Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (221/366); Epuka Mabishano.

By | June 9, 2022

#SheriaYaLeo (221/366); Epuka Mabishano. Mabishano huwa hayana manufaa yoyote. Hiyo ni kwa sababu kila mtu huwa anaamini maoni yake ni sahihi zaidi. Hivyo unavyobisha na kupinga maoni ya mtu, humshawishi, bali unamfanya azidi kuamini maoni yake. Kadiri unavyombishia mtu ndivyo anavyoacha kukusikiliza na kusimamia upande wake. Kama unataka kuwashawishi watu (more…)

2716; Nataka nikuoe/unioe.

By | June 8, 2022

2716; Nataka nikuoe/unioe. Pata picha, umekutana na mtu mahali kwa mara ya kwanza, humjui hakujui na hapo hapo akakuambia anataka akuoe/umuoe. Ni jambo ambalo litakushtua na kukushangaza. Iweje mtu akutake ufanye maamuzi makubwa hivyo wakati hata bado hamjajuana? Maamuzi ya kuoa/kuolewa na mtu huwa yanajengeka taratibu baada ya watu kuwa (more…)

#SheriaYaLeo (220/366); Zingatia maslahi yao binafsi.

By | June 8, 2022

#SheriaYaLeo (220/366); Zingatia maslahi yao binafsi. Njia ya haraka na ya uhakika ya kuteka akili za watu na kuwashawishi ni kuwaonyesha jinsi ambavyo kitu kinakwenda kuwanufaisha wao wenyewe. Maslahi binafsi ndiyo nguvu yenye msukumo mkubwa kwa wengi. Tukio muhimu linaweza kuwahamasisha watu mwanzoni. Lakini baada ya hamasa hiyo ya mwanzo (more…)

#SheriaYaLeo (219/366); Waweke kwenye hali ya kudhani.

By | June 7, 2022

#SheriaYaLeo (219/366); Waweke kwenye hali ya kudhani. Ili kuwafanya wengine wakufuatilie na hivyo kuweza kuwashawishi, unapaswa kuwaweka kwenye hali ya kudhani. Usiwape uhakika kwa kujua kila kitu kuhusu wewe.Kwani watu wakishakijua kitu na kuwa na uhakika nacho huwa wanakizoea, wanakichoka na kuacha kukifuatilia. Watu huwa wanachoshwa haraka sana na kitu (more…)

#SheriaYaLeo (218/366); Shinda kwa kutumia vitendo na siyo maneno.

By | June 6, 2022

#SheriaYaLeo (218/366); Shinda kwa kutumia vitendo na siyo maneno. Watu wengi huwa wanakazana sana kutumia maneno kwenye kuwashawishi wengine. Lakini watu huwa ni wagumu sana kushawishika na kubadilika kwa kutumia maneno. Kwa watu, matendo yana nguvu na ushawishi mkubwa kuliko maneno. Hivyo pale inapowezekana kutumia vitendo, usihangaike sana na maneno. (more…)

2713; Matamanio makubwa zaidi.

By | June 5, 2022

2713; Matamanio makubwa zaidi. Hakuna ubaya wowote kwenye kuridhika haraka na kile ambacho mtu umekipata. Lakini ili uweze kupata mafanikio makubwa zaidi, lazima mtu uwe na matamanio makubwa zaidi. Ni matamanio makubwa ndiyo yaliyoisukuma dunia na kuifanya kuwa bora zaidi ya ilivyokuwa huko nyuma. Ni watu ambao hawakuridhika na kile (more…)

#SheriaYaLeo (217/366); Tumia hisia kali.

By | June 5, 2022

#SheriaYaLeo (217/366); Tumia hisia kali. Pale unapotaka kuonyesha msisitizo wa kitu na kuwa na ushawishi mkubwa, unapaswa kutumia hisia kali. Hisia kali, hasa za chuki huwa zinaeleweka sana na kuwashawishi wengine. Hiyo ni kwa sababu zinakuwa ni hisia walizonazo ila hawathubutu kuziweka wazi. Hivyo pale wewe unapoziweka wazi, wanakuona kama (more…)

2712; Utakuja kushangazwa na matokeo.

By | June 4, 2022

2712; Utakuja kushangazwa na matokeo. Kitu kinachowakwamisha wengi kwenye kuendelea kuchukua hatua ni kutokuyaona matokeo haraka. Mtu anataka kupunguza uzito, anahamasika kufanya mazoezi. Anaanza mazoezi kwa siku chache, ila kila akipima uzito uko pale pale. Anajiambia haya mazoezi hayafanyi kazi na kuamua kuachana nayo. Mtu anataka kuongeza mauzo kwenye biashara (more…)