Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (152/366); Mjue vizuri unayekabiliana naye.

By | April 1, 2022

#SheriaYaLeo (152/366); Mjue vizuri unayekabiliana naye. Uwezo wa kuwajua vizuri watu kwa undani ni hitaji muhimu sana kwenye kupata na kutunza mamlaka. Bila ya uwezo huo unakuwa kipofu anayefanya mambo kwa kubahatisha. Kwa sababu utachagua kukabiliana na watu wasio sahihi au wakiwa sahihi utashindwa kuwajua vizuri. Kabla ya kukabiliana au (more…)

2647; Sheria zipo wazi? Na je zinasimamiwa?

By | March 31, 2022

2647; Sheria zipo wazi? Na je zinasimamiwa? Changamoto nyingi kwenye maisha, kuanzia kwetu binafsi na hata kwa wale tunaoshirikiana nao zinatokana na sababu kubwa mbili. Moja ni kutokuwa na sheria zilizo wazi na kujulikana na kila mmoja. Mbili ni kushindwa kusimamia sheria hizo mara zote. Tukianza na sababu ya kwanza, (more…)

#SheriaYaLeo (151/366); Kila mtu anataka mamlaka zaidi.

By | March 31, 2022

#SheriaYaLeo (151/366); Kila mtu anataka mamlaka zaidi. Watu huwa wanafanya yale wanayofanya ili kupata mamlaka zaidi. Ipo kauli kwamba mamlaka huwa yanawaharibu watu. Lakini kinyume chake pia ni kweli. Kukosa mamlaka kunawaharibu watu pia. Hakuna anayeweza kuvumilia hali ya kutokuwa na mamlaka. Hivyo mtu hufanya lolote ili tu kupata mamlaka. (more…)

2646; Watu hawabadiliki, wanakufa.

By | March 30, 2022

2646; Watu hawabadiliki, wanakufa. Kwenye moja ya mahijiano aliyokuwa anafanyiwa, bilionea Elon Musk aliulizwa kwamba anafanya uwekezaji mkubwa sana kwenye teknolojia na anga, mbona hawekezi kwenye kuongeza umri wa watu kuishi? Elon alitoa jibu ambalo lilinifanya nifikiri kwa kina kuhusu asili yetu kama binadamu na namna bora ya kuendana na (more…)

#SheriaYaLeo (150/366); Usichukulie chochote kwa ubinafsi.

By | March 30, 2022

#SheriaYaLeo (150/366); Usichukulie chochote kwa ubinafsi. Katika safari ya maisha utakutana na watu mbalimbali, ambao watafanya mambo ambayo hukutegemea wafanye. Ni rahisi kuchukulia hayo kibinafsi, kuona wamefanya ili kukuonea na mtazamo mwingine wa aina hiyo. Lakini hilo siyo sahihi, watu hawafanyi lolote kwa ajili yako, bali wanafanya kwa ajili yao (more…)

2645; Mstari ni mwembamba sana.

By | March 29, 2022

2645; Mstari ni mwembamba sana. Kuna mstari mwembamba sana kati ya ushujaa na utapeli. Kadhalika katika ya kufanikiwa na kushindwa, mshari ni mwembamba sana. Elon Musk huwa anasema ilikuwa imebaki siku moja tu kampuni yake ya Tesla ifilisike. Kampuni ilikuwa inahitaji sana fedha na hakukuwa na aliyekuwa tayari kuwezeka kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (149/366); Ukweli halisi.

By | March 29, 2022

#SheriaYaLeo (149/366); Ukweli halisi. Watu wapo tayari kusema chochote ili tu kutetea na kuhalalisha matendo yao. Watatoa sababu na hadithi za kila aina kuonyesha kwamba matendo yao ni sahihi, muhimu na yenye manufaa kwa wengine. Kwa kuwasikiliza watu, unaweza kuwaamini kwa yale wanayosema, maana wanakuwa wamejipanga vizuri kweli. Lakini huwezi (more…)

ONGEA NA KOCHA; HELL YEAH, BOSCO MLOMO.

By | March 28, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kuna mambo matatu makubwa. Jambo la kwanza ni uchambuzi wa kitabu cha HELL YEAH OR NO kilichoandikwa na Derek Sivers. Kwenye kitabu hiki mwandishi ametushirikisha falsafa yake fupi ya kuchagua nini afanye. Anatuambia kama kitu hukipi NDIYO kubwa basi unapaswa (more…)

2644; Hizo nguvu hazitumiki vizuri.

By | March 28, 2022

2644; Hizo nguvu hazitumiki vizuri. Kanuni za fizikia ni kanuni za asili, hakuna namna unaweza kuzivunja. Moja ya kanuni za fizikia ni ile ya nguvu au nishati. Ambayo inasema huwezi kutengeneza au kuharibu nishati, bali unaweza kuibadili kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine. Unapowasha mkaa, nguvu ya kemikali iliyo ndani yake (more…)

#SheriaYaLeo (148/366); Jua nia zao halisi.

By | March 28, 2022

#SheriaYaLeo (148/366); Jua nia zao halisi. Kwa kawaida sisi binadamu ni wabinafsi. Huwa hatufanyi mambo kama hayana manufaa kwetu. Hivyo kwa kila jambo ambalo watu wanafanya, jua kuna manufaa fulani wanayoyapata. Mara nyingi hilo linaweza lisiwe wazi. Wengi wenye nia isiyo njema huwa wanaificha. Wanatengeneza mwonekano fulani wa kuficha nia (more…)