Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (301/366); Ona kivuli chako.

By | August 28, 2022

#SheriaYaLeo (301/366); Ona kivuli chako. Kila mtu huwa ana pande mbili. Upande mzuri ambao ndiyo anauonyesha kwa wengine. Na upande mbaya ambao anauficha. Wengi wakiwa hadharani hufanya mambo mazuri na ya kupendeza. Lakini wakiwa faraghani hufanya mambo mabaya na yasiyo ya kupendeza. Na mara nyingi, wale wanaojionyesha ni wema sana (more…)

2796; Uhakika kwamba unaweza kufanikiwa.

By | August 27, 2022

2796; Uhakika kwamba unaweza kufanikiwa. Thomas Edison amewahi kunukuliwa akisema; “Kama tungefanya mambo yote tunayoweza kufanya, tungejishangaza wenyewe.” Sina cha kuongeza hapo, tunaenda moja kwa moja kwenye hatua ya kuchukua. Hatua ya kuchukua; Chukua kalamu na karatasi na orodhesha mambo yote unayoweza kufanya kwenye biashara au kazi yako. Orodhesha yote (more…)

#SheriaYaLeo (300/366); Kataa maelezo rahisi.

By | August 27, 2022

#SheriaYaLeo (300/366); Kataa maelezo rahisi. Sisi binadamu huwa tuna ukomo fulani kwenye uwezo wetu wa kufikiri ambao ndiyo chanzo cha matatizo mengi tunayokutana nayo. Tunapofikiria kuhusu watu au kitu ambacho kimetokea, huwa tunakimbilia kwenye maelezo rahisi kwetu kuelewa. Huwa tunakimbilia kwenye kuangalia kama mtu au kitu ni kizuri au kibaya, (more…)

#SheriaYaLeo (299/366); Chunguza mizizi ya hisia zako.

By | August 26, 2022

#SheriaYaLeo (299/366); Chunguza mizizi ya hisia zako. Kila hisia unazokuwa nazo, huwa zinakuwa na mizizi yake ambayo huwa haionekani wazi. Ni mpaka uchunguze kwa kina ndiyo utaweza kujua chanzo halisi cha hisia unazokuwa nazo. Kwa mfano umepatwa na hasira, unapaswa kuacha hisia hizo zitulie, kisha kuchunguza nini kimezisababisha. Kama zimesababishwa (more…)

#SheriaYaLeo (298/366); Jua hujui.

By | August 25, 2022

#SheriaYaLeo (298/366); Jua hujui. Huwa tunapenda kuwabeza watu wa zama zilizopita jinsi ambavyo hawakuwa wanajua yale ambayo tunajua sasa. Tunaona kama walikuwa watu wajinga na walioshindwa kujua yale ya msingi. Hebu fikiria ni kwa namna gani watu wa vizazi vijavyo watatushangaa na kutubeza kwa mambo tunayofanya sasa. Kuna mengi tunajua, (more…)

2793; Eneo lako la nguvu.

By | August 24, 2022

2793; Eneo lako la nguvu. Jamii huwa inapenda kuwadhibiti na kuwatawala watu. Na ili kuhakikisha hilo linafanikiwa, hatua kubwa na ya kwanza ambayo jamii huwa inafanya ni kuhakikisha mtu hawi yeye. Kwa sababu inajua mtu ana nguvu na mamlaka makubwa sana pale anapokuwa yeye, anapokuwa halisi kwake. Hivyo inakuondoa kwanza (more…)

#SheriaYaLeo (297/366); Nafsi iliyopotea.

By | August 24, 2022

#SheriaYaLeo (297/366); Nafsi iliyopotea. Kila mtu huwa ana nafsi yake ambayo ameipoteza. Hilo linatokana na mtu kuchagua kuwa kama vile ambavyo watu wanataka awe na siyo kama anavyosukumwa kuwa kutoka ndani yake. Wajibu wako mkubwa kwenye maisha ni kuondokana na hali ya mgando unayokuwa nayo, vile unavyojiweka ili kuwaridhisha wengine. (more…)

2792; Umewafundisha?

By | August 23, 2022

2792; Umewafundisha? Kama watu hawafanyi kitu, kuna sababu mbili tu; HAWAWEZI au HAWATAKI. Wanakuwa hawawezi pale wanapokuwa hawajui jinsi ya kufanya kitu hicho. Hilo linakuwa gumu kwao kufanya. Na mbaya zaidi, watu huwa hawapendi kukiri kwamba hawajui. Hivyo hujifanya wanajua, lakini kutokujua kwao kunakuwa kikwazo kwenye ufanyaji. Hapo hujaweka hali (more…)