Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (296/366); Usipotezwe na vitu visivyo na tija.

By | August 23, 2022

#SheriaYaLeo (296/366); Usipotezwe na vitu visivyo na tija. Kuna wakati unajikuta umezidiwa na majukumu ambayo unapaswa kuyatekeleza. Unajikuta ukiwa na mambo mengi ya kufanya, lakini muda wa kuyafanya unakuwa mdogo. Ni katika wakati huo ndiyo unapata hali ya kuvurugwa, kwa kuona kuna mambo unapoteza au unayakosa kwa sababu umepoteza udhibiti. (more…)

2791; Uwanja wa nyumbani.

By | August 22, 2022

2791; Uwanja wa nyumbani. Kwenye michezo yote, huwa kuna dhana ya uwanja wa nyumbani. Kwamba timu inakuwa kwenye nafasi nzuri ya kushinda inapokuwa inacheza kwenye uwanja wa nyumbani. Hivyo timu inapokuwa inacheza uwanja wa ugenini, huko hucheza kwa kujilinda zaidi ili isifungwe. Timu ikiwa ugenini haiangalii sana kusinda, bali inakazana (more…)

#SheriaYaLeo (295/366); Tambua msukumo wako wa shari.

By | August 22, 2022

#SheriaYaLeo (295/366); Tambua msukumo wako wa shari. Sisi binadamu tuna asili ya ushari. Na hilo siyo jambo baya mara zote. Maana ni ushari huo ndiyo unaotupa msukumo wa kufanya makubwa na kufanikiwa. Lakini pale ushari huo unaposhindwa kudhibitiwa vizuri, unakuwa chanzo cha machafuko makubwa. Wizi, utapeli, uhasama na vita yote (more…)

2790; Kuna anayeweza kununua kwako?

By | August 21, 2022

2790; Kuna anayeweza kununua kwako? Hivi karibuni nilikutana na ujumbe unaozunguka mtandaoni unaosema kampuni ya magari ya Lamboghini (moja ya magari ya bei ghali zaidi) huwa haijitangazi kwenye tv kwa sababu watu wanaoweza kumudu kununua aina hiyo ya magari, hutawakuta wamekaa wanaangalia tv. Ujumbe huo unaweza kuchukuliwa kama kichekesho, lakini (more…)

#SheriaYaLeo (294/366); Ona zaidi ya wakati uliopo.

By | August 21, 2022

#SheriaYaLeo (294/366); Ona zaidi ya wakati uliopo. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya kuishi kwenye wakati uliopo. Hii ni sehemu kubwa ya asili yetu, ambayo tumeipata kutoka kwa wanyama. Mara nyingi huwa tunakimbilia kujibu kile kilicho mbele yetu kwa wakati husika, ambacho kinanasa umakini wetu zaidi. Lakini sisi siyo tu (more…)

#SheriaYaLeo (293/366); Wakubali watu kama walivyo.

By | August 20, 2022

#SheriaYaLeo (293/366); Wakubali watu kama walivyo. Kuchangamana na watu wengine ndiyo moja ya chanzo kikuu cha matatizo ya kihisia, lakini haipaswi kuwa hivyo. Tatizo ni kwamba huwa tunawahukumu watu mara zote, tukitamani wangekuwa tofauti na walivyo. Huwa tunataka kuwabadili watu, tukitaka wafikiri na kufanya kama sisi. Lakini hilo huwa haliwezekani, (more…)

2788; Usiage mashindano.

By | August 19, 2022

2788; Usiage mashindano. Fikiria timu yako unayoipenda ya mpira wa miguu. Imeingia uwanjani kushindana na timu nyingine. Dakika tano tu za kwanza za mchezo, timu yako inafungwa goli moja. Cha kushangaza sasa, baada ya kufungwa goli hilo moja, wachezaji wote wanaamu kuondoka uwanjani. Wanajiona hawafai kabisa, wamefungwa haraka na hawana (more…)

#SheriaYaLeo (292/366); Fikiria kama mwandishi.

By | August 19, 2022

#SheriaYaLeo (292/366); Fikiria kama mwandishi. Waandishi huwa wanachunguza kitu kwa ndani ili kuweza kujua uhalisia wake. Huwa hawachukulii kitu juu juu kama wanavyofanya watu wengine. Kwanza kabisa wanajizuia wasihukumu kitu chochote kile wanachofanya watu, hata kama ni kibaya kiasi gani. Huchukulia kwamba watu wana sababu ya kila wanachofanya, sababu inayoonekana (more…)

2787; Jipe uhakika mwenyewe.

By | August 18, 2022

2787; Jipe uhakika mwenyewe. Kitu kimoja kinachotukwamisha sana kwenye maisha ni kukosa uhakika. Hilo ndiyo limekuwa linatuzuia kufanya maamuzi na hata tukifanya maamuzi tunashindwa kuyasimamia. Kwa mfano nikikupa wateja 10 ambao kwa uhakika watanunua kwako, ila wanachosubiri ni wewe uwatembelee, utafanya kila namna kuwatembelea. Hutakuwa na sababu yoyote ya kukuzuia, (more…)