Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Kuwa Sehemu Sahihi Kwa Wakati Sahihi…

By | July 29, 2016

Moja ya vitu ambavyo unahitaji kwenye biashara ni kuwa na taarifa sahihi kwa wakati sahihi. Na taarifa hizi zitakuwezesha wewe kufanya maamuzi sahihi kwa pale ulipo kibiashara ili kuweza kusonga mbele zaidi. Mafanikio ya biashara yanategemea wakati uliopo na kile unachofanya. Kwa mfano mtu aliyekuwa anajua matumizi ya kompyuta wakati (more…)

BIASHARA LEO; Jinsi Ya Kuifanya Biashara Yako Kuwa BRAND.

By | July 28, 2016

Brand ni lile jina ambalo biashara inakuwa imejijengea kwenye jamii na wateja wake. Ni ile sifa ya kipekee ambayo biashara inayo na inajulikana na wengine. Coca Cola ni brand, unaposikia tu neno coca cola unajua ni kinywaji bora, hata kama hujawahi kunywa. Samsung ni brand, unaposikia neno samsung unajua ni (more…)

BIASHARA LEO; Ajiri Taratibu, Fukuza Haraka…

By | July 22, 2016

Mafanikio ya biashara yoyote yanatokana na falsafa ambayo biashara hiyo inaendeshwa nayo. Ukiangalia wafanyabiashara wengi wanaotokea kwenye nchi ambazo ni za kibepari, wana falsafa tofauti kabisa na wale wanaotokea kwenye nchi za kijamaa. Nchi za kibepari kama marekani, zina ushindani mkubwa sana wa kibiashara na hivyo watu kujali ubora wa (more…)

BIASHARA LEO; Kwa Mabadiliko Yanayoendelea Nchini, Ni Lazima Tubadili Mbinu Zetu Za Kibiashara Kama Tunataka Kufanikiwa.

By | July 21, 2016

Kumekuwa na kilio na malalamiko ya wafanyabiashara nchi nzima juu ya hali ngumu ya ufanyaji wa biashara. Tangu kumetokea mabadiliko ya uongozi kwenye nchi yetu Tanzania, kumekuwa na mabadiliko mengi yanayoendelea nchini. Mabadiliko haya yamebadili sana hali ya uchumi na hivyo kuvuruga mambo mengi ya kibiashara. Tunashuhudia biashara kubwa zikifungwa (more…)

Njia bora za kutatua hali ya kutoelewana baina yako na mteja wako.

By | June 13, 2016

Biashara zina changamoto mbalimbali katika uendeshaji. Zile biashara ambazo unaona zimekua na kufanikiwa, siyo kwamba hazina changamoto ila waendeshaji wa biashara hizo wanajua jinsi ya kukabiliana na changamoto za kibiashara wanazokutana nazo. Moja ya changamoto ambazo zinasumbua biashara nyingi ni hali ya kutokuelewana baina ya mteja na mfanyabiashara. Kuna nyakati (more…)

Sababu tatu kwa nini biashara nyingi zinakufa haraka.

By | June 6, 2016

Kati ya watu wengi wanaoingia kwenye biashara kila mwaka, ni wachache sana wanaoweza kuendeleza biashara zao na zikaweza kufikia ngazi kubwa ya mafanikio. Watu wengi wamekuwa wanaishia katikati na kufunga biashara zao. Na wale ambao hawazifungi, wanakuwa wanaziendesha bila ya faida au kwa faida kidogo kiasi cha kushindwa kuzikuza zaidi. (more…)

Mambo ya kuzingatia ili kupata wawekezaji kwenye biashara yako.

By | May 30, 2016

Mtaji wa fedha ni eneo muhimu kwa biashara yoyote. Ili uweze kuanza au kukuza biashara yako, mtaji wa fedha unahitajika. Inawezekana ukawa ni mtaji kidogo au mkubwa kulingana na wazo la biashara ulilonalo. Kwa wajasiriamali na wafanyabiashara, wengi hawana kiasi cha fedha cha kutosha kuanzisha au kukuza biashara zao. Na (more…)

Dhumuni kuu la biashara siyo kupata faida pekee.

By | May 23, 2016

Moja ya tofauti ya wajasiriamali na wafanyabiashara ni kwenye faida. Wafanyabiashara wanaongozwa na faida pekee, yaani wao wanaangalia ni kipi chenye faida na hivyo kukifanya. Lakini wajasiriamali wapo tofauti kidogo, wao hawaangalii faida pekee, bali wanaangalia mchango wanaoutoa kwa wengine. Wajasiriamali wanaangalia ni kipi ambacho kinakosekana na wanatafuta njia ya (more…)

Vitu vinne vinavyochangia thamani na kipato cha biashara yako.

By | May 16, 2016

Kujua thamani ya biashara yako na kipato unachoweza kuingiza kupitia biashara hiyo ni moja ya vitu muhimu unavyotakiwa kuzingatia. Na kama ukiweza kufanya hivi kabla hujaanza biashara yako unaweza kuianza ukiwa na mpango bora wa kutoa thamani kubwa na kutengeneza kipato kizuri.  Watu wengi wamekuwa wanaingia kwenye biashara na kufanya (more…)

Badilika au potea; aina mpya ya ushindani kwenye biashara.

By | May 9, 2016

Kama umewahi kuona biashara zinazofanya vizuri sana lakini ikatokea zikafa ghafla, unatakiwa kujua ya kwamba kifo cha biashara hizo hakitoki nje bali ndani ya biashara.  Na kwa biashara zote kinachopelekea biashara kufa siyo sababu za nje, bali sababu za ndani. Na hivi piia ndivyo ilivyo kwa mafanikio ya biashara, yanaanzia (more…)