#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu.

By | April 10, 2022

#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu. Watu wanapenda sifa na kutukuzwa, wanapenda kuona wapo juu na wengine wanawategemea kwa mambo mbalimbali. Pale unapotaka kitu kutoka kwa watu, hasa wale wenye mamlaka, wafanye wajione wako juu. Wafanye waone upo chini yao na unawategemea sana kwa kile unachotaka. Hilo linawafanya wajione (more…)

2656; Teknolojia itakunyoosha.

By | April 9, 2022

2656; Teknolojia itakunyoosha. Siku siyo nyingi nilikuwa nataka kuwahi mahali na hivyo kuhitaji usafiri wa haraka wa pikipiki. Nikitumia mtandao wa kuita vyombo vya usafiri na mara moja usafiri ukaja. Lakini dereva aliyekuja hakuwa mzuri, hakuendesha vizuri wala kufuata vyema maelekezo. Pamoja na kumwambia lakini hakuonekana kusikiliza au kuelewa. Basi (more…)

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi.

By | April 9, 2022

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi. Kwa chochote unachotaka, kuna watu ambao ni kikwazo kwako, ambao wapo tayari kukuzuia usikipate. Njia bora ya kuwavuka watu hao na kupata kile unachotaka ni kuwavuruga. Unawavuruga kwa kuwahadaa, kuwafanya waone unataka kitu kingine ambacho siyo nia yako halisi. Kwa njia hii huendei (more…)

2655; Tatizo lako umekosa msimamo.

By | April 8, 2022

2655; Tatizo lako umekosa msimamo. Unakumbuka ile siku ambayo ulihudhuria semina, ukajifunza mambo mengi na kutoka na hamasa ya kwenda kuyabadili kabisa maisha yako. Siku chache za mwanzo ukawa wa tofauti kabisa, ukijituma kweli kweli. Lakini baada ya muda ukarudi kwenye mazoea yako. Unakumbuka mara zote ambazo umekuwa unasoma vitabu (more…)

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine.

By | April 8, 2022

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine. Huwa hatupendi kukubali kwamba wengine wana akili kuliko sisi. Tunapokutana na watu wenye akili sana, huwa tunatafuta kila njia ya kujitetea ili kuonyesha kwamba hatupo nyuma. Tutasema wana akili za darasani tu. Au wana akili kwa sababu walisoma shule za gharama kubwa. Au wana (more…)

2654; Kumbuka wewe ni binadamu.

By | April 7, 2022

2654; Kumbuka wewe ni binadamu. Kadiri ninavyokaa kwenye hii huduma ya ukocha, ndivyo ninavyojifunza kwa karibu tabia za watu na kuwa bora zaidi katika kuwasaidia kufika kule wanakotaja kufika. Zamani alikuwa akija mtu kwangu, mwenye njaa kweli ya mafanikio na anayesema yupo tayari kufanya kazi usiku na mchana ili kupata (more…)

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri.

By | April 7, 2022

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri. Maisha ni maigizo, kile ambacho watu wanaonyesha kwa nje, sivyo walivyo ndani yao. Hivyo moja ya wajibu wako mkubwa kwenye maisha ni kuigiza nafasi yako vizuri. Hasa kwenye eneo la hisia, lazima uweze kuvaa hisia sahihi kwa wakati sahihi. Pale unapohitajika kuwa na hisia (more…)

#SheriaYaLeo (157/366); Waweke watu kwenye shauku ya kukufuatilia.

By | April 6, 2022

#SheriaYaLeo (157/366); Waweke watu kwenye shauku ya kukufuatilia. Watu huwa wanapenda kufuatilia vitu ambavyo vinawaweka juu juu. Vitu ambavyo hawana uhakika vitakwendaje. Vitu ambavyo ni tofauti kabisa na mazoea na hivyo havitabiriki. Kwa kila unachofanya, kifanye kwa namna hiyo na siyo kwa mazoea. Wafanye watu wawe wanajiuliza kipi kingine utafanya (more…)

2652; Kuchuma matunda ya chini.

By | April 5, 2022

2652; Kuchuma matunda ya chini. Ukiingia kwenye shamba jipya la matunda kama miembe au michungwa, inakuwa rahisi kuchuma matunda hayo. Kwa sababu yanakuwa yananing’inia kwa chini na karibu kabisa kufikia kwa mkono. Utaona hiyo ni fursa na kuifurahia, kwa kuwa unayapata matunda kirahisi kabisa, bila ya kutumia nguvu kubwa. Lakini (more…)