Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (281/366); Tofauti ya hisia na mantiki.

By | August 8, 2022

#SheriaYaLeo (281/366); Tofauti ya hisia na mantiki. Watu wengi hutumia maneno hisia na mantiki bila kuelewa maana yake halisi. Watu huona wale wasiokubaliana nao kama wanatumia hisia badala ya mantiki. Tunachopaswa kujua ni kwamba sisi binadamu wote ni viumbe wa kihisia. Huwa tunaathiriwa na hisia mbalimbali ambazo zinachochea fikra zinazotufanya (more…)

#SheriaYaLeo (280/366); Ielewe Asili Yako.

By | August 7, 2022

#SheriaYaLeo (280/366); Ielewe Asili Yako. Sisi binadamu tuna mambo mengi. Hatujui mawazo yetu yanatoka wapi. Wala hatujui hisia zetu zinatokea wapi. Lakini tunaweza kuelewa vyanzo vya hayo kama tukiwa na udadisi na kuhoji maswali mengi. Na hayo ndiyo matumaini pekee unayoweza kuwa nayo, kwa sababu ni vigumu kujua pale unapokuwa (more…)

#SheriaYaLeo (279/366); Usiruhusu mafanikio yawe sumu kwako.

By | August 6, 2022

#SheriaYaLeo (279/366); Usiruhusu mafanikio yawe sumu kwako. Sisi binadamu huwa tuna udhaifu ambao upo ndani ya kila mmoja wetu. Udhaifu huo huwa unapelekea tujione na kujichukulia kwa namna ambayo siyo sahihi. Udhaifu huo unatokana na asili yetu ya kupenda kujisifia na kukuza chochote tulichonacho. Huwa tunaona tuna uwezo mkubwa kuliko (more…)

2774; Wanajua usichojua.

By | August 5, 2022

2774; Wanajua usichojua. Watu wote ambao wamefanikiwa zaidi kwenye maisha, kuna vitu ambavyo wanavijua ambavyo wasiofanikiwa hawavijui. Kwa hao waliofanikiwa, wanaweza kuwa wanajua vitu hivyo kwa sababu ndivyo mtazamo wao ulivyo au kwa sababu wamepata nafasi ya kujifunza vitu vya tofauti. Hivi karibuni nimesoma mahojiano ya msanifu majengo mkubwa, Frank (more…)

#SheriaYaLeo (278/366); Chambua, chunguza na hoji.

By | August 5, 2022

#SheriaYaLeo (278/366); Chambua, chunguza na hoji. Ili kujenga uwezo mkubwa wa ndani unaoweza kufanya maamuzi sahihi, unapaswa kutafuta njia ya kutawala hisia zako. Hisia huwa zinatuondoa kwenye uwezo wetu mkubwa wa kufikiri. Hisia hizo zinatuteka na kuathiri mtazamo tunaokuwa nao. Tunapokuwa tumetawaliwa na hisia, hatuvioni vitu kama vilivyo kwa uhalisia (more…)

2773; Usichokitaka.

By | August 4, 2022

2773; Usichokitaka. Kama kuna kitu ambacho hukitaki kwenye maisha yako, dawa yake ni kukipuuza. Hapaswi kupambana na chochote ambacho hukitaki. Kwa sababu kwenye kupambana na kitu, unakipa nguvu zaidi na hivyo kuishia kushindwa. Njia ya uhakika na ya ushindi ni kupuuza kile ambacho hukitaki. Kuchukulia kama vile hakipo na hukihitaji (more…)

#SheriaYaLeo (277/366); Uwezo Mkubwa Wa Ndani.

By | August 4, 2022

#SheriaYaLeo (277/366); Uwezo Mkubwa Wa Ndani. Kila binadamu huwa ana kitu anachokiabudu. Huwa kuna kitu cha juu ambacho mtu anakijeshimu na kukitukuza zaidi. Kwa baadhi ya watu ni ufahari wao wa ndani. Wengine ni familia zao, dini zao au jamii zao. Wanafalsafa wa kale waliamini na kuabudu uwezo mkubwa ulio (more…)

2772; Uzuri wa ukweli.

By | August 3, 2022

2772; Uzuri wa ukweli. Uzuri wa kusema ukweli ni kwamba huhitaji kuweka kumbukumbu yoyote ile kwenye yale unayoongea. Kwa sababu ukweli hubaki hivyo daima, huhitaji kujiuliza mara mbili mbili kabla ya kusema kitu. Unaposema uongo inabidi uwe na kumbukumbu nzuri ili kukumbuka yote ambayo umeshayadanganya kuepuka kusema kitu cha tofauti. (more…)