wengine, lakini tatizo linakuja kwamba tunakuwa hatuna namna ya (more…)

#SheriaYaLeo (284/366); Fikiri kwa ajili yako mwenyewe.

By | August 11, 2022

#SheriaYaLeo (284/366); Fikiri kwa ajili yako mwenyewe. Sisi binadamu huwa tunapenda sana vitu ambavyo ni rahisi na tumeshavizoea. Tunayapata mawazo yetu kutoka kwa wazazi, shule na jamii inayotuzunguka. Na mitandao ya kijamii imezidisha sana hali hiyo ya kutegemea fikra za wengine. Hivyo ndivyo tunavyoishia kufikiri kuhusu dunia na maisha kwa (more…)

2779; Kutokutaka kupitwa.

By | August 10, 2022

2779; Kutokutaka kupitwa. Habari, tv, umbeya, udaku, majungu na mitandao ya kijamii ni vitu ambavyo vimekuwa na nguvu kubwa kwa wengi kwa sababu vinatumia msingi mmoja muhimu; hofu ya kupitwa. Kwa Kiingereza wanaita FOMO (Fear Of Missing Out). Hebu fikiria, kila siku kuna habari mpasuko (breaking news). Unadhani zote hizo (more…)

#SheriaYaLeo (283/366); Nguvu ya ushirikiano.

By | August 10, 2022

#SheriaYaLeo (283/366); Nguvu ya ushirikiano. Sisi binadamu huwa tunaathiriwa sana na fikra na hisia za watu ambao tunashirikiana nao. Huwa tunaishia kuwa kama wale ambao tunakaa nao kwa muda mrefu. Wale waliotawaliwa na hisia hasi, wasio na furaha na wenye kisirani huwa wana nguvu kubwa ya kushwishi kwa sababu hisia (more…)

2778; Itafanyika njia kwa ajili yako.

By | August 9, 2022

2778; Itafanyika njia kwa ajili yako. Ukweli mmoja ambao watu wengi wamekuwa hawaelewi kwenye maisha ni huu, kila mtu huwa anapata kile anachokitaka kweli kwenye maisha yake. Yaani kama kuna kitu ambacho unakitaka sana kwenye maisha yako, na hakuna namna unakubali kutokukipata, basi unakipata. Hata pale inapoonekana hakuna njia kabisa, (more…)

#SheriaYaLeo (282/366); Wazimu wa kundi.

By | August 9, 2022

#SheriaYaLeo (282/366); Wazimu wa kundi. Wewe peke yako, ukiwa na wazo au mpango ambao ni wa kijinga, watu watakutahadharisha mara moja na kukurudisha kwenye uhalisia. Lakini hilo linapokuwa kwenye kundi, kinyume chake hutokea. Hata kama wazo au mpango ni wa kijinga kiasi gani, kama umekubalika na kundi, kila mtu anakubaliana (more…)

2777; Maji hufuata mkondo wake.

By | August 8, 2022

2777; Maji hufuata mkondo wake. Hii ni kauli rahisi sana ya Waswahili, lakini iliyobeba ujumbe mzito sana. Ni ujumbe ambao ukiweza kuuelewa utajitenganisha kabisa na mambo yanayokuzuia kufanikiwa. Kwenye kitabu cha The Richest Man In Babylon ipo hadithi ya bwana mmoja ambaye hakuwa makini na matumizi ya fedha zake. Alijikuta (more…)