Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (226/366); Penyeza kwenye akili zao.

By | June 14, 2022

#SheriaYaLeo (226/366); Penyeza kwenye akili zao. Ili uweze kuwa na ushawishi kwa watu, lazima kwanza uweze kupenyeza kwenye akili zao. Mara nyingi watu ambao wana madaraka makubwa huwa hawapo tayari kusikiliza ushauri, hasa wa walio chini yao. Huku wale wasio na madaraka wakiona hawahitaji ushauri huo. Ili kuvuka ukinzani huo, (more…)

#SheriaYaLeo (225/366); Tumia hisia zao.

By | June 13, 2022

#SheriaYaLeo (225/366); Tumia hisia zao. Kama unataka kumshawishi mtu abadilike, usipingane na hisia zake, bali zitumie hizo kuchochea mabadiliko. Kama mtu ni mkorofi na mtukutu, badala ya kuyapinga hayo, mweke kwenye hali ya kutaka kubadilika ili kuonyesha ukorofi na utukutu wake. Kwa kuyafanya mabadiliko yaendane na kile ambacho tayari mtu (more…)

2720; Unataka au hutaki?

By | June 12, 2022

2720; Unataka au hutaki? Hadithi tulizokuwa tunajifunza utotoni zilikuwa na mafunzo makubwa sana, japo siyo mara zote tuliweza kuyang’amua. Chukua mfano wa hadithi ya sungura na ndizi. Sungura anapita zake, anaziona ndizi, anaona ni nzuri na kujiambia anazitaka. Anaanza kurukia ndizi zile. Anaruka na kuruka tena, Lakini hazifikii ndizi. Anaruka (more…)

#SheriaYaLeo (224/366); Bobea sanaa ya maigizo.

By | June 12, 2022

#SheriaYaLeo (224/366); Bobea sanaa ya maigizo. Huwezi kufanikiwa kwenye kuwashawishi wengine bila kubobea kwenye lugha na sanaa ya maigizo. Lazima uweze kupenyeza maneno yenye ushawishi wakati wa mazungumzo na wengine. Yanakuwa ni maneno ambayo wengine hawayatarajii, lakini yanajenga ushawishi mkubwa kwao. Ili maneno hayo yawe na nguvu ya ushawishi unapaswa (more…)

#SheriaYaLeo (223/366); Nasa Ufahari wao.

By | June 11, 2022

#SheriaYaLeo (223/366); Nasa Ufahari wao. Kila mtu huwa ana ufahari au majigambo ndani yake. Hali ya kujiona ni muhimu kwenye hii dunia. Pale mtu anapokushambulia na hujui ni kwa nini, mara nyinyi ni kwa sababu unakuwa umetishia ufahari wao. Mara zote unapaswa kuhakikisha watu wanajisikia vizuri kuhusu wao wenyewe kwa (more…)

#SheriaYaLeo (222/366); Waonjeshe dawa yao wenyewe.

By | June 10, 2022

#SheriaYaLeo (222/366); Waonjeshe dawa yao wenyewe. Kama ambavyo tumeshaona, mabishano huwa hayafanyi kazi. Kuwaambia watu kile wanachokosea hakuwafanyi wajirekebishe. Badala yake watajitetea na kuendelea kukifanya. Njia bora ya kuwapa funzo ili wabadilike ni kuwaonjesha dawa yao wenyewe. Hapo unachofanya ni kuwafanyia kile ambacho wamekufanyia wewe, kwa namna ambavyo wamekifanya. Unakifanya (more…)

2717; Nusu muda, muda kamili na muda wote (au safari ya kuelekea kwenye ubilionea).

By | June 9, 2022

2717; Nusu muda, muda kamili na muda wote (au safari ya kuelekea kwenye ubilionea). Siku chache zilizopita nilikuwa naangalia video kwenye mtandao wa youtube. Nilikutana na video moja ya Patrick Bet David ambapo alikuwa anaelezea hatua nne za kupata utajiri mkubwa. Kitu kipya nilichojifunza kwenye video hiyo ni dhana ya (more…)