Tag Archives: USHAURI WA BIASHARA

BIASHARA LEO; Njia Tatu Muhimu Za Kukuza Biashara Yako.

By | June 9, 2015

Unafanyia kazi haya unayojifunza kwenye kipengele hiki cha BIASHARA LEO? Kama unafanyia tushirikishe kwenye maoni hapo chini ni jinsi gani biashara yako inabadilika. Na kama hufanyii kazi tuambie ni kwa nini? Yote tunayojifunza kwenye kipengele hiki sio vitu vya kufurahia kusoma, bali ni vitu unatakiwa kufanya. Unasoma kitu hapa na (more…)

Jinsi ya kutumia wateja wako kama sehemu ya kutangaza biashara yako.

By | June 8, 2015

Linapokuja swala la kutangaza biashara, watu hufikiria matangazo kwenye vyombo vikubwa vya habari, kupata tangazo wakati wa taarifa ya habari, ambapo watu wengi wanaangalia. Au kudhamini michezo inayofuatiliwa na wengi. Au kuweka bango kubwa kwenye eneo ambalo watu wengi wanapita. Hizi zote ni njia nzuri za kutangaza biashara yako, ila (more…)

BIASHARA LEO; Usihofu Kama Watu Hawakuelewi.

By | June 6, 2015

Moja ya changamoto za kuwa mjasiriamali ni kwamba watu wengi hawatakuelewa. Kama unayafanyia kazi haya mambo ambayo unajifunza hapa kila siku, watu wengi hawawezi kukuelewa. Usiogope pale hali hii inapotokea, maana ndio umeanza kuuelewa ujasiriamali. Watu wengi hawawezi kukuelewa kwa sababu walitegemea ufanye biashara kama wanavyofanya wao. Ufungue biashara yako (more…)

BIASHARA LEO; Kama Sio Namba Moja Au Namba Mbili Acha Kupoteza Muda Wako.

By | June 5, 2015

Kwa haraka tu na bila ya kuzunguka zunguka nikuambie kwamba biashara unayofanya kama wewe sio namba moja, au sio namba mbili basi acha kupoteza muda wako kwenye hiyo biashara. Kama sio namba moja au namba mbili kwenye biashara unayofanya maana yake huna biashara yenye wateja wa kutosha, unapata wale wateja (more…)

BIASHARA LEO; Biashara Inayolipa Kuliko Hiyo Unayofanya Sasa.

By | June 4, 2015

Katika wakati wowote kwenye maisha yako ya kibiashara, kuna biashara ambayo itakuwa inalipa kuliko biashara unayofanya wewe. Katika hali hii unaweza kushawishika kwamba biashara uliyopo wewe sio nzuri na kutamani kuwepo kwenye biashara ile ambayo inalipa. Na kuna baadhi ya watu huamua hata kufanya maamuzi ya kubadili biashara na kuhamia (more…)

BIASHARA LEO; Sababu Moja Kwa Nini Biashara Yako Haina Soko.

By | June 3, 2015

Kama biashara haina soko kuna jambo moja tuna uhakika nalo, itakufa. Hakuna biashara ambayo itaweza kujiendesha bila ya kuwa na wateja. Mafanikio yako wewe kama mfanyabiashara ni kiasi gani cha soko umeshika. Kuna biashara nyingi sana ambazo zinakufa kwa kukosa soko. Leo nataka nikupe sababu moja kwa nini biashara yako (more…)

BIASHARA LEO; Kabla Hujaanza Biashara Yoyote Mpya, Zingatia Jambo Hili Moja Muhimu Sana.

By | June 2, 2015

Biashara mpya zina kasi kubwa sana ya kushindwa. Hapa kwetu Tanzania hatuna tafiti za kutosha ila kwa nchi zilizoendelea na zilizofanya tafiti, biashara 8 kati ya 10 zinazoanzishwa hufa mwaka mmoja baada ya kuanzishwa. Hii ni hatari sana na kwa uzoefu tu hapa kwetu hali inaweza kuwa mbaya zaidi. Kuna (more…)

Tofauti ya biashara kubwa na biashara ndogo na jinsi ya kuitumia kukuza biashara yako.

By | June 1, 2015

  Wafanyabiashara wengi wadogo wamekuwa wanafanya kosa moja kubwa sana linalogharimu ukuaji wa biashara zao. Kwa kufanya kosa hili wamekuwa wakishindwa kukuza biashara zao na hivyo biashara kufa au kubaki kwenye kiwango kilekile. Kosa kubwa ambalo wafanyabiashara wengi wadogo wamekuwa wanafanya ni kufikiri kwamba biashara ndogo ni aina ndogo ya (more…)

BIASHARA LEO; Hiki Ndio Kikomo Cha Biashara Yako Kukua.

By | May 30, 2015

Biashara yako ina ukomo wake wa kukua, yaani biashara inaweza kukua mpaka itakapofikia ukomo huo utakaoujua leo. Bila ya kujua ukomo hii ni vigumu sana kwa biashara yako kuweza kukua zaidi. Wafanyabiashara wengi ambao biashara zao zimedumaa hawajui kwamba tayari zimefikia ukomo. Hivyo hukazana kufanya mambo mengi ambayo bado hayasaidii (more…)

BIASHARA LEO; Hatua Za Kuajiri Wafanyakazi Bora Kwenye Biashara Yako.

By | May 28, 2015

Mafanikio ya biashara yako yatategemea wafanyakazi utakaokuwa nao kwenye biashara yako. Kwanza kama unafikiria kw anini uajiri, kama bado ni mfanyabiashara mdogo na unafanya kila kitu peke yako, ni muhimu sana kuandaa mpango wa kuajiri ili wakati wa kuajiri utakapofika usipate tabu. Jua majukumu unayohitaji kuyatoa kwa wengine ili biashara (more…)