Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (246/366); Dhibiti mchezo mzima.

By | July 4, 2022

#SheriaYaLeo (246/366); Dhibiti mchezo mzima. Maisha ni kama mchezo wa drafti. Anayefanikiwa ni yule anayekuwa na udhibiti kwenye mchezo mzima. Kila kete inachezwa kwa kusudi maalumu, ambalo ni kupata ushindi mkubwa baadaye. Hivyo ndivyo maisha yanavyokuwa. Hakun hatua yoyote inayochukuliwa kwa kubahatisha. Badala yake kila hatua inakuwa imepimwa na kupangiliwa (more…)

#SheriaYaLeo (245/366); Fikiria zaidi ya pale ulipo sasa.

By | July 3, 2022

#SheriaYaLeo (245/366); Fikiria zaidi ya pale ulipo sasa. Kwenye vita, mkakati ni sanaa ya kudhibiti mpango mzima wa kivita. Wakati mbinu ni ujuzi wa kukabiliana na pambano lililo mbele yako. Wengi wetu kwenye maisha ni watu wa mbinu badala ya mikakati. Tunavurugwa na yale yanayoendelea kwa wakati huo kiasi kwamba (more…)

2740; Wanataka kukutumia.

By | July 2, 2022

2740; Wanataka kukutumia. Baadhi ya mambo ambayo tumekuwa tunajifunza kuhusu binadamu ni ubinafsi na maslahi. Huwa tuna ubinafsi mkubwa na kujali zaidi maslahi yetu wenyewe. Na hilo ndiyo linawafanya watu kuwa tayari kuwatumia wengine pale wanapoona kuna maslahi mazuri kwa ajili yao. Hivyo lazima ujue kwenye mahusiano yako mengi na (more…)

#SheriaYaLeo (244/366); Yatambue maoni yako mwenyewe.

By | July 2, 2022

#SheriaYaLeo (244/366); Yatambue maoni yako mwenyewe. Tambua ya kwamba hata wewe una maoni yako mwenyewe. Tambua jinsi maoni hayo yanafanya kazi ndani yako. Kubali kwamba haupo huru kama unavyodhani. Umekuwa unashawishiwa na wengine kwa namna mbalimbali. Lazima pia utambue ya kwamba siyo mjanja kama unavyojichukulia. Unaweza kulaghaiwa na kushawishiwa kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (243/366); Wachukulie kwa mtazamo sahihi.

By | July 1, 2022

#SheriaYaLeo (243/366); Wachukulie kwa mtazamo sahihi. Jinsi unavyowachukulia watu, ndivyo pia wanavyokuwa. Matarajio uliyonayo kwa watu ndiyo matokeo utakayoyapata hata kama hutawaambia moja kwa moja. Tegemea watu watafanya vizuri au kuwa vizuri na hilo ndiyo litatokea. Na kama utategemea watu wafanye vibaya au kuwa wabaya ndivyo watakavyokuwa. Matarajio yetu kwa (more…)

2738; Siyo lazima ufanye.

By | June 30, 2022

2738; Siyo lazima ufanye. Sehemu kubwa ya msongo tunaokuwa nao kwenye maisha huwa ni wa kujitakia. Tunakuwa na msongo pale tunapoona kwamba ni lazima tufanye vitu fulani ambavyo tumejiambia tunapaswa kufanya. Ukweli ni kwamba hulazimiki kufanya kitu chochote kile. Mahangaiko unayokuwa nayo kwenye kujilazimisha kufanya vitu, ni kujipa tu umaarufu (more…)

#SheriaYaLeo (242/366); Waambukize hisia sahihi.

By | June 30, 2022

#SheriaYaLeo (242/366); Waambukize hisia sahihi. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia ambapo maamuzi yetu huwa tunayafanya kwa kusukumwa na hisia. Kama unataka kuwashawishi watu, itakuwa rahisi kwako kama utaanza kwa kugusa hisia zao. Na njia rahisi ya kugusa hisia ni kwa kuziambukiza. Anza kwa kuwa na zile hisia ambazo unataka (more…)

2737; Hakuna ambacho umewahi kufanya mara moja ukawa umemaliza.

By | June 29, 2022

2737; Hakuna ambacho umewahi kufanya mara moja ukawa umemaliza. Unakula chakula kila siku, Hakuna kitu unaweza kula mara moja na kuwa umeshiba milele. Unasafisha mwili wako kila siku. Hakuna namna ya kuusafisha mara moja na ukawa msafi milele. Ukitaka kupungua uzito unafanya mazoezi kila siku. Ukitaka kupata utajiri unaongeza kipato (more…)