Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (241/366); Wajengee Kujiamini.

By | June 29, 2022

#SheriaYaLeo (241/366); Wajengee Kujiamini. Unapojaribu kuwashawishi watu kwenye kitu chochote, moja kati ya haya matatu litatokea. Moja unaweza kukosoa na kupinga maoni yao. Kitu ambacho kitawafanya wayalinde na kutatetea maoni yao na hapo watakuwa wagumu kushawishika. Mbili unaweza usiguse kabisa maoni yao, usiyapinge wala kuyaunga mkono, kitu ambacho hakigusi hisia (more…)

2736; Kujitoa nusu haisaidii.

By | June 28, 2022

2736; Kujitoa nusu haisaidii. Maandiko ya dini yanaeleza wazi kwamba ni bora kuwa moto au baridi, lakini siyo kuwa vuguvugu. Kuwa vugu vugu hakukuweki kwenye upande wowote wa uhakika hivyo hunufaiki kwa namna yoyote ile. Utanufaika zaidi kwa kujitoa kweli kweli kwenye upande mmoja, kuliko kujaribu kuwa kwenye kila upande. (more…)

#SheriaYaLeo (240/366); Jifunze kusikiliza kwa kina.

By | June 28, 2022

#SheriaYaLeo (240/366); Jifunze kusikiliza kwa kina. Chochote unachofikiria ni ambacho tayari unakijua. Na yale unayojua ni machache mno ukilinganisha na mengi ambayo huyajui. Unapokuwa unazungumza au kufikiria, akili yako ina tabia ya kuzunguka kwenye mambo yale yale ambayo tayari unayajua. Lakini unapokutana na watu wengine, wanakuwa na vitu vya tofauti (more…)

2735; Maana halisi ya kufokasi.

By | June 27, 2022

2735; Maana halisi ya kufokasi. Steve Jobs aliwahi kutoa hotuba iliyopendwa na wengi sana ambapo alieleza kwa ufupi sana kwamba maana halisi ya kufokasi ni kusema HAPANA. Haijalishi unafanya nini, kila mara utakuwa na machaguo mengi mbele yako. Kila mara kuna vitu vizuri vitakuja. Kuna fursa ambazo utaona hazipaswi kukupita. (more…)

#SheriaYaLeo (239/366); Tumia ndoto kubwa ambazo hawajazifikia.

By | June 27, 2022

#SheriaYaLeo (239/366); Tumia ndoto kubwa ambazo hawajazifikia. Watu wengi huwa wanaamini wana uwezo mkubwa ndani yao kuliko ule unaoonekana kwa nje. Kila mtu ana ndoto kubwa sana ambazo bado hajazifikia. Inaweza kuwa ni mafanikio makubwa wanayotaka kufikia na ngazi za juu zaidi wanazotaka kupanda. Bado wanakuwa hawajafika kule wanakotaka kufika (more…)

2734; Kama ungekuwa huogopi chochote.

By | June 26, 2022

2734; Kama ungekuwa huogopi chochote. Sehemu kubwa ya kikwazo cha watu kufanikiwa inatokana na woga ambao watu wanao. Watu wanaogopa sana kushindwa, wanaogopa kukataliwa na wanaogopa wengine watawachukuliaje. Kinachotokea ni watu kufanya mambo ambayo ni ya kawaida na yanayoficha woga wao. Na hilo linapelekea washindwe kupata mafanikio makubwa. Ili uweze (more…)

#SheriaYaLeo (238/366); Tengeneza jicho la tatu.

By | June 26, 2022

#SheriaYaLeo (238/366); Tengeneza jicho la tatu. Watu wengi huwa wamekwama kwenye wakati uliopo, kwa kuvurugwa na yale yanayoendelea kwenye wakati huo. Wanayafikiria zaidi mambo hayo kitu kinachowapelekea kupata taharuki na kufanya maamuzi ambayo siyo bora sana. Wanashindwa kuona zaidi ya kile kilichopo sasa au mbadala wake. Wachache ambao wanaweza kufikiri (more…)

2733; Hakuna kukosea.

By | June 25, 2022

2733; Hakuna kukosea. Kipindi cha nyuma kidogo palikuwa na kichekesho kwamba kulikuwa na bendi ya waimbaji ambao walikuwa wanasafiri kwenda kutoa burudani. Mmoja wa wanamuziki akawa amechomwa na msumari ndani ya gari waliyokuwa wanasafiria. Kwa kuwa aliyechomwa alikuwa muimbaji, aliamua kumwambia dereva kwamba amechomwa na msumari, lakini akamwambia kama vile (more…)

#SheriaYaLeo (237/366); Changanya ukali na wema.

By | June 25, 2022

#SheriaYaLeo (237/366); Changanya ukali na wema. Unapokuwa kiongozi unahitaji sana kuwa na ushawishi mkubwa kwa wengine ili kuweza kuwaongoza vizuri na kufanya makubwa. Njia bora ya kufanya hivyo ni kuchanganya ukali na wema. Na hilo unalifanya kupitia zawadi na adhabu unazozitoa. Kama kiongozi unapaswa kueleza taratibu za watu wako kufuata. (more…)

2732; Kukosa kwako umakini kunakuumiza.

By | June 24, 2022

2732; Kukosa kwako umakini kunakuumiza. Kiwango chako cha kukosa umakini, kinaiumiza sana biashara yako. Huo ni ujumbe nilioutuma kwa mmoja wetu baada ya kuona kuna mambo ya msingi kabisa yanamsumbua. Nilipozungumza naye, nikagundua tatizo ni kubwa kuliko nilivyokuwa nadhani awali. Na maumivu kwenye biashara yanayosababishwa na kukosekana kwa umakini yalikuwa (more…)