Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi.

By | April 22, 2022

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi. Changamoto kubwa tunazokutana nazo kwenye maisha huwa zinaanzia kwenye hukumu tunazotoa kwa wengine. Mara nyingi hukumu hizo huwa ni za upendeleo. Kama mtu tunampenda au kukubaliana naye tunamhukumu vizuri kwa sababu tunaona upande wake mzuri tu. Na kama mtu hatumpendi au (more…)

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha.

By | April 21, 2022

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha. Kuna vitu vingi unajifunza kuhusu mafanikio, lakini kina unapojaribu kuviishi unashindwa. Labda umejifunza umuhimu wa kutumia muda wako vizuri na kutokuupoteza kwenye mambo yasiyo na tija. Unajaribu kuzingatia hilo ila bado unajikuta tu unapoteza muda kwa mambo yasiyo na tija. Labda umejifunza kwamba kuongea sana (more…)

2667; Sumu ya mafanikio.

By | April 20, 2022

2667; Sumu ya mafanikio. Huwa kuna hadithi fupi kuhusu mwanzilishi wa Dubai ambayo huwa inazunguka sana mtandaoni. Mwanzilishi huyo anaulizwa anauonaje mustakabali wa nchi yake, anajibu kama ifuatavyo; Babu yangu aliendesha ngamia, baba yangu akaendesha ngamia, mimi ninaendesha Mercedea, mtoto wangu anaendesha Land Rover na mjukuu wangu atakuja kuendesha Land (more…)

2666; Umetingwa na yapi?

By | April 19, 2022

2666; Umetingwa na yapi? Kutingwa au kuwa bize kama wengi walivyozoea kutumia ndiyo kuna nguvu kubwa ya kuamua matokeo ambayo mtu anayapata kwenye maisha yake. Kile kinachokuweka bize ndiyo kinachozalisha matokeo kwenye maisha yako. Matokeo unayopata sasa, iwe ni mazuri au mabaya yamezalishwa na yale yaliyokutinga huko nyuma. Usilaumu watu (more…)

2665; Unahitaji watu wa kukusukuma.

By | April 18, 2022

2665; Unahitaji watu wa kukusukuma. Pamoja na magumu na changamoto mbalimbali za dunia, bado asili ya binadamu huwa ina nguvu sana. Kwa mfano, ni asili yetu binadamu kuridhika na kile ambacho tayari tumeshakipata. Pamoja na kwamba dunia inabadilika na chochote kinachoturidhisha sasa hakiwezi kuturidhisha kesho, bado hatuwezi kulivuka hilo peke (more…)

2664; Ni wewe umewafundisha.

By | April 17, 2022

2664; Ni wewe umewafundisha. Kama watu wanakuchukulia kwa namna ambayo hupendezwi nayo, wao siyo wa kulaumu, bali wewe ndiye wa kujilaumu. Kwani kwa vyovyote vile watu wanavyokuchukulia, ni wewe umewafundisha. Wewe ndiye umewaonyesha na kuwaruhusu kwa namna gani wanaweza kukuchukulia. Kama watu wanakudharau, ni kwa sababu umewaonyesha ni sawa wao (more…)

2663; Ambacho hutumii nguvu kufanya.

By | April 16, 2022

2663; Ambacho hutumii nguvu kufanya. Watu wamekuwa wanajiuliza sana ni njia ipi rahisi ya kufanikiwa. Ni kipi ambacho wakifanya watafanikiwa. Wamekuwa wakiwaangalia wale waliofanikiwa kwenye yale wanayoyafanya na kujaribu kuyaiga. Lakini bado hawafanikiwi. Hawafanikiwi kwa sababu wanajaribu kuiga vitu vya nje, Wakati mafanikio yanatokana na vitu vya ndani. Mengi yameandikwa (more…)

2662; Kama Ninge….

By | April 15, 2022

2662; Kama Ninge…. Hakuna njia rahisi ya kuyaharibu maisha yako na kujizuia kufanikiwa kama kuwa na majuto. Kuangalia yale ambayo hukufanya au hukuchagua na kuona labda ndiyo yangekuwa bora ni uhakika unachofanya sasa hakiwezi kuwa bora. Uliacha kazi na kuingia kwenye biashara, lakini mambo hayaendi kama ulivyotegemea. Unaweza kujiambia, kama (more…)

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia.

By | April 14, 2022

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia. Mpishi mmoja mbobezi amewahi kusema njia ya haraka ya kujua kama chakula ni kizuri au kibaya ni kuangalia viungo ambavyo vimewekwa kwenye chakula hicho. Akaendelea kusema unapoona chakula kina viungo vingi sana, jua siyo kizuri. Hivyo wanaweka viungo vingi ili kukuvuruga usione uhalisia. Alitumia maneno makali (more…)