Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (211/366); Kumshawishi anayetaka kukushawishi.

By | May 30, 2022

#SheriaYaLeo (211/366); Kumshawishi anayetaka kukushawishi. Kuna wakati unajikuta kwenye hali ambapo unahitaji kumshawishi mtu ambaye na yeye pia anataka kukushawishi. Hapo unapaswa kutumia mbinu ya kumwonyesha kitu au tabia ya kutaka kushawishika naye. Yaani unamrahisishia zoezi lake la kukushawishi wewe, kitu ambacho kinakuwa rahisi kwako kumshawishi yeye pia. Unapomnasa mtu (more…)

2706; Kupanga na kufanya.

By | May 29, 2022

2706; Kupanga na kufanya. Kwa ujumla, mchakato mzima wa mafanikio unategemea sana kwenye kupanga na kufanya. Ni kitu rahisi lakini chenye nguvu kubwa sana ya kuamua mtu afanikiwe au ashindwe. Watu wengi huwa wanapanga lakini hawafanyi. Kupanga ni rahisi, kufanya siyo. Hivyo watu wana mipango mingi, lakini hawaitekelezi. Watu wengine (more…)

#SheriaYaLeo (210/366); Tumia lugha ya picha.

By | May 29, 2022

#SheriaYaLeo (210/366); Tumia lugha ya picha. Kuwasiliana na watu kwa njia ya kawaida, ambapo unatumia maneno pekee huwezi kuwa na ushawishi mkubwa. Hiyo ni kwa sababu watu huwa wanayasahau maneno haraka. Lakini unapowasiliana na watu kwa kutumia lugha ya picha, unakuwa na ushawishi mkubwa zaidi. Hiyo ni kwa sababu watu (more…)

2705; Imani na matendo.

By | May 28, 2022

2705; Imani na matendo. Imani na matendo ni vitu vinavyokwenda pamoja. Ni mapacha ambao hawawezi kutenganishwa. Ili uweze kufanya makubwa zaidi kwenye maisha yako, ni vitu viwili unavyohitaji kwa pamoja. Imani bila matendo ni mfu, hakuna chochote kitakachotokea kwa kuamini tu. Lazima mtu uchukue hatua kwenye kile unachoamini. Matendo bila (more…)

#SheriaYaLeo (209/366); Jua wakati sahihi wa kuwa jasiri.

By | May 28, 2022

#SheriaYaLeo (209/366); Jua wakati sahihi wa kuwa jasiri. Hakuna mtu yeyote anayezaliwa akiwa muoga. Woga ni tabia ambayo tunajifunza kwenye maisha ili kujilinda. Woga unatuaminisha kwamba kama hatutafanya yale yanayofanya tuonekane, kama hatutajaribu mapya na makubwa, basi hatuwezi kusumbuliwa na matokeo ya kufanikiwa au kushindwa. Huwa tunaamini kama tukiwa wema (more…)

2704; Huhitaji kuomba ruhusa.

By | May 27, 2022

2704; Huhitaji kuomba ruhusa. Sehemu kubwa ya malezi ambayo tumepitia ni kikwazo kikubwa sana kwenye safari yetu ya mafanikio. Tumejengewa sana nidhamu ya woga kiasi cha kukosa uthubutu wa kufanya yale ambayo tunapaswa kufanya ili tufanikiwe. Na eneo kubwa na lenye madhara makubwa ni kwenye kuomba ruhusa. Tangu tukiwa watoto, (more…)

#SheriaYaLeo (208/366); Jua wakati sahihi wa kupotea.

By | May 27, 2022

#SheriaYaLeo (208/366); Jua wakati sahihi wa kupotea. Ili kuwa na ushawishi mkubwa kwa watu, hupaswi kupatikana wakati wote. Kuna wakati unapaswa kupotea na usipatikane kabisa. Pale watu wanapojua unapatikana muda wote wanakuchukulia poa, maana wanajua upo tu. Lakini pale unapopotea, tena bila ya taarifa ndiyo watu wanashtuka kwa kuwa hawakutegemea (more…)

#SheriaYaLeo (207/366); Cheza na utata.

By | May 26, 2022

#SheriaYaLeo (207/366); Cheza na utata. Kunasa umakini wa watu na kuwafanya wakufuatilie, unapaswa kuonyesha sifa ambazo ni kinyume na mwonekano wako. Unapaswa kutengeneza hali ya utata ambao unafanya watu washindwe kukuelewa. Sisi binadamu huwa hatuwezi kutulia pale ambapo hatujakielewa kitu. Huwa tunakifuatilia mpaka tukijue na kukielewa kwa undani. Pale unapoonyesha (more…)

2701; Bila msimamo umefika hapo, vipi ukiweka msimamo?

By | May 24, 2022

2701; Bila msimamo umefika hapo, vipi ukiweka msimamo? Pamoja na kukosa msimamo mkubwa kwenye yale unayofanya, umeweza kufika hapo ulipo sasa. Umekuwa hufanyi mambo kwa viwango vya juu kabisa mara zote. Kuna wakati unahamasika na kufanya kwa viwango vya juu. Na kuna wakati mazoea yanakuingia na unafanya kwa mazoea. Pamoja (more…)