Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (251/366); Gawa ili kushinda.

By | July 9, 2022

#SheriaYaLeo (251/366); Gawa ili kushinda. Pale tunapokabiliana na kitu chochote kikubwa, iwe ni adui, jukumu au changamoto, huwa tunahofia. Ukubwa wa kile kinachotukabili unatuogopesha kwa kuona hatuwezi kukishinda. Lakini huo siyo ukweli, hakuna chochote kikubwa ambacho hatuwezi kukishinda kama tutatumia njia sahihi. Na moja ya njia bora kabisa ya kushinda (more…)

2746; Kutamani, kupanga na kufanya.

By | July 8, 2022

2746; Kutamani, kupanga na kufanya. Matamanio ni bure kabisa, kila mtu huwa anatamani kuwa na vitu vizuri. Ni matamanio ya kila binadamu kupata mafanikio makubwa. Kupanga ni rahisi, watu wengi huwa wanaweka mipango mizuri kabisa ya kupata kile wanachotamani. Wanakuwa wanajua nini wanapaswa kufanya ili kupata wanachotaka. Tatizo kubwa lipo (more…)

#SheriaYaLeo (250/366); Usimshambulie adui kwenye uimara wake.

By | July 8, 2022

#SheriaYaLeo (250/366); Usimshambulie adui kwenye uimara wake. Kile ambacho adui anakionyesha wazi wazi ndiyo uimara wake. Ukimshambulia kwenye hicho huwezi kumshinda, bali utamfanya azidi kuwa imara. Njia pekee ya kumshinda adui yeyote yule ni kumshambulia kwenye madhaifu yake. Kila mtu ana madhaifu, ambayo huwa anajaribu kuyaficha. Hivyo chochote anachokionyesha mtu (more…)

2745; Atatenganishwa na fedha zake.

By | July 7, 2022

2745; Atatenganishwa na fedha zake. Mteja yeyote yule, huwa anakutana na watu wa mauzo ambao hufanikiwa kumtenganisha na fedha zake. Mteja akiwa na fedha, kuna namna ambavyo atashawishika na watu wa mauzo na kununua vitu ambavyo hata hakuwa na uhitaji navyo. Ndiyo maana wengi wakiwa hawana fedha wanakuwa na mawazo (more…)

#SheriaYaLeo (249/366); Kuwa na machaguo mengi.

By | July 7, 2022

#SheriaYaLeo (249/366); Kuwa na machaguo mengi. Ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kupata ushindi kwenye pambano lolote lile, unachohitaji siyo mkakati bora unaofuatwa hatua kwa hatua, bali mkakati wako unapaswa kuwa na machaguo mengi kuliko aliyonayo adui yako. Badala ya kuwa na chaguo moja sahihi ambalo ndiyo unalikumbatia, mkakati bora (more…)

2744; Usichoambiwa kuhusu mauzo.

By | July 6, 2022

2744; Usichoambiwa kuhusu mauzo. Kitu kimoja ambacho watu wengi huwa hawaelewi kwa uhalisia kwenye mauzo ni kwamba mara nyingi wateja huwa wanakudanganya. Na wanafanya hivyo kwa nia njema kabisa ya kutokutaka kukuumiza. Lakini wanaishia kukuumiza zaidi kwa kutokununua kwako. Mapingamizi mengi ambayo mteja anakupa siyo halisi, hasa kwenye pingamizi la (more…)

#SheriaYaLeo (248/366); Epuka vita zisizo na manufaa.

By | July 6, 2022

#SheriaYaLeo (248/366); Epuka vita zisizo na manufaa. Siyo kila vita ni ya wewe kupigana. Siyo kila pambano lazima ushinde. Na siyo kila anayekukabili unapaswa kujibizana naye. Wengi wanakutega uingie kwenye mitego yao ili kukuvuruga usiendelee na mikakati yako mikubwa. Wanakuchosha na mapambano yasiyo na tija kitu kinachoondoa nguvu zako kwenye (more…)

#SheriaYaLeo (247/366); Piga kwenye mhimili.

By | July 5, 2022

#SheriaYaLeo (247/366); Piga kwenye mhimili. Ni kawaida ya mamlaka kuonyesha uimara wake kwa lengo la kutisha au kuhadaa wengine. Hakuna mamlaka inayopenda kuonyesha udhaifu wake, japo kila mamlaka ina udhaifu. Kila mamlaka huwa ina mhimili wake, ambapo ndiyo uimara na nguvu za mamlaka hiyo vimejikusanya. Huo ndiyo mhimili ambao unakuwa (more…)

2747; Hawaoni unachoona.

By | July 4, 2022

2742; Hawaoni unachoona. Kuna mahali unayaona maisha yako yakiwa yamefika. Hakuna mwingine yeyote mwenye maono ya aina hiyo. Watu wengine wanapokushauri, hawakushauri kulingana n maono makubwa uliyonayo ndani yako. Bali wanakushauri kwa vile wanavyoona itakupendeza zaidi. Lakini siyo kinachokupendeza ndiyo chenye manufaa kwako. Bali kile kinachoendana na maono makubwa uliyonayo (more…)