Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Mambo muhimu ya kufanya pale mauzo yanaposhuka.

By | March 23, 2015

Wewe kama mjasiriamali kipato chako kinategemea mauzo ya bidhaa au huduma unayotoa. Hii ni sawa na kusema kwmaba kama huuzi basi huna biashara na kama huna biashara maana yake upo kwenye hali mbaya sana kifedha. Vile vile katika ujasiriamali, kipato hakilingani siku zote, kuna wakati ambao utakuwa na kipato kikubwa (more…)

Nani ni mshindani wako kwenye biashara? Umuhimu wa kujua na jinsi ya kutumia vizuri ushindani.

By | March 16, 2015

Kila biashara ina ushindani, kama unaamini kwamba biashara yako wewe haina ushindani basi bado hujaijua vizuri biashara unayofanya. Na kwa maana hiyo basi upo kwenye hatari kubwa sana ya kuondolewa kwenye biashara hiyo kama hutobadilika. Katika makala ya leo hapa kwenye KONA YA MJASIRIAMALI, tutajadili umuhimu wa kujuwa mshindani au (more…)

Matumizi sahihi ya mtandao wa intaneti katika ukuaji wa biashara yako.

By | March 9, 2015

Dunia imebadilika sana kwa siku hizi. Mambo ambayo yalikuwa yanafanyika miaka ya nyuma sasa hivi ni kama hayana faida tena au hayaendani na mazingira tuliyopo. Moja ya mabadiliko makubwa yaliyotokea duniani ni kusambaa kwa mtandao wa intaneti. Miaka 20 iliyopita mtandao wa intaneti ulikuwa unatumika na watu wachache sana na (more…)

Je ni kweli unahitaji mkopo kwenye biashara yako?

By | March 2, 2015

Zamani kidogo, kabla taasisi za kifedha hazijawa nyingi hapa nchini, kupata mkopo ilikuwa ni kazi kubwa sana. Ulihitaji kuwa na sifa nyingi zinazokuwezesha kupata mkopo na hata ukiwa nazo bado ulihitaji kusubiri mlolongo mrefu ndio uweze kupata mkopo unaohitaji. Sasa hivi mambo yamebadilika sana, taasisi za kifedha zimekuwa nyingi sana (more…)

Je unamiliki biashara au biashara inakumiliki?

By | February 23, 2015

Hakuna kitu kizuri kwenye maisha ya sasa kama kuwa mjasiriamali. Kwa nini? Sababu zipo wazi na tumekuwa tunazijadili kwenye kona hii mara kwa mara. Na faida kubwa kabisa katika faida nyingi za kuwa mjasiriamali ni kuwa na uhuru wa maisha yako. Unapokuwa mjasiriamali unakuwa na uhuru ufanye nini ambacho kitakuwa (more…)

Mbinu bora na rahisi ya kutangaza biashara yako.

By | February 16, 2015

Wote tunajua kwamba biashara ni wateja, ili biashara iweze kuendelea ni lazima iwe na wateja. Kama una bidhaa au huduma nzuri sana ambayo inaweza kuwasaidia watu wengi lakini hakuna watu ambao wapo tayari kuinunua, huna biashara. Lengo la biashara yoyote ni kutengeneza wateja halafu wateja ndio wanaleta faida na faida (more…)

Mbinu Sita za kukuza biashara yako.

By | February 9, 2015

Kila mtu anayeingia kwenye ujasiriamali na biashara, moja ya malengo yake ni kukua kupitia biashara hiyo. Wajasiriamali wengi huanza kidogo wakitegemea kwamba kwa kufanya juhidi na maarifa watakua na kufikia nafasi kubwa sana. Kwa Bahati mbaya sana hiki sio kinachotokea kwa wajasiriamali wengi. Wajasiriamali wengi wanaishia kuendesha biashara ambazo zinadumaa (more…)

Uwekezaji wa faida kwenye biashara.

By | February 2, 2015

Moja ya njia ambazo wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo wanazotumia kupata mtaji wa biashara ni kupitia akiba zao wenyewe. Hii ni njia bora sana kwani inakupa wakati mzuri wa kuweza kukuza biashara yako bila ya kufikiria kuhitajika kulipa mkopo wakati bado biashara haijakomaa. Lakini pia wajasiriamali na wafanyabiashara wengi wadogo wamekuwa (more…)

Upangaji na mabadiliko ya bei kwenye biashara.

By | January 26, 2015

Moja ya maeneo muhimu sana kwenye biashara yako wewe kama mjasiriamali ni upangaji wa bei za bidhaa au huduma unazotoa. Hili ni eneo muhimu kwa sababu ukikosea kupanga bei unaweza kuiathiri biashara yako kwa kiasi kikubwa sana. Unaweza kukosa wateja au hata kupoteza wateja uliokuwa nao awali. Katika makala ya (more…)

Makosa Makubwa Yanayofanywa Na Wajasiriamali Wageni.

By | January 19, 2015

Kama ilivyo kwenye jambo lolote kwenye maisha, watu wanaoingia kwenye ujasiriamali kwa mara ya kwanza huwa wanafanya makosa mengi sana. Kwa wale wanaogundua makosa haya na kuyatumia vizuri wanaweza kufanikiwa sana. Ila wale wanaoshindwa kujifunza kupitia makosa yao huishia kushindwa na kukata tamaa kabisa. Kama unataka kuingia kwenye ujasiriamali ni (more…)