Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (231/360); Tumia hisia kueleweka.

By | June 19, 2022

#SheriaYaLeo (231/360); Tumia hisia kueleweka. Unapotumia maneno pekee kuelezea kitu, inakuwa vigumu kueleweka. Na pia unaishia kuibua ubishi ndani ya watu ambao hawatakubaliana na maelezo yako kirahisi. Lakini ukitumia hisia ambazo zinawanasa wengine, wanakuelewa kwa urahisi zaidi bila hata ya kuleta ubishi. Kwa kuwafanya watu wajisikie vile unavyojisikia wewe, unakuwa (more…)

2726; Huhitaji kuvumbua kitu kipya.

By | June 18, 2022

2726; Huhitaji kuvumbua kitu kipya. Kama unatengeneza chombo cha mwendo, tairi inabaki kuwa tairi. Huhitaji kuja na aina mpya ya uvumbuzi wa tairi. Hata utengeneze tairi kwa upya kiasi gani, itabaki kuwa ya duara. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye mambo mengi ya maisha yako. Mengi unayopitia kama changamoto au mkwamo (more…)

#SheriaYaLeo (230/366); Tumia utani kushawishi.

By | June 18, 2022

#SheriaYaLeo (230/366); Tumia utani kushawishi. Mabishano ni sumu kubwa kwenye ushawishi. Ukishaingia kwenye ubishani unaishia kutengeneza adui na hivyo inakuwa vigumu kumshawishi mtu. Ipo njia bora ya kuwashawishi watu ambayo ni kutumia utani. Pale watu wanapotoa shutuma kuhusu wewe, badala ya kuanza kwa kuwashambulia, unaanza na utani kwanza. Utani huo (more…)

2725; Una moto kiasi gani?

By | June 17, 2022

2725; Una moto kiasi gani? Dunia inaendeshwa na moto. Mwanga wa jua, ambao ndiyo unafanya maisha yote yawezekane hapa duniani unatokana na moto unaoendelea ndani ya jua. Nyota mbalimbali tunazoziona angani, ni mawe yenye moto na ambayo yapo kwenye kasi kubwa. Moto unasafisha kila kitu. Moto unaimarisha vitu. Moto unateketeza (more…)

#SheriaYaLeo (229/366); Tumia ubishi wao kuwashawishi.

By | June 17, 2022

#SheriaYaLeo (229/366); Tumia ubishi wao kuwashawishi. Kijana wa mfanyabiashara ya mikopo alienda kwa kiongozi wa dini akilalamika jinsi amejaribu kumshawishi baba yake azingatie misingi ya dini kama kusali lakini baba yake huyo alidai hana muda wa hayo mambo ya dini. Kiongozi huyo wa dini alikuwa anajua tabia za baba wa (more…)

2724; Siyo kuanza, bali mwendelezo.

By | June 16, 2022

2724; Siyo kuanza, bali mwendelezo. Ingekuwa kuanza kitu ndiyo mafanikio, kila mtu angekuwa amefanikiwa. Maana karibu kila mtu alishaanza kitu fulani kwenye maisha yake. Na watu wengi huwa na shauku na hamasa kubwa pale wanapoanza. Lakini haichukui muda mrefu shauku na hamasa hiyo vinayeyuka na wanakosa msukumo wa kuendelea. Huwezi (more…)

#SheriaYaLeo (228/366); Tumia maigizo na siyo maneno.

By | June 16, 2022

#SheriaYaLeo (228/366); Tumia maigizo na siyo maneno. Kutumia maneno kuwashawishi watu ni jambo hatari sana. Kwani watu huishia kuelewa kinyume na kile ambacho tumemaanisha. Maneno huwa yana nafasi kubwa ya kueleweka vibaya. Lakini pia maneno huwa ni rahisi kuwaumiza watu na kuleta hali ya kutokuelewana. Lakini maigizo huwa yanaeleweka moja (more…)

2723; Ukishapanda mbegu.

By | June 15, 2022

2723; Ukishapanda mbegu. Kila mmoja hapa anajua kitu kuhusu kilimo, maana tumepita mazingira ambayo kilimo ni jambo la msingi. Katika kilimo kuna kupanda, kupalilia na kuvuna. Huwezi kuvuna kama hujapanda, hivyo cha msingi kabisa ni kuhakikisha unapanda. Lakini pia unapopanda, huwezi kutegemea kuvuna hapo hapo. Lazima ujipe muda, uwe na (more…)

#SheriaYaLeo (227/366); Waachie watu hisia.

By | June 15, 2022

#SheriaYaLeo (227/366); Waachie watu hisia. Watu wengi huwa wanakazana kutumia maneno kuwashawishi watu. Iwe ni kupitia mazungumzo au maandiko. Wanasema mengi wakiamini baadhi yatakuwa na ushawishi kwa watu hao. Lakini maneno matupu huwa hayana ushawishi mkubwa. Badala yake yanawaacha watu wakiwa na wasiwasi. Kwa sababu watu wanaweza kuondoka na maana (more…)

2722; Wanadanganya, lakini tunawakubali.

By | June 14, 2022

2722; Wanadanganya, lakini tunawakubali. Umewahi kuangalia maigizo au tamthilia mbalimbali. Na katika hizo, kuna ambazo zilinasa hisia zako, ukajikuta ukifurahi na kucheka au kuhuzunika na kulia. Ulijua kabisa kila kilichokuwa kinaonyeshwa kwenye maigizo au tamthilia siyo ukweli. Kama ni mtu amekufa kwenye igizo au tamthilia unajua kabisa kwamba hajafa kweli. (more…)